Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 10,484
- 19,987
Salamu wana JF
Hii mada ya vazi la taifa ni miongoni mwa mada zinazoonesha namna gani hatupendi kukubaliana na ukweli wa mambo sisi kama watanzania.
Ukweli ni kwamba kama taifa lenye zaidi ya makabila 120 haiwezekani kuea na vazi moja la taifa tena tukabaki kuzingatia tamaduni zetu.
Ni vipi taifa lenye makabila zaidi ya 120 likawa na tamaduni moja?, desturi moja?, hii ni uongo. Tupo na mchanganyiko wa tamaduni nyingi sana za makabila yetu.
Mimi wazo langu ni bora tukawa na mavaxi rasmi kwa kila ukanda au makabila kisha baadae yapi yatakayobaki kuwa kama utambulisho wa watu wetu.
Hata huko Nigeria hawana vazi moja la taifa bali wana mavazi yanayowakilisha makabila yao.
Changamoto kuu ya hili swala ni liamshwa kwa hali na hulka za ukabila na hili hatuwezi kulikwepa kama tutataka kuwa na hicho tunachokiita vazi la taifa.
Kama taifa tukiona hii mada haina maslahi mapana ya utaifa ni bora tukaachana nayo.
Asanteni.
Hii mada ya vazi la taifa ni miongoni mwa mada zinazoonesha namna gani hatupendi kukubaliana na ukweli wa mambo sisi kama watanzania.
Ukweli ni kwamba kama taifa lenye zaidi ya makabila 120 haiwezekani kuea na vazi moja la taifa tena tukabaki kuzingatia tamaduni zetu.
Ni vipi taifa lenye makabila zaidi ya 120 likawa na tamaduni moja?, desturi moja?, hii ni uongo. Tupo na mchanganyiko wa tamaduni nyingi sana za makabila yetu.
Mimi wazo langu ni bora tukawa na mavaxi rasmi kwa kila ukanda au makabila kisha baadae yapi yatakayobaki kuwa kama utambulisho wa watu wetu.
Hata huko Nigeria hawana vazi moja la taifa bali wana mavazi yanayowakilisha makabila yao.
Changamoto kuu ya hili swala ni liamshwa kwa hali na hulka za ukabila na hili hatuwezi kulikwepa kama tutataka kuwa na hicho tunachokiita vazi la taifa.
Kama taifa tukiona hii mada haina maslahi mapana ya utaifa ni bora tukaachana nayo.
Asanteni.