Video: YESU wewe na Ev Mhugo Hantish

mhugo hantish

Senior Member
Apr 21, 2015
135
33


WIMBO: YESU WEWE
Na Ev Mhugo Hantish (The sound of worship)

Autro
Mmmmh! X2

PREACHES
"Ndugu yangu, jiulize wewe mwenzangu bila Yesu ungekuwa wapi leo hii. Bila shaka hujui, hata mimi sijui"

VERSE 01
Ndege wa angani wanajua uweza wako.
Nasi wa ardhini tunajua matendo yako,
Hata viumbe vya majina vinajua miujiza yako,
Kuwa (umejawa na neema na rehema tele X2) Baba.

CHORUS
Bila Yesu wewe ningekuwa wapi mimi (bila Yesu mii...)
Bila Yesu wewe ningekuwa wapi mimi?
(Umejawa na neema na rehema tele,.. X2) Baba

VERSE 02
Baba waguse na wajane majumbani,
Baba waguse na yatima mitaani,
Baba waguse na wagonjwa mahospitalini,
Wajue kwamba (wewe Baba upo.. X2)
Wajue kwamba wewe mwokozi wetu,
Wajue kwamba wewe Baba upo mtetezi wa karibu!

CHORUS
Bila Yesu Wewe ningekuwa wapi mimi....

VERSE 03
Uweza wako umejionyesha kwa viwete,
Uweza wako Baba wajidhihirisha na kwetu.
(Hakuna X2) jambo usilo liweza Baba.
(Hakuna X2) jambo usilo timiza.
Vile kama ulivyo wagusa wa kale nami niguse.
Naamini nami Bwana hutoniacha

PREACHES
"Ooh! Haleluya,
Ndugu yangu unayepata nafasi ya kuusikiliza wimbo huu sasa, nataka nikukumbushe jambo moja juu ya mwanamke aliyetokwa na damu kwa miaka kumi na miwili. Alipata nafasi ya kugusa vazi la Yesu ambalo ndio tiba aliyoiamini kwake na akapata kukaukwa damu zake.
Nakukumbusha tu na wewe ambaye unamwamini Mungu katika Roho na kweli usimwache aende zake maana yeye ndiye chakula cha uzima. Ooh Haleluya!"

AUTRO
Mmmmh! Mmmmh! Mmmmh!
Haa! Ha! Ha! Ha! Ha!
Haa! Ha! Ha! Ha! Ha!
Mmmmh!

Bila wewe X3

CHORUS
Bila Yesu Wewe ningekuwa wapi mimi.....

AUTRO
Haa! Ha! Ha! Ha! Ha!
20c0356a0b85ab0a6de2dc40c8264765.jpg
Haa! Haaaah!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom