Video inaongelea jinsi gani uchumi wetu unavyochukuliwa kutokana na mikataba mibovu na makampuni makubwa. Misaada tunayopewa ni theluthi ndogo sana ukilinganisha jinsi makampuni ya kigeni yanavyochota. Hapa wanaongelea uchimbaji wa shaba Zambia, lakini tunaweza pia kufananisha na hapa kwetu Tanzania kwenye uchimbaji wa madini mbalimbali pamoja na mikataba mingi mibovu. Fedha zinazopatikana ni nyingi mno lakini hazimsaidii kwa vyovyote vile mwananchi wa kawaida. Ndio maana umaskini wetu unaendelea kushamiri.