Vifurushi vya internet

Vifurushi vya internet

Arnomos

Member
Joined
Jun 5, 2015
Posts
30
Reaction score
25
Hivi jamani, pengine mi ndo ambaye sielewi labda ama vipi nitaomba mnieleweshe. Hivi kwanini siku hizi vifurushi vya Internet vinapanda bei sana? Yaani kwa sasa hivi kifurushi cha bei ya chini kabisa cha Internet kwa mitandao karibu yote ni shillingi 3,000 ambapo hapo unapata MB 700 kwa Zantel na Voda unapata Mb 500 vyote hivyo ni vya wiki.

GB 1 kwa wiki sasa hivi inauzwa kuanzia shillingi 5,000 kwenda juu, na siku hizi ukinunua Kifurushi chochote cha kawaida tu unapewa either Mb 1 hadi 10 kwa mitandao tofauti hata kama ungenunua cha Mwezi ujazo wa data unakuwa unafanana wakati zamani kwa shillingi 500 tulikuwa tukijiunga na Extreme tunapewa dakika, sms na data mb 100, lakini siku hizi sijui hata nini kimetokea.

Nikitafuta sababu mtandaoni ni kwanini sipati majibu ya moja kwa moja, nakutakana na nukuu (quotes) chache tu zinazodai kuwa kodi wanazotozwa ndizo zinazofanya wapandishe bei na wao, sasa hii serikali ya Tanzania itaacha lini ku survive kwa kupitia kodi tu, kwanini yenyewe kama entity isianzishe miradi yake kama biashara hivi then ikawa inajipatia faida huko kuliko kuishi kwa kodi tu, mfano huu UDART (Mwendokasi) si mradi wao, sasa kwanini wasianzishe project zao wenyewe zitakazo waingizia hela tofauti na kodi, maana kwa style hii ni kumuumiza Mtanzania ambaye gharama zote hizo zinamrudia yeye. Ofcourse kodi zitozwe lakini zisiwe excessive kiasi hiki jamani, hebu imagine kutokea 3,000 hadi 5,000 kwa GB 1 jamani hivi ni kweli kabisa.

Na vishindo hivi vyote hutokea baada ya bunge la budget yaani lenyewe halijuagi kuacha kodi zilizopo, linachojua ni kupandisha kodi kila mwaka wa fedha, na hizi bei za sasa hivi kwa mwaka mwingine wa fedha wataongeza kodi tena, sasa hebu niambie hiyo ni nini.

Hivi wanajua kuwa kodi nyingi nazo zina madhara yake, thamani ya fedha inashuka, kama ningeweza kupata kitu fulani kwa 10,000 basi nitahitaji 15,000 ili kuweza ku afford kitu ambacho hapo mwanzo ningeweza kukipata kwa 10,000.

Jamani serikali, jitahidini mpate project za kuwaingia pesa kama wafanya biashara wanavyofanya biashara na kupata faida basi nyie pia fanyeni hivyo kwa maana hayo sio maisha bora kwa kila mtanzania, yaani hapa nawaza huo mwaka mwingine wa fedha sijui kama hatujanuna GB 1 kwa 10,000 bundle ya wiki tu.
 
Halotel
 

Attachments

  • 1474739892897.jpg
    1474739892897.jpg
    27.6 KB · Views: 98
Pole mkuu hamia halotel
Hata hao watapatwa tu, na halotel labda line ya chuo ndo ina bundle zinazotazamika amd then nikisema nihamie halotel basi nitajikuta nina line jumla saba za simu na hapo bado sijajumlisha line nazotumia kwenye modem, yaani nina tabia kila nikiona sehemu fulani ina bundle za nafuu nakimbiliaga huko na nikishafika sikai sana nao wanapandisha tena. Yaani kama kodi inatozwa kwa voda, basi hata tigo, airtel na wengine watakuwa wanatozwa hivyo hivyo.
 
Ofcourse menu yao ni impressive sasa nao wakipandisha which they will nitaenda wap, na sawa, labda mimi nitahamia halotel, does that mean kila mtu naye ahamie halotel just for the internet bundles.
 
Hii hapa hatari
 

Attachments

  • 1474742693810.png
    1474742693810.png
    11.3 KB · Views: 56
hiyo ni ofa kwa walio na simcard za Halotel, Vipi kwa wasio wanafunzi wanatoa ofa gani tofauti na hii mitandao mingine?

Jadili kama mtumiaji wa kawaida na si kundi maalum!
Hiyo simcard hata kama si mwanachuo unapata

daily packages kwa laini ya kawaida
500=350 Mbs
1000=1.sth GB
1500=2.sth GBS speed kubwa >10Mbps
 
Hivi jamani, pengine mi ndo ambaye sielewi labda ama vipi nitaomba mnieleweshe. Hivi kwanini siku hizi vifurushi vya Internet vinapanda bei sana? Yaani kwa sasa hivi kifurushi cha bei ya chini kabisa cha Internet kwa mitandao karibu yote ni shillingi 3,000 ambapo hapo unapata MB 700 kwa Zantel na Voda unapata Mb 500 vyote hivyo ni vya wiki.

GB 1 kwa wiki sasa hivi inauzwa kuanzia shillingi 5,000 kwenda juu, na siku hizi ukinunua Kifurushi chochote cha kawaida tu unapewa either Mb 1 hadi 10 kwa mitandao tofauti hata kama ungenunua cha Mwezi ujazo wa data unakuwa unafanana wakati zamani kwa shillingi 500 tulikuwa tukijiunga na Extreme tunapewa dakika, sms na data mb 100, lakini siku hizi sijui hata nini kimetokea.

Nikitafuta sababu mtandaoni ni kwanini sipati majibu ya moja kwa moja, nakutakana na nukuu (quotes) chache tu zinazodai kuwa kodi wanazotozwa ndizo zinazofanya wapandishe bei na wao, sasa hii serikali ya Tanzania itaacha lini ku survive kwa kupitia kodi tu, kwanini yenyewe kama entity isianzishe miradi yake kama biashara hivi then ikawa inajipatia faida huko kuliko kuishi kwa kodi tu, mfano huu UDART (Mwendokasi) si mradi wao, sasa kwanini wasianzishe project zao wenyewe zitakazo waingizia hela tofauti na kodi, maana kwa style hii ni kumuumiza Mtanzania ambaye gharama zote hizo zinamrudia yeye. Ofcourse kodi zitozwe lakini zisiwe excessive kiasi hiki jamani, hebu imagine kutokea 3,000 hadi 5,000 kwa GB 1 jamani hivi ni kweli kabisa.

Na vishindo hivi vyote hutokea baada ya bunge la budget yaani lenyewe halijuagi kuacha kodi zilizopo, linachojua ni kupandisha kodi kila mwaka wa fedha, na hizi bei za sasa hivi kwa mwaka mwingine wa fedha wataongeza kodi tena, sasa hebu niambie hiyo ni nini.

Hivi wanajua kuwa kodi nyingi nazo zina madhara yake, thamani ya fedha inashuka, kama ningeweza kupata kitu fulani kwa 10,000 basi nitahitaji 15,000 ili kuweza ku afford kitu ambacho hapo mwanzo ningeweza kukipata kwa 10,000.

Jamani serikali, jitahidini mpate project za kuwaingia pesa kama wafanya biashara wanavyofanya biashara na kupata faida basi nyie pia fanyeni hivyo kwa maana hayo sio maisha bora kwa kila mtanzania, yaani hapa nawaza huo mwaka mwingine wa fedha sijui kama hatujanuna GB 1 kwa 10,000 bundle ya wiki tu.
Niliongelea hili kua tatizo internet kwetu ni anasa wakati hukombele ukianza na Asia hii kitu ni kama nyenzo muhimu ya kupanda kuelekea maendeleo hivyo wao wameifanya kua very cheap na inavyoendea huko mbele itakuja kua free service kabisaa!Mfano mzuri Nchini Malaysia tuliopata Uhuru nao Kipindi kimoja
 
Back
Top Bottom