Vidonda vya koo vinanitesa

Sawa mkuu
 
Kuna huu ugonjwa unaitwa LPR Laryngopharyngeal Reflux Disease. Nimesoma tatizo lake linafanana vile vile na huu ugonjwa. Huu ugonjwa unaweza kumpata mtu yeyote ila kwa watu wazima unazidishwa na kula vyakula vya spicy and acidic food. Dawa inayoshauriwa ni Dexlansoprazole 60 mg capsule. Ila kikubwa epuka vyakula visababishi, avoid alcohol and quit smoking. Usile masaa matatu au mawili kabla ya kulala na usilalie mto mkubwa. chacha mwewe soma kuhusu huu ugonjwa uone kama unafanana na wewe unavyojisikia.
 
Mbona unamshambulia sana, una uhakika gani kama tatizo hilo linatokana na kuzama chumvini? Tujifunze ustaarabu jamani, hebu imagine ndio wewe unaomba ushauri halafu ndio unashambuliwa namna hii, would you be happy?. Halafu jifunze kuandika maneno ya Kiingereza vizuri kama hujui ni vizuri ukaandika Lugha yetu ya taifa tu
 
Wacha nitajaribu mkuu maana mpaka sasa sauti yangu INA shida na masikio pia wakati mwengine yanauma
Pole sana mkuu, Mungu akuponye, kama ni mkristu nakushauri uwe unafanya na maombi pia wakati mwingine shetani huwa anachezea afya zetu.
 
Nenda hospitali pima vipimo vya afya yako. Magonjwa kwa sasa ni mengi na kama dawa zote hizo hazionyeshi mafanikio, vipimo ni muhimu
 
ni dalili pia ya mtu anasumbuliwa na virus
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…