Vifurushi Vya Siku (24hours): Dstv, Startimes, Zukutv n.k

Vifurushi Vya Siku (24hours): Dstv, Startimes, Zukutv n.k

Swizzy

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2016
Posts
773
Reaction score
516
habari wanajukwaa!!

kila siku nimekuwa nikijiuliza ni kwanini haya makampuni ya tv (ving'amuzi) kwenye vifurushi vyao huwa wana weka tulipie kwa mwezi/nusu mwezi tu?.

Kwanini wasiweke vifurushi vya kulipia kwa siku ili kuwasaidia watanzania wengi wanao shindwa kulipia kwa mwezi/nusu mwezi nao waweze kufurahia hivyo vifurushi kwa kulipia kwa siku, kama wanavyo fanya kwenye mitandao ya simu (kuna mabando ya siku/wiki/mwezi/mwaka). Startimes kuna kipindi waliweka huduma ya kulipia kwa siku (kwenye kifurushi chao cha mambo kama sikosei tulikuwa tunalipia Tsh 133 per day) lakini huduma hii kwa sasa haipo tena.

Kama wahusika wana usoma huu uzi naomba walifikilie hili la kuweka vifurushi vya kulipia kwa siku. Saizi imefikia hatua ya watu wengi kutolipia ving'amuzi vyao, utakuta nyumba imefungwa dishi juu la dstv au startimes au zuku n.k ukifuatilia unakuta king'amuzi hakijalipiwa kwa mda mrefu sana . kwa kutu rahisishia sisi watanzania (wabahili wa kutoa mwisho wa mwezi) tunaomba mtuletee vifirushi vya kulipia kwa siku.

......Kwa mwenye Nyongeza/mawazo kuhusiana na hawa wamiliki wa hivi ving'amuzi una karibishwa hapa....
 
continental wana cha siku,wiki,mwezi chasiku ni sh 1000
 
Kaka umeongea la maana. Mimi ni bachelor kwangu naishi mwenyewe. Huwasishindi kwangu. Narudi jioni tu. Na huwa nasafiri at least kwa wiki mara moja.

Kifurushi nachonunuaga cha dstv ni kile cha family. Sasa ni elf 42. Chanel nazoangalia ni discovery, M-Action, sound city, E.A maisha magic basi.

Hiki kifurushi kina zaidi ya chanel 70. So chanel 60 kwangu hazina maana.

Sasa wangeleta vifurushi mtu ananunua chanel anazotaka yeye. Huwezi kuwa na Tv moja chanel 300. Unaweza ziangalia zote.

Watuletee vfurush kma vya cm. Ni kma mtu unaweza nunua kifurush cha calls tu au text tu au internet tu.
 
Kaka umeongea la maana. Mimi ni bachelor kwangu naishi mwenyewe. Huwasishindi kwangu. Narudi jioni tu.
ma bachelor tupo wengi mfano kama mimi kwa mwezi huwa naangalia tv mara2 au3 hivi...sasa hivi vifurushi vya mwezi vina nitesa kweli mimi nina Dstv
 
hata kama sio bachelor nani zama hizi anashinda nyumban??? Hata hivyo naamini huko kote tutafika tu
 
Naunga mkono hoja.

Nshawahi kulipia DSTV kifurushi kikubwa baada ya siku mbili nikasafiri nikarudi baada ya mwezi.

Wangeweka vifurushi vya siku na week.
 
Naunga mkono hoja.

Nshawahi kulipia DSTV kifurushi kikubwa baada ya siku mbili nikasafiri nikarudi baada ya mwezi.

Wangeweka vifurushi vya siku na week.
ha ha haaa!!! huko ulikoenda ulikuwa unakumbuka kifurushi chako tu.
 
hata kama sio bachelor nani zama hizi anashinda nyumban??? Hata hivyo naamini huko kote tutafika tu
Kitu pekee nina uhuru nacho kwangu ni gari tu maana Tv nahusika kulipia tu na nikilipa wife na watoto hawataki niguse remote!poor me!
 
Back
Top Bottom