Uzuri hasa ni nini ?

kitunguu saumu

New Member
Joined
Apr 23, 2020
Posts
4
Reaction score
8
Uziri ni kitu gani uzuri ? uzuri wapimwa vipi?
Uzuri upo dukani kama wanunua pipi?
Uzuri ule wa ndani , au umbo la halisi?
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri kalio kubwa linalozidi kiuno,
Kwenye nguo likakaba, likasheheni unono,
Akitembea si haba, wausikia mvumo,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri jicho jeupe, ukilona larembua,
Na tena wanja lipakwe, mizigo yote watua,
Ni kama lasema nipe, uende kulitungua,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Ama uzuri ni rangi, ile ya kimalikia?
Nyeusi na hudhurugi, ni zipi zakuvutia?
Lilo chaguo msingi, hata ndani kuingia,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri guu la bia, la kuvalia kimini,
Mwendo wa punda milia, unaotesa mjini,
Vile ulivyojazia, na hamasa ya chumbani,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri ama ni sura, wanaita mapokezi,
Kama mepimwa na rula, jinsi lilivyo amaiz,
Ikakukaa taswira hata kukaa huwezi,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri ama ni nywele zilojaa mabegani,
Zinawaka mwele mwele, kama wale walatini,
Sio mawigi ya mbali, yakutoa kabatini,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri kitu machine, isio mwaga mafuta,
Yani vyuma vinatane, bila boliti kuvuka,
Wastani iwe nene, harufu njema wapata,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri tabia njema, kwa wa nje na wandani?
Anapotaka kusema, anawaza kwa makini,
Anafanya yalomema, na kuyaweka manani,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri kushika dini, zile sheria za MUNGU,
Kwa kukesha ibadani, na sadaka za mafungu,
Kutubu madhabahuni, kwa machozi ya uchungu,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri ni hela nyingi, za kufanya matanuzi,
Ya ziada na msingi, bila kuwaza michuzi
Safari zilo kwa wingi, baada ya zako kazi?
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

Uzuri akili nyingi, yakuiseti mipango,
Yale mambo ya mzingi, ujinga kuweka kando,
Ushauri wake mwingi, kuunyoosha mkondo,
Uzuri hasa ni nini? Na upo sehemu gani ?

hakuna alokamali, kuyapata hayo yote,
weka tamaa za mwili, na akili usiache,
kupata mlo kamili, ni lazima ubalanse,
haya ni yangu mawazo, uzuri kwako ni nini ?
 
Uzuri kwanza Akili ndo mengine yafuate
 
Hapa wenye sura za baba zetu tunasoma comments tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…