TUNASEMA WAMEKOSEA HILI AMA LILE. INGELIKUWA KWELI TUNA AKILI HIVI HATA KUSHAURI HAWA WAFANYABIASHARA AMBAO HAWAKUANZA LEO KAMPUNI ZAO, TUNGELISHAKUWA NA MAKAMPUNI YETU NA WASINGEWEZA KUJA KUFANYA BIASHARA HAPA.
Ikiwa umeshindwa kuanzisha hata genge, usifikiri unaweza kumshauri mtu mwenye kampuni kubwa ya miaka. Hujui hata ana mtaji kiwango gani, na bajeti yake ya mwaka huu ni ipi, na ana malengo gani kwa miaka hii mitano, utawezaje sasa kumshauri shughuli zake za uendeshaji? HAWAJAKOSEA, NI WEWE UNATAMANI ZAIDI YA MASTAHILI YAKO. Ukweli ni wazoefu hao na hiyo shughuli yao kiasi wanajua kila mtu wanayemuajiri ana thamani gani kwa mapato yao, na watakulipa accordingly.
Ikiwa wewe ni nusu-mungu kwa maendeleo ya kampuni yao, haitajalisha hata kama una funza miguuni, utalipwa sawa na umuhimu huo. Na ukiwa mtu tu wanayeweza kumbadili na mtu mwingine, you will also be paid low. USILALAMIKE UTAFIKIRI USIPOKUWEPO HAITAENDELEA. haitakusaidia. JIPE THAMANI KWANZA, KUWA MTU UNAYETAFUTWA, SIO UNAYETAFUTA. HILO NDO JIBU LA MSHAHARA MDOGO. Bahati nzuri huhitaji shule kuwa hivyo, unahitaji tu kuwa humo ndani, na umeshaingia kwa kuajiriwa nao.
Ajiri house girl tu ndo uone maana ya kulipa watu mishahara. Halafu ndo utajua.