mkuu nami nipo hatua hiyo ila dar(kariakoo) naiogopa mbaya kwa vtu fake i was even thinking kwenda Kampala besides nasikia kule bei nzuri sana na quality unapakia ndani ya kampala coach hamna longolongo ya ushuru wala nn boda,ama nairobi,wadau acha watujuze kama iko duka ya uhakika twende tusipeleke pesa nje
Wakuu nadhani tatizo lililopo ni sisi wajenzi kwa kuwa tuko busy basi huwa tunawaamini mafundi wakatunulie vifaa. Nakwambia mafundi wengi lazima atakuchakachua na hata ukiongozana nae atakuwa amekwisha kwenda kuongea na wenye maduka ili wale chao cha juu. Na mbaya zaidi wakati mwingine ukienda wewe mafundi anakwambia ohooo mimi sikutaka kifaa hiki. Ukweli ni kuwa mafundi wengi wana njaa kali na ndo chanzo cha wateja wengi kulia. Am sure kuna product nzuri tu Kariakoo na ambazo nina uhakika nazo especially on that shop.
Contact 0714779110.tuna kampuni inayojihusisha na electrical instillation,tuna maduka yetu yenye vifaa vya kuaminika kama vile switch,circuit braker,taa za aina mbalimbali,na tunatoa huduma za za ukarabati na service za umeme kwenye majengo mbalimbali hapa dar.
Asante mkuu kwa kontakti ina nina swali, products zenu mna import kutoka nchi gani?
rmashauri; Asante mkuu kwa kontakti ina nina swali, products zenu mna import kutoka nchi gani?
Mkuu naona una wasiwasi na vitu toka China, siyo? Mpaka kiandikwe made in England/UK, Germany, Italy, nk ndo angalau uwe na imani na ubora wake. Kuna vitu vingi sana vinatengenezwa China bado vipo Imara, ukizingatia China inatumiwa na nchi nyingi zilizoendelea kama sehemu ya kuzalishia vitu kwa bei nafuu na kwenda kuviuza nchini mwao kwa bei kubwa. Zaidi ya asilimia 90% ya vitu vinavyouzwa US vimetengenezwa China na hayo makampuni ya US yaliyoamishia viwanda vyao China kuzalisha kwa gharama nafuu. Hivyo vitu vinavyozalishwa siyo vyote vinauzwa US, vingine vinaenda kwenye masoko mbalimbali duniani Ikiwemo Africa/Tanzania. Siyo kwa US tu wanaofanya hivyo bali kwa capitalist countries nyingi wanajaribu kupunguza gharama na kuongeza ushindani kwenye bei za kuuzia.
Nenda kariakoo mtaani wa Narung'ombe duka la Tropical wana vifaa vya ukweli, ushauri bure na guarantee ya kutosha. Nenda mwenyewe ukiweza kwani Mafundi lazima wale cha juu.
asante sana mkuu. Hawa jamaa ndo wenyewe kwa hapa dar wana vifaa vyenye quality ya juu na products zao ni make za australia.
Nami ndio nimefika hatua hiyo. Wauzaji, tunaomba mawasiliano yenu.Wakuu ni duka gani kwa Dar es Salaam wanauza genuine (made in Europe if possible) wiring materials na vikorombwezo vyake kama vile soketi, swichi n.k. Niko kwenye hatua ya kufanya wiring kwenye nyumba mpya.
Natanguliza shukrani zangu.