Vidonda mdomoni husababisha sana maumivu makali pamoja na kumfanya mtu asiweze kuongea vizuri na watu.Vidonda hivi husababishwa na kutafuta kwa muda mrefu hasa bigijii au kitu chochote, uvutaji wa sigara,maambukizi ya virusi, bakteria na fungasi sambamba na ukosefu wa madini na virutubisho vya folic, zinc, vitamin c,vitamin B12, na madini ya chuma.
Vidonda hivi huwaathiri sana watu wengi na hutokea sana kwenye lips, ulimi , mashavu, kingo na kuta za meno ambapo pia huweza kusambaa hadi kwenye koromeo endapo havitatibiwa mapema.
Pamoja na kutembelea hospitali ambapo dawa kama za antibiotiki, fangasi, virusi na zile za kupunguza maumivu na uvimbe huweza kutolewa kulingana na ukubwa wa tatzo pia unaweza kufanya yafuatayo kujitibu nyumbani
Epuka vyakula na vinywaji vya moto au baridi sana kwani huchelewesha kupona kwa vidonda
Kunywa juice ya matunda mbali mbali itakayokuwezesha kupata virutubisho na madini ambayo huongeza kinga ya mwili
Kunywa maji mengi kila siku ambayo sio ya moto wala baridi
Piga mswaki mara kwa mara na taratibu ili kuepuka kukwangua na kutonesha sehemu zenye vidonda
Kula sana matunda asa machungwa, machenza na malimao kwani yana kiasi kikubwa cha vitamin ambayo huongeza kinga ya mwili. Pia yana asidi ambayo inaweza kuua wadudu wanaokuwepo mdomoni
Unaweza kununua pia Maltivitamini dawa yenye mchanganyiko wa virutubisho vingi ambavyo huweza kusaidia kurudisha kinga ya mwili katika hali ya kawaida
Kama vidonda vinaambatana na maumivu makali tumia dawa ya kutuliza maumivu au kuweka barafu ambayo hupunguza maumivu kwa muda
Tumia Asali ambayo husaidi kuua vimelea, kuponya makovu na kulainisha sehemu zenye vidonda pakaa asali kwenye vidonda asubuhi mchana na usiku.
Kunywa maji ya nazi(madafu) ambayo upoza mwili na huua wadudu hatari mdomoni sambamba na kupaka mafuta ya nazi kwenye kidonda ili kupona haraka.
Kumbuka vidonda visivyopona kwa muda zaidi ya wiki mbili vinaweza kuashiria tatizo kubwa na sugu mwilini hivyo inakupasa kufika hospitali ambapo utapewa dawa za bakteria, fungasi, virusi au dawa nyingine zozote kulinga na ukubwa na visababishi vya tatizo.
Usipo pona nitafute kwa wakati wako nipate kukutibia upate kupona.
Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu.
Kamauone daktari wa kinywa na meno kwa ushauri mzuri wa kitabibu lakini unawez pia kutumia "Medi oral solution " nidawa ya kusukutua kinywa,pamoja na "Daktarin oral Gel" Kwa upande wa fizi kutoa damu ni ishara kuwa kuna kitu hakiko sawa kinywani,take antibiotic to manage it,medicine like Ampicloxacillin ni dawa nzuri tu ,na kwa upande wa homa tumia panadol tu. Narudia tena ,nenda hospital kamuone daktari wa kinywa na meno.
Opthous/stress ulcers
Zinatokea zinawasumbua wengi mainly mwili unakua hypersensitive
Use of anti hypersensitive kumodulate body immunity unafanya mzuri
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.