Vijana mjifunze kupitia mwandishi Erick Kabendera

Kawe Alumni

JF-Expert Member
Mar 20, 2019
8,685
11,988
Vijana wa kiafrica wamekuwa wahanga wakubwa na siasa za uchumia tumbo kwa Viongozi wa Africa wenye tamaa ya madaraka.

Kwa kuwa vijana Wengi wanakuwa wametoka vyuoni hawana mwelekeo wa maisha wanarubunika na kila fursa inayojitokeza mbele yao ili mradi wapate kushibisha tumbo.

Hali ambayo unawapelekea katika hatari pale wanapojikuta wamevunja sheria za Nchi na kuingia matatani.

Vijana wanakuwa wabeba mabegi wa Wanasiasa walaghai. Wanasiasa wao tayari wameshajijenga kiuchumi wengi wameficha mapesa nje ya Nchi, wengi wana visa mkononi akikosea anakimbilia nje ya Nchi anakuacheni nyie vijana mnaozea mahabusu.

Pia mwanasiasa akiona kesi uliyofanya inaweza kumuharibia jina kisiasa anakutelekeza mahabusu upambane na hali yako.

Wanasiasa wanakuwa wanagombana wanapokuwa wameshika maik wanahutubia tu,ila wengi nyuma ya pazia ni marafiki wanakunywa wain pamoja. Nyie mnaokesha mtandaoni kuwapigania mnapoteza muda muda tu.

Vijana mjifunze kwa Kabendera mslighaiwe na wanasiasa wasaliti wa Nchi yetu wenye tamaa ya madaraka mkipata matatizo mnatelekezwa mahabusu.

Vyama vingi vya upinzani Africa ni kwa ajili ya ujasiriamali na si kusaidia Mwananchi

Tuwakimbie hawa Wanasiasa waongo

Bahati nzuri tuna Rais anayeongoza bila kujali Chama cha mtu haina haja kukaa vyama vya upinzani
 
Mnaendekeza propaganda za kijinga kwenye mambo ya msingi, kusema Kabendera ametumika na wanasiasa una ushahidi?

Mimi nasema mnabambikia watu makosa ya uongo nina ushahidi, ndio maana DPP kamuondolea kosa la kumiliki genge la uhalifu baada ya kuona hakuna uthibitisho wa kumtia hatiani.

Hata hayo ya Uhujumu Uchumi nayo siwezi kukiri kweli Kabendera alikutwa na hatia kwasababu mahakama haikuwahi kumhukumu kwa kosa hilo.

Hivyo ulichoandika hapa ni hisia tu zisizo na ushahidi wala maana yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya Ndio Mawazo tunayohitaji, vijana tumechezewa sana na wanasiasa wa upinzani hawajatusaidia kwa lolote

Bora umetualimisha tuwakimbie hawa Wanasiasa wachumia tumbo
 
Mkuu mtu kakiri kuwa amefanya makosa Hayo we ubabisha?

Mtu ambaye ni maskini angekubali hayo makosa? Pesa angetoa wapi? Na tunaambiwa tayari amelipa million mia jd41,
 
jd41, Tuambie hizo kampuni alifungua kwa ajili gani?
Huduma gani au biashara gani amefanya tangu kusajili kampuni hizo?

Je, kazi alizofanya, zinaendana na malipo ya bilions of money alizolipwa?

Kwa nini kagoma kutaja akaunti zake zote?

Kwa nini ameshindwa kutaja waliomtumia pesa?

Mwanzoni nilidhani anaonewa tu lkn alistahili misukosuko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli IQ yako ni ndogo sana, yaani unaanzisha uzi kisha wewe mwenyewe unajibu.

Huu ni mfano wa akili za wanachama wa chama cha mapinduzi.

Akili zao zilishapinduka zamanii!!
Haya Ndio Mawazo tunayohitaji, vijana tumechezewa sana na wanasiasa wa upinzani hawajatusaidia kwa lolote

Bora umetualimisha tuwakimbie hawa Wanasiasa wachumia tumbo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza kabisa, Tanzania hakuna vyama vya siasa, kuna magenge ya kutafuta ulaji.

Pili, hilo halina maana kwamba vyama vilivyopo haviwezi kutumika kuongeza demikrasia, elimu na ufanisi.

Tatu, Kabdendera ni kama mtu aliyeshikwa na magaidi, akaambiwa, kubali dini yetu, usiokubali tunakuua.

Mtu huyo akikubali dini hiyo kwa muda ili tu ayanusuru maisha yake, siwezi kumlaumu. Hiyo inaweza kuwa military streategy inayoitwa "tactical retreat". Style hii kwa sisi tuliyemsoma Shaka Zulu na upiganajibwake wa kurudi nyuma, kujioanga uoya na kumzunguka adui, kisha kumpiga vizuri, haiwezi kutushangaza sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya Ndio Mawazo tunayohitaji, vijana tumechezewa sana na wanasiasa wa upinzani hawajatusaidia kwa lolote

Bora umetualimisha tuwakimbie hawa Wanasiasa wachumia tumbo
Wa ccm wamukusaidia wewe kuwadi na walamba viatu wenzio. Kuna mwanaccm aliyesaidia mtu nchi hii? Wezi wakubwa msiojali maisha ya watu maskini zaidi ya kuwatumia kwa faida binafsi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom