Vijana na siasa ya Tanzania

Vijana na siasa ya Tanzania

REBEL

Senior Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
166
Reaction score
65
Nimekuwa nikitafakari hali ya siasa na mchango wa vijana katika maendeleo ya Jamii.

Mungu amenijalia kutembelea maeneo mengi ya nchi yetu kama mji magharibi, Unguja kusini, Mwanza, Arusha, Bukoba, Iringa,dodoma n.k .Na wimbo ni ule ule kuwa vijana hawadhaminiwi kabisa.

Suala moja la kwanza ninalotaka kulizungumzia ni wamachinga. Kitendo cha maaskari wa mji/ jiji kuwar vijana kwa kuwaibia na kuwabughudhi wamachinga kunawarudisha nyuma kimaendeleo vijana. Kwa mfano mwezi uliopita hapa mji magharibi, Zanzibar serikali imeamua mji uwe msafi. Na wao walichoamua ni kuwa wafanyabiashara ndio wanaochafua mji na wakaanza kuwakamata na kuwaghasi.
swali :Je hii ni haki?

Na hili si tatizo la hapa zanzibar tu bali ni chanzo cha migogoro kote bara kuanzia Mbeya, Mwanza, Arusha na miji yote mikubwa.Ni imani yangu kuwa sheria inabidi zitungwe ili kuleta maendeleo kwa watu wake na kutambua sekta zisizo rasmi na sio kunyanyasa vijana.

Kitu cha pili, ni wimbi la vijana wasio na kazi walio wasomi na wasio wasomi linazidi kuongezeka. Hili ni bomu ambalo serikali inalikuza kama Lowassa alivyosema. Tatizo wizara ya kazi na yule waziri mwizi wa kura Prof. Makongoro Mahanga wa jimbo la segerea hajui kuimudu wizara yake yuko tu kuuza sura.Simpendi huyu wazirikabisa kazi kukaa tu ofisini.

Sema katika haya yote kuna vitu vinavyonipa matumaini kwa kuona vijana wanamudu siasa vyema sana sana wa NCCR- Mageuzi na ChaDEMA. Vijana hao ni Mkosamali, Kafulila, Machali, Mnyika, Lema, Silinde. Wengine ni Wenje, Halima Mdee, Regia Mtema na Sugu. Sema wakaze buti na Mungu atawasaidia. Vijana waliotuangusha ni yule katibu mwenezi wa CCM Nape Nnauye na yule zero Lusinde hata na Makamba January, na kingwangala hawako kwa ajili ya vijana na wanaboa.

Vijana tutetee haki zetu na katiba mpya.sio tu kila siku tunaimba mapenzi tu.

Nawasilisha.
 
kweli kabisa mkuu,
inatakiwa kuwa taifa lisilokuwa na watu waoga!ukisahaelewa mpigania haki yoyote lazima akumbane na misukosuko basa woga unakaa pembeni kisha tunasonga mbele,hata kama chadema au NCCR wakiwa madalakani wakaleta ushenzi nao tunawang'oa tu
 
Wadau mjadala upo hewani sasa unaendele wale wenye acces na itv mnaweza mkaufatilia moja kwa moja.
 
Wanachotaka vijana ni mabadiliko ya uongozi wa serikali maana waliopo ni upuuzi mtupu! Tunataka tukibadilishe chama kinachoongoza serikali tusikilizie tena!
 
Vjana ni taifa la leo.ila aina ya vjana kama january makamba ni janga la kitaifa
 
Wakuu hii thread ili isipoteze mvuto wekeni updates sio wote wanaoangalia TV sasa.
 
Updates plz sio mnapiga porojo hapa kama rejao, leteni updates
 
lazima mabadiliko--hata kiranja wa darasa hubadilika kila mwaka----acha na watu wengine wakakusanye madaftari kwani nao wanazijua ofisi za walimu zilipo.
 
Kuna dogo limedai huu mpango wa kila kitu kufanyia maamuzi Dar wakati akili za watu zishachoka hakuna lolote,
Ushauri-yeye haamini kama Mungu alilazimisha Mara,Kigoma au Shinyanga ziwe Tanganyika. Anasema ni bora ziwe nchi halafu kuwe na shirikisho la Tanganyika.
Anaunga mkono CDM
 
memberz wengi kwenye huu mjadala wanahitaji vijana kushika hatamu ya uongozi kwani hata ukombozi kwenye nchi mbalimbali uliletwa na vijana.
 
Kuna motheri mmoja anadai nchi imeongeza vichaaa wengi kuliko zamani. Yeye toka aanze kupata akili ni majina yale yale ya viongozi waliokuwa madarakanimiaka ya sitini hadi leo ni watoto kama si wao.
Vijana amueni, ingieni ktk siasa
 
Huyu mdada hapa kwenye meza kuu kafunguka vizuri kwa kusema vijana waache kutumika kama makarai na waamini kua hata wao wanaouwezo wakusimama kwa miguu yao na kufanya maamuzi sahihi.
 
Mother anaendelea-vijana ni wa muhimu kwa sababu kila siku wanawaza mawazo mapya, ya nini kubaki na mizee inayosinzia ovyo halafu ikiamka inapiga mabenchi kuunga hoja bila kujua nini kiliongelewa?
 
mama anaendele kwa kusema kua hata jk nae atafute muda wakuongea na vijana sio kilasiku anaita wazee tu wanakuja kusinzia.
 
Deodatus-UDSM
tunahitaji mabadiliko lakini naomba madiliko haya ni lazima yawe na sura ya kuwakumbuka walemavu.
pia naomba mafisadi washughulikiwe, juzi juzi nimesikia redioni kuna waziri kanunua nyumba kwa mil zaidi ya 600 pesa ambayo inaweza kujenga shule kigogo mwizi bado analelewa.
Mabadiliko si lazima yaje kwa njia ya amani ni vizuri kutumia njia ya mapinduzi.
nchi zetu za afrika wazee wameng'ang'ania madaraka wamataka wafie pale. (hayo ni maoni ya kijana wa UDSM -ni mlemavu wa macho)
 
Deodatus-UDSM
tunahitaji mabadiliko lakini naomba madiliko haya ni lazima yawe na sura ya kuwakumbuka walemavu.
pia naomba mafisadi washughulikiwe, juzi juzi nimesikia redioni kuna waziri kanunua nyumba kwa mil zaidi ya 600 pesa ambayo inaweza kujenga shule kigogo mwizi bado analelewa.
Mabadiliko si lazima yaje kwa njia ya amani ni vizuri kutumia njia ya mapinduzi.
nchi zetu za afrika wazee wameng'ang'ania madaraka wamataka wafie pale. (hayo ni maoni ya kijana wa UDSM -ni mlemavu wa macho)

Sasa huyo mlemavu wa Macho kafunguka, hao wenye macho wakina Rejao bado hawajafunguka na wanona kila utumbo tunaofanyiwa na Mafisadi
 
Back
Top Bottom