Vifaru vya jeshi vyawashitua wananchi

Vifaru vya jeshi vyawashitua wananchi

Siku ya Muungani yakaribia, hayo ni mazoezi nadhani
 
hivi wale faru bado wapo au wametoweka moja kwa moja?
 
Hivi huwa si wana magari makubwa yale kwa ajili ya kubebea vitu kama hivyo?!

- au yalikuwa mabovu?

- au ni show-off tu ili "tuwajue" vizuri?!

- si salama sana kusafirisha vitu ka hivyo wazi wazi...
 
Si kila kitu mnakimbilia kuweka JF jamani

- na si kila kitu kinasafirishwa kama unasafirisha Mahindi kutoka Kibaigwa!...

- kama waliamua kuyaweka wazi maana yake waliona hakuna madhara na sisi tunajadili wazi wazi kama hivi.
 
kweli kuna watu sijui hamwezi kufikir? Hvi kuna umuhim gan wa kutoa taarifa kama hiz?? Kwan ww ni msemaji wa jeshi?? Unastahiri kufichwa na kufanyiwa mahojiano ili siku ningne ukome kubweka

Acha ubabe.
 
Wewe si mtanzania ndiyo maana unavujisha siri za jeshi letu ili ndugu zako waliokutuma wajue. Mzalendo wa kweli haropoki hovyohovyo ipo siku utakuja sema kuwa wanajeshi wetu wamejificha pale wanataka kumpiga adui. Ili uishi salama tz acha kabisa kuropoka hovyo kuhusu vyombo vyetu vya ulinzi.
 
Unamtazamo wa kizamani sana kuhusu upashanaji habari. Enzi hivi za digitali ni tafauti na Enzi zilee za mwalimu ambako kila kitu ni Siri na ukisema unawekwa kizuizini.

Umesema kilekile nilichofikiri.

Kuna watu wana uzalendo wa kizamani.

Mtu kauliza, that shows an inquisitive mind. Waswahili wamesema kuuliza si ujinga.

Hizi habari za kutaka "self censorship" kwenye kitu chochote kinachofanywa na jeshi kitafanya wajanja watumie jeshi na "usalama wa taifa" kufanya ufisadi wao wote.

Utafanya nini? Ukiulizwa utaambiwa "hilo ni suala la usalama wa taifa".

Utasema nini na wewe ushafanya jeshi na usalama wa taifa some "holy cow"?

Kama.jeshi limeamua kufanya gwaride lisilo rasmi, pengine thtead kama hii inalisaidia kuwapasha habari wananchi kwamba jeshi lipo, kwa nini mnataka kitu ambacho jeshi halijaficha kiwe siri hapa JF, ambapo tunajivunia uhuru wa kujieleza?

Wanaotaka kujua nyendo za jeshi letu ambao inabidi tuwahofie ni wenye satellites zinazoweza kuona mwendo wa kifaru kutoka anga za juu. Jeshi linajua hilo, na kama lingetaka usiri lingesafirisha vifaru vyake kwanusiri zaidi

Hawa watu wanaotaka self censorship inabidi wasome motto ya JF.

Jamiiforums. Where We Dare To Talk Openly.
 
Eti mfumo wajitali kila kitu wazi....!!?. Uhuru bila utii ni uwendawazimu. Kwa tabia hii inaonekana huna hata chembe kidogo ya uzalendo naamini utakuja kuripoti kuwa rada ya tanzania mbovu bila kujua madhara ya kuripoti habari kama hii ila tambua majeshi yanafanya kazi ya kulinda nchi sasa ukiwa unaanika siri zao ujue kabisa unayadhohofisha kwa adui anayetunyemelea. Acha kutumia vibaya mtandao maana usalama wa nchi si jambo la mchezo kama simba na yanga yaani unataniana mpaka mchoke.
 
Kumbe wakati sisi tunalala bila chupi na wake zetu kuna watu wapo kazini hawalali.

Uwe unaweka kabukta basi hata laini ili hata akiingia jambazi unapambana . utakuja kupambana uchi na watatake advantage watakukata naniiiiii mkuu
 
Ni sahihi wale tuliokwenda JKT hatuogopi vitu kama hivyo yaonekana huyu bwana wala hata mgambo hajapitia
 
Ukiona zana nzito namna hiyo zinasafirishwa mchana na kutofunikwa ujue ni ujumbe unatumwa kwa raia kwamba jeshi liko alive and well

Viva Jwtz!
 
Umesema kilekile nilichofikiri.

Kuna watu wana uzalendo wa kizamani.

Mtu kauliza, that shows an inquisitive mind. Waswahili wamesema kuuliza si ujinga.

Hizi habari za kutaka "self censorship" kwenye kitu chochote kinachofanywa na jeshi kitafanya wajanja watumie jeshi na "usalama wa taifa" kufanya ufisadi wao wote.

Utafanya nini? Ukiulizwa utaambiwa "hilo ni suala la usalama wa taifa".

Utasema nini na wewe ushafanya jeshi na usalama wa taifa some "holy cow"?

Kama.jeshi limeamua kufanya gwaride lisilo rasmi, pengine thtead kama hii inalisaidia kuwapasha habari wananchi kwamba jeshi lipo, kwa nini mnataka kitu ambacho jeshi halijaficha kiwe siri hapa JF, ambapo tunajivunia uhuru wa kujieleza?

Wanaotaka kujua nyendo za jeshi letu ambao inabidi tuwahofie ni wenye satellites zinazoweza kuona mwendo wa kifaru kutoka anga za juu. Jeshi linajua hilo, na kama lingetaka usiri lingesafirisha vifaru vyake kwanusiri zaidi

Hawa watu wanaotaka self censorship inabidi wasome motto ya JF.

Jamiiforums. Where We Dare To Talk Openly.

Well - said & sayings...

"pokea Likes"

"Kiranga"
"Shitwiku"
"Rapherl"
"andybird314"
"mizambwa"
"KakaKiiza"
"peho"
 
Siku ya Muungani yakaribia, hayo ni mazoezi nadhani

24.jpg

Ndege za kivita zilizoonyeshwa kwenye sherehe hizo, zikilinda Ndege ya Rais katika maonyesho ya Ndege yaliofanyika kwenye Kilele cha Maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano.
23.jpg

Kikosi cha Wanamaji kikionyesha vifaa vya jeshi la wananchi kitonga cha wanamaji.
22.jpg

Baadhi ya silaha zakijeshi zikipitishwa mbele ya umati wa wananchi.
35.jpg

Ndege za kijeshi zikipita kwa speed ya ajabu juu ya uwanja wa Uhuru.
 
Back
Top Bottom