Kazi kweli kweli!!
....Ili kuendelea ku-balance darasa hili informative, pengine ningependa kuuliza hoja ya nyongeza kwa mkuu Deception :
1. ARVs. Mara nyingi tu inashuhudiwa kwamba ARVs zinaokoa maisha ya wagonjwa wenye maradhi ya Ukimwi. Mimi mwenyewe nimeshuhudia kwa wagonjwa watatu. Kwamba, mtu anaugua mpka kufikia critical condition ya kutisha kiasi kwamba mnaona kabsa kuwa huyu anakufa muda wowote. LAKINI akishaanza dozi ya ARVs ananyanyuka anapona na kuwa healthy kabsa!!
NOTE: Huo ndo UHALISIA & UZOEFU huku 'site'.
SWALI: JE, kama kweli ARVs pia zinasababisha Ukimwi (kama unavyodai), ni kivipi tena dawa hizi zinawasaidia wagonjwa kiasi hicho??
DARASA HURU.
Mkuu ulichofanya sio kujibu, bali kuandika kile ulichokalilishwa na wenye mladi wao.
Yani ulichofanya ni kutokukubali kuitukanisha taaluma yako.
Ahsante mkuu!!
Vipi tena mkuu.....
Very very very good question.
Swali hili nilishawahi kuulizwa na wenye fikra pevu huko nyuma,na jambo hili ni mojawapo ya matukio yanayotokea kwenye 'site' ambayo ndio huwafanya watu wasiamini moja kwa moja kwamba HIV hasababishi AIDS,watu wanabaki kutokuwa na msimamo wowote kwa sababu ya mambo kama haya.
Jibu:
"Watu wengi wanaweza kuona tukio hilohilo lakini kila mmoja akatoka na jinsi alivyolielewa,hii inatokana na viwango tofauti vya elimu/uelewa walionao hawa watu kuhusu tukio hilo"
"All people can observe the same event but they will come out with different judgement/understanding,this is due to their level of pre existing knowledge about that particular event"
Sasa baada ya hapo twende kwenye suala lenyewe.
Siku zote huwaambia watu kwamba wanashindwa kuelewa matukio haya kutokana na kutofanya uchunguzi wa kina wa wagogonjwa hao.Watu wanatumia hisia zaidi kuliko uhalisia.Watu wengi huwa wanaona au wanasikia kwa mbali tu matukio haya,na hata kama yeye mwenyewe anauguza pia inategemea uelewa wake kuhusu sayansi hii.
POINT 1:
1.ARVs hazina uwezo wa kutibu TB.Kama huamini muulize daktari yeyote atakwambia.
2.ARVs hazina uwezo wa kutibu Cancer.
3.ARVs hazina uwezo wa kutibu malaria.
4.ARVs hazina uwezo wa kutibu Pneumonia.
5.ARs hazina uwezo wa kutibu kisukari.
6.ARVs hazina uwezo wa kutibu hepatitis.
.....
.....
ARVs hazina uwezo wa kutibu maonjwa yote tunayoyajua sasa.Msije kudanganywa kwamba ARVs zinaweza kutibu aina fulani za cancer.NO!!!
POINT 2:
Wagonjwa hawaugui ukimwi bali wagonjwa wanadhoofika na kuugua maradhi yanayoingia mwilini kutokana na kinga kupungua(yaani ukimwi).Magonjwa haya yanafahamika sana,mfano;Malaria,TB,PCP,Hepatitis,cancer nk.TB umekuwa ugonjwa kinara unaodhoofisha watu walio na upungufu wa kinga.
Sasa inabidi tuelewane kwamba,ukiona mtu anaugua au amedhoofika,ujue kuna ugonjwa fulani kati ya hayo niliyotaja hapo juu au mengine,lakini SIO UKIMWI.
POINT 3:
Hivyo basi,mgonjwa yeyote ambaye amepimwa na amegundulika(amesingiziwa) kuwa na HIV huwa hapewi ARVs peke yake.
Mfano:Kama mtu ameambiwa ana TB kwa mfano,halafu akapimwa HIV+.Mgonjwa huyu atadhoofika kutokana na TB lakini SIO HIV/UKIMWI.Wewe utamwona amekonda,anakohoa sana,ana homa za mara kwa mara,amepungua uzito,amekosa nguvu nk.Dalili zote hizi hazisababishwi na HIV,bali husababishwa na TB,ok???Tuko pamoja???OOOOK!!!Twende kazi...
Sasa sijawahi kuona au kusikia daktari yeyote amekuwa mpumbavu kiasi cha kumpa mgonjwa kama huyu ARVs peke yake bila ya kumpa vidonge vya TB.Au wewe umewahi kusikia/kuona mtu kapona TB kwa kupewa ARVs peke yake??Nijuze kama umewahi.
Sasa hakuna mtu yeyote asiyejua kwamba TB inapona kabisa kama mgonjwa atapata dozi inayostahili ya TB kwa wakati unaostahili.Sasa mgonjwa kama huyu atapona TB aliyonayo huku akitumia ma ARVs yake,ofcourse,kama amepona TB na anakula vizuri(ofcourse ndivyo wanavyoshauriwa) utamwona ananenepa,anapata nguvu,ananawiri,hakohoi tena,hana tena homa,LAKINI ANAENDELEA KUTUMIA ARVs.
Sasa kama mtu hajui undani wa mgonjwa mwenyewe na hana uelewa sahihi wa mambo haya,lazima atajua kwamba ARVs ndizo zimemponya/ziemnyanyua mgonjwa huyu.Umeona eenh???
Sasa huu ni mfano tu unaoonesha jinsi watu wanavyojichanganya kutoa judgement mbovu.Kuna mifano mingi.
Ndio maana wale wanaoniuliza mimi swali kama hili huwa nawaambia waniletee mfano mmoja tu ambao umeshiba data za kutosha halafu mimi nitawapa jibu sahihi,lakini hamna hata mtu mmoja aliyewahi kunipa mfano hai wenye data za kutosha zaidi ya kutumia hisia na kusikia kutoka kwa watu wengine.Haya mambo yana janja janja nyingi sana,kama watu hawako sawasawa kichwani wataendelea kuwa desciples/followers/wafuata nyanyo tu.
NOTE:
ARVs hazisababishi ukimwi kwa muda huohuo unapoanza kuzitumia.ARVs husababisha ukimwi baada ya muda mrefu wa kuzitumia.Na hii hutegema mambo mengi sana yakiwemo,asili ya mtu,ulaji wa mtu,style ya maisha ya mtu nk.Kama dozi ya ARVs itaanza pamoja na dozi ya TB,basi dozi ya TB itaisha baada ya takribani miezi 6(kwa dozi nyingi za TB).Sasa muda wa miezi 6 bado si rahisi kuona madhara ya ARVs kwenye kinga,muda huu bado mgonjwa atakuwa strong ukiachilia mbali viji madhara vidogovidogo tu.Hivyo kwa case hii,huwezi kuona mgonjwa amedhoofika kwa ARVs,bali utaona mgonjwa ame recover/amepona TB na labda ameanza kunenepa.Lakini baada ya long term use ya ARVs utaanza kuona dalili nzito nzito zinajitokeza ambazo nilishazitaja huko nyuma.
Je,Kuna swali lingine kwenye hilo jibu?
Mkuu Deception,
Nimeelewa vizuri sana, kwamba mgonjwa anapoanzishiwa dozi ya ARVs, hupewa na dawa zingine pia ambazo sasa ndo zinazotibu iyo specific disease inayomdhoofisha mgonjwa. Mfano mgonjwa wa TB mwenye HIV+, atapewa dawa za kutibu TB, na atapewa ARVs. Atapona TB na dozi itaishia hapo, lakini ARVs ataendelea kuzimeza siku zote za maisha yake yote!!! Nadhani hii ni point muhimu sana watu kuielewa. Ahsante sana mkuu Deception kwa clarification hii muhimu sana.
SWALI la mwisho kabsa:
Kwa kuzingatia ukweli kwamba almost DAWA ZOTE zina side effects, (I stand to be corrected).
JE, mtu akimeza dawa nyngne yoyote (apart from ARVs) on daily basis kwa muda mrefu atapata upungufu wa kinga yaani Ukimwi? Mfano dawa za Malaria, au dawa za TB, au dawa za Typhoid, zikimezwa daily kwa muda mrefu zitasababisha Ukimwi?
Kama jibu ni NDIYO, je inamaana kumbe ata dawa zingine pia zaweza sababisha Ukimwi, na sio ARVs tu?
SWALI la mwisho kabsa kwa mkuu mkuyati og :
JE, mgonjwa wa TB mwenye HIV+ , akipewa dozi ya TB pekee (bila ARVs) na akazingatia lishe & healthy life-style, atapona na afya kuimarika??
mzee wa kigonzile, Eiyer, pakamwam.
naomba nijibu part yangu.
ukitibu tb peke yake.bila ku-confront the primary cause of the immunosuppression (HIV) ni kazi bure. kuna kipindi katika stages of the disease (sanasana pale unapoanza kupata opportunistic infections) ambapo HIV viral load inakuwa kubwa sana na kushusha kinga sana mpaka unaanza kupata haya magonjwa nyemelezi. hata ule vizuri namna gani, hauwezi ku-reverse hii immunocompromisation inayotokea, maana you have no control over the virus causing it. inakuwa ngumu hata kupona TB maana katika vita dhidi ya TB mwili hutegemea dawa (anti-TB), lakini pia uwezo wa mwili ku-respond na ku-contain TB infection (immunity.) hivyo treating tb without adressing HIV is simply a futile cycle
lakini pia, sio kila mtu anayekutwa na HIV anaanzishiwa ARV. kuna criteria za ku-qualify kuanza ARV (with the exception of watoto below 15yrs). unaweza kusoma zaidi
naam, leo kupitia post yako hii nimeelewa kwanini mimi na wewe tunatofautiana.
kwanza, naomba uelewe kwamba :
1.ARVs hazikutengenezwa kutibu TB.Kama huamini muulize daktari yeyote atakwambia.
2.ARVs hazikutengenezwa kutibu Cancer.
3.ARVs hazikutengenezwa kutibu malaria.
4.ARVs hazikutengenezwa kutibu Pneumonia.
5.ARs hazikutengenezwa kutibu kisukari.
6.ARVs hazikutengenezwa kutibu hepatitis.
ARV zimetengenezwa ili kupunguza uwezo wa HIV ku-infect seli, zimetengenezwa kupunguza uwezo ea seli zenye maambukizi kuzalisha virusi zaidi, na zimetengenezwa kuongeza namba ya seli hai nyeupe zenye uwezo wa kulinda mwili na maradhi (kupandisha kinga ya mwili)
Mimi na Wewe tunakubaliana kwamba kinga ya mwili ya mtu inaposhuka, mtu anakuwa katika hatari ya kupata magonjwa nyemelezi mfano TB, mkanda wa jeshi, PCP, etc
Pia tunakubaliana kwamba kirusi cha HIV hakina uwezo wa kusababisha TB (tb husababishwa na M.tuberculosis), HIV hana uwezo kusababisha PCP (pcp husababishwa na p.jirovecii, wala HIV hana uwezo kusababisha mkanda wa jeshi.
Tunapotofautiana ni kwamba wewe unaamini kwamba HIV hawezi kushusha kinga ya mwili, HIV haambukizwi, and mostly HIV kirusi ha-exist.
mimi nimetoa facts hapa kuhusu existance ya kirusi HIV, na athari zake katika kuathiri mfumo wa kinga ya mwili.data nimetoa na referrence pia, for all to see.
Pia tunatofautiana maana halisi ya neno UKIMWI. wewe unali-define katika its most literal form and meaning (bila kumuhusisha HIV), mimi nali-define in its most intended meaning/medical meaning.
ukimwi kwangu ni HIV-AIDS, yaani mtu mwenye magonjwa nyemelezi kutokana na effect ya kirusi HIV kushusha kinga ya mwili, na si vinginevyo.
Kwa hiyo basi, mgonjwa anayepata virusi HIV na baada ya kirusi kuathiri na kushusha kinga yake ya mwili, anakuwa at risk ya kupata TB sio kwasababu HIV imesababisha TB bali sababu HIV imeshusha kinga ya mwili na kumpa mwanya mdudu wa TB kuingia na ku-attack mwili.
Kama utaelewa haya yote, sioni sababu ya wewe kushindwa kuelewa kwanini tunatoa ARV (kazi yake nimeelezea hapo juu). ARV hupandisha kinga iliyoshuka, na kupunguza idadi ya virusi. kwa kufanya hivyo, kinga ya mwili huimarika na ile risk ya kupata magonjwa nyemelezi na ya mara kwa mara hupungua ama kuisha kabisa. hivyo basi, wagonjwa hawa hawatapata TB, ama PCP ama mkanda wa jeshi etc maana kinga zao ni imara. lakini pia, mdudu wa TB hutibiwa kwa dawa za TB, sio ARV. ukimtibu TB akapona, na ukampa dawa kupandisha kinga ya mwili, ugonjwa huu nyemelezi hauwezi kumpata tena.
ndio maana wagonjwa wanaoanza ARV na kinga zao kuimarika huonyesha mabadiliko sana ya afya, maana yale magonjwa yaliyokuwa yanawapata mara kwa mara sababu ya kinga ndogo ya mwili yanakuwa hayana nafasi tena( improved kinga ya mwili will take care of them).
mwili hupata hata muda kujijenga na kutumia resources zake kujijenga, na sio kuchoma resouces kila unapoumwa mara kwa mara. ndio maana watu hawa hunenepa na kunawiri
unaposema baadaye ARV inakuja kusababisha ukimwi unakuwa unajichanganya,, lakini sababu hasa ya wewe kujichanganya ni kwa kuwa huifahamu maana halisi ya ukimwi.
denialists kibao wamekufa kwa kuwa na mawazo kama yako, je wajua watu wangapi walikufa south africa wakati wa thabo mbeki na support yake kwa denialists? do you have the figures? na kwanini south africa leo hakuna denialism?
utaelewa tu taratibu
Mkuu Deception,.....
JE, mtu akimeza dawa nyngne yoyote (apart from ARVs) on daily basis kwa muda mrefu atapata upungufu wa kinga yaani Ukimwi? Mfano dawa za Malaria, au dawa za TB, au dawa za Typhoid, zikimezwa daily kwa muda mrefu zitasababisha Ukimwi?
Kama jibu ni NDIYO, je inamaana kumbe ata dawa zingine pia zaweza sababisha Ukimwi, na sio ARVs tu?....
naomba nijibu part yangu.
ukitibu tb peke yake.bila ku-confront the primary cause of the immunosuppression (HIV) ni kazi bure. kuna kipindi katika stages of the disease (sanasana pale unapoanza kupata opportunistic infections) ambapo HIV viral load inakuwa kubwa sana na kushusha kinga sana mpaka unaanza kupata haya magonjwa nyemelezi. hata ule vizuri namna gani, hauwezi ku-reverse hii immunocompromisation inayotokea, maana you have no control over the virus causing it. inakuwa ngumu hata kupona TB maana katika vita dhidi ya TB mwili hutegemea dawa (anti-TB), lakini pia uwezo wa mwili ku-respond na ku-contain TB infection (immunity.) hivyo treating tb without adressing HIV is simply a futile cycle
lakini pia, sio kila mtu anayekutwa na HIV anaanzishiwa ARV. kuna criteria za ku-qualify kuanza ARV (with the exception of watoto below 15yrs). unaweza kusoma zaidi
Siwezi kukujibu mpaka usome tena ulichoni quote na uelewe kile nilichokilenga.Wewe hujanielewa,ninaposema hujanielewa namaanisha kweli hujanielewa,umejibu kwa haraka sana bila kuelewa nilichomaanisha,pole sana mkuu.
Soma vizuri swali nililoulizwa halafu soma vizuri jinsi nilivyojibu,utaelewa tu.
Kwa mtu mwenye uwezo mzuri wa kufikiri akisoma jinsi nilivyojibu halafu akasoma jinsi wewe ulivyoni quote na kunijibu lazima atagundua kwamba wewe unakubaliana na ukweli fulani wa kile nilichoandika mimi.
Sina haja ya kuandika mengi kwa kuwa hujaelewa nilichoandika.Nitajibu mfano mmoja tu kukuonesha kwamba hujanielewa.
Mfano:
1.Wapi nimesema ARVs zimetengenezwa kutibu TB?
2.Wapi nimesema ARVs zimetengenezwa kutibu cancer?
3.Wapi nimesema ARVs zimetengenezwa kutibu Malaria?
4.Wapi nimesema ARVs zimetengenezwa kutibu Pneumonia?
5.Wapi nimesema ARVs zimetengenezwa kutibu kisukari?
5.Wapi nimesema ARVs zimetengenezwa kutibu hepatitis?
Huu ni mfano mmoja tu kukuonesha kwamba hujanielewa.Halafu mfano huuhuu pia unaonesha jinsi ulivyokubaliana na hoja yangu kwamba wale watu waliozidiwa na kudhoofika kwa kuumwa magonjwa mbalimbali hawaponi eti kwa sababu wamepewa ARVs,umeelwa eenh?Bali watu hao wanapona kwasababu wamepewa madawa maalum kwa ajili ya kutibu magonjwa maalum.
Soma tena.
Dawa zote(namaanisha synthetic medicine/kemikali) za hospitalini hasa zile zilizolengwa kuathiri vijidudu au zinazotibu magonjwa ya vijidudu/zinazoua vijidudu pamoja zinashusha kinga ya mwili kama zitatumika kwa muda mrefu.Sivyo hivyo bali aina nyingine ya dawa hizo zinakuua hata kabla kinga yako haijaanza kuathirika vibaya.
1.Mfano dawa za Malaria:Hizi mkuu nadhani unajua mziki wake hata ukimeza kwa siku 3 tu.Sasa chukulia unatumia kwa mwezi 1 tu,wewe unadhani utabaki hai,pengine hata wiki unaweza usifike.Ndio maana dawa hizi hutumika siku chache tu ukilinganisha na ARVs.Dawa za typhoid pia vivyo hivyo.
2.Dawa za TB:Hizi angalau unaweza kuzitumia kwa muda mrefu zaidi ya zile za malaria au typhoid.Lakini principally zote zina potential ya kushusha kinga ya mwili.
Hivyo dawa nyingi zaidi ya ARVs huwa zinatumika kwa muda mfupi tu,hivyo hatuwezi kuweka concern yetu sana huko.Pia zipo dawa nyingine hutumika maisha yote,mfano zile za kisukari,hizi pia hushusha kinga as a matter of principle.
unadhani kupona magonjwa kunahusiana na kunywa dawa specific kwa huo ugonjwa peke yake tu? hakuna role ya kinga ya mwili? inamaana gani kutibu mgonjwa mwenye TB sababu ya kinga ndogo ya mwili bila ku-confront sababu iliyopelekea kinga hiyo kushuka? kwa hyo, mgonjwa mwenye kinga ndogo ya mwili iliyopelekea yeye kupata TB, ukitibu hyo TB peke yake bila ku-improve kinga ya mwili ambayo ndio sababu iliyosababisha yeye kupata TB in the first place, inahisi utakuwa ume-solve tatizo kweli? kama unakubaliana na mimi kwamba kinga ndogo ya mwili ndio iliyoleta TB, huoni kwamba mtu huyu atapata hyo TB tena na tena mpaka wafe unless you do something ku-improve hyo kinga ya mwili?
acha kujitoa ufahamu kaka, you can make much more sense than this!
kuhusu wewe kutosema ARV kutibu hayo hapo juu, then why did you have them written in the first place? lengo ni nini? tatizo hufahamu immunity hasa ni nini, inafanyaje kazi, na umuhimu wa immunity imara.
jipange urudi tena, tumebaki mimi na wewe tu hapa. I will only leave when you are gone. kudos!!
unadhani kupona magonjwa kunahusiana na kunywa dawa specific kwa huo ugonjwa peke yake tu? hakuna role ya kinga ya mwili? inamaana gani kutibu mgonjwa mwenye TB sababu ya kinga ndogo ya mwili bila ku-confront sababu iliyopelekea kinga hiyo kushuka? kwa hyo, mgonjwa mwenye kinga ndogo ya mwili iliyopelekea yeye kupata TB, ukitibu hyo TB peke yake bila ku-improve kinga ya mwili ambayo ndio sababu iliyosababisha yeye kupata TB in the first place, inahisi utakuwa ume-solve tatizo kweli? kama unakubaliana na mimi kwamba kinga ndogo ya mwili ndio iliyoleta TB, huoni kwamba mtu huyu atapata hyo TB tena na tena mpaka wafe unless you do something ku-improve hyo kinga ya mwili?
acha kujitoa ufahamu kaka, you can make much more sense than this!
kuhusu wewe kutosema ARV kutibu hayo hapo juu, then why did you have them written in the first place? lengo ni nini? tatizo hufahamu immunity hasa ni nini, inafanyaje kazi, na umuhimu wa immunity imara.
jipange urudi tena, tumebaki mimi na wewe tu hapa. I will only leave when you are gone. kudos!!
Wewe utakuwa na uchovu wa kazini,ninakushauri upumzike kwanza halafu kesho usome tena ile post yangu labda unaweza kuielewa.
Halafu mpaka sasa siamini kwamba wewe hujui kwamba nutrition na mambo mengine kama hayo hupandisha kinga ya mwili bila kujali kama una HIV stage fulani au la.Hivi umefanya uchunguzi wako kwa vitendo kweli wewe?Au unataka kurubuni akili za watu wasiojua?
Yaani umejikita kwenye ma ARVs eti yanapandisha kinga kwa kupandisha CD4.Yaani wewe na udaktari wako kweli hujui kama kinga ya mwili ni zaidi ya CD4?Hivi kweli hujui kama CD4 zinaweza kushuka hata kama huumwi chohote na huna huyo HIV?
Wewe unatafuta ushindani na si ukweli.Ndio maana nilikwambia tuachane na haya,mimi nataka unijibu kile nilichokuandikia PM,huu ndio utakuwa ushuhuda wa kweli kwako kwa kuwa utaona kwa macho yako mwenyewe,vinginevyo hapa tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu.Kama kweli unataka kujua ukweli,basi nijibu kule PM,vinginevyo nitajua kwamba unataka ushindani.