Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Ulinzi umeendelea kuimarishwa na Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuzunguka makutano yote yanayoingilia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam ambako kuna kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu.
Katika kesi hiyo inayosikilizwa leo, waandishi wa habari wamepigwa marufuku kusogea mahakamani hapo.
Katika eneo hilo la Mahakama, polisi waliovaa sare na wasio na sare wapo ndani ya magari wakifanya doria huku wakiwa wameshikilia silaha mbalimbali zikiwamo bunduki na virungu.
Mahakamani hapa leo Jumatatu, Aprili 28, 2025 kesi ya kuchapisha taarifa za uongo mitandaoni inayomkabili Lissu itaendelea kunguruma, mawakili wa pande zote wanatarajiwa kuchuana kwa hoja, kuhusu kuendeshwa kwa njia ya mtandao.
Ulinzi huo ni sawa na uliokuwa Alhamisi ya Aprili 24, 2025 wakati kesi hiyo pamoja na ile ya uhaini zinazomkabili Lissu zilipoitwa kwa hatua mbalimbali.
Polisi walitanda maeneo ya Mahakama kuzuia wasohusika kuingia.
Katika kesi hiyo inayosikilizwa leo, waandishi wa habari wamepigwa marufuku kusogea mahakamani hapo.
Katika eneo hilo la Mahakama, polisi waliovaa sare na wasio na sare wapo ndani ya magari wakifanya doria huku wakiwa wameshikilia silaha mbalimbali zikiwamo bunduki na virungu.
Mahakamani hapa leo Jumatatu, Aprili 28, 2025 kesi ya kuchapisha taarifa za uongo mitandaoni inayomkabili Lissu itaendelea kunguruma, mawakili wa pande zote wanatarajiwa kuchuana kwa hoja, kuhusu kuendeshwa kwa njia ya mtandao.
Ulinzi huo ni sawa na uliokuwa Alhamisi ya Aprili 24, 2025 wakati kesi hiyo pamoja na ile ya uhaini zinazomkabili Lissu zilipoitwa kwa hatua mbalimbali.
Polisi walitanda maeneo ya Mahakama kuzuia wasohusika kuingia.