Uzinzi ni dhambi ya mauti...

Sasa kama anafanya uzinzi sii maana yake ana mafanikio.....utapataje mbususu bila hela kwa karne hii?

Hahahaaa uzinzi haunaga mafanikio. Tena unakuta ule uzinzi ni wa kukusudia ndio mbaya mno. Yaani inawezekana kabisa inakua ngumu kuacha lakini ni kuomba neema ya Mungu tuu mtu uweze kuacha kabla ya kukutana na adhabu yake

Adhabu ya zinaa popote kwenye maandiko ni kifo tuu... iwe biblia iwe Qur'an adhabu ni kifo
Sheria zimekua zikisimamia haki za binadamu lakini Mungu mkaliiiiiiii
unaweza usife kwa kupigwa mawe lakini ukafa ukiwa unafanya zinaa au ukafa baada ya zinaa kwa magonjwa
Mungu atusaidie
 
Na shetani nae ndio katulia hapo kwenye mbususu na de libolo. Anajua kabisa hapa anatupata.
Mie kwa kweli katika kitu nachojutia kuhusu uzinzi ni jinsi uzinzi ulivyonifanya niwaone wanawake kuwa sio binadamu wa kuwaheshimu. Yaani kweli shetani ana nguvu mnooo.

Binadamu mwenzio unaishia kumuona kama chombo cha starehe tuu...huna empathy yoyote kumuelekea mwanamke unachoona wewe ni kama likitu tuu ambalo unaweza limwagia shahawa na kusepa zako. Its realy bad. Unataka kuacha lakini demu akikula nauli yako tuu basi ndio unapata justification ya kuwachukulia kama chombo cha starehe.

Wanawake muwe na ubinadamu pia kwenye suala la nauli zetu tunazowatumia. Mnatufanya tuendelee kuwa wafuasi wa shetani.
 

Muda sio mrefu Mungu atakuondoa kwenye huo udhaifu
Usiache kuja hapa kushukuru
 
Dhambi zote sio sawa, Kila dhambi atendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake, isipokuwa dhambi ya uzinzi. Unaonaje ukimsikia mke wako amezini, na ametukana mtu. Ipi inakuuma moyoni.


YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI
 
1 Wakorintho 6 (Biblia Takatifu)
Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―
¹⁸ Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
¹⁹ Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
²⁰ maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
 
Mtoa mada Mwenyezi Mungu akubariki sana kwa kutukumbusha kuishi vyema kadiri ya maagizo ya Mungu.

Binadamu tuna asili ya kujisahau na ndo hapo shetani huchukua point kutuvuta dhambini, ndio maana Yesu ametusihi tusali kila wakati ili tusiingie dhambini.

Sala ni chakula bora kwa afya ya mwanadamu, pia hutuweka karibu na Mungu hivyo maombi yetu husikilzwa na kujibiwa mapema

Tukimbieni zinaa, mifano hai ipo mitaani hakuna mahusiano yenye uzinzi ndani yake ambayo yanafika mbali, matukio ni mengi kusalitiana, kuuwana yote hutokana na kumchukiza Mungu kwa dhambi ya uzinzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu howardlite tafadhali tunaomba msaada hapa..
HAPANA MKUU MUNGU HAKUWAHI KURUHUSU,SOMA MUNGU ALIMWAMBIA NINI NA ALIVYOKASIRIKA:
1 Wafalme 11:1-13
[1]Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti,
[2]na wa mataifa BWANA aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda.
[3]Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.
[4]Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa BWANA, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.
[5]Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni.
[6]Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA, wala hakumfuata BWANA kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.
[7]Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni.
[8]Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu.
[9]Basi BWANA akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha BWANA, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili,
[10]akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru BWANA.
[11]Kwa hiyo BWANA akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako.
[12]Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako.
[13]Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.
 
Reactions: Cyb
Hapa Yesu anaulizwa maswali na wasomi wa dini(Mafarisayo) kuhusu talaka na kuwa na mke zaidi ya mmoja na wanamwambia mbona Musa aliruhusu?
Anawajibu hamsomi?Tangu mwanzo Mungu aliumba mtu mume na mtu mkeπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ hamna mtu mume na watu wake you see,ni mmoja kwa mmoja,so anamaanisha kama Mungu aketaka mtu mume awe na wake wengi then akempa(angewaumba),jamaa wanasema mbona Musa aliruhusu?
Anawajibu kwasababu ya ugumu wa mioyo yao,lakini from the beginning is not,na anasema wanaofanya hivyo ke/me wanazini akiunganiaha na talaka.Just read πŸ‘‡

Mathayo 19:4-11
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
[6]Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
[7]Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
[8]Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
[9]Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
[10]Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
[11]Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
 
Shukrani kwa ufafanuzi pia katika ZABURI 33:1 imeandikwa "Mpigieni BWANA vigelegele, enyi wenye haki, Kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo" je mtu anaposifu na kuapoabudu akiwa anajijua ana dhambi na hajatubu hiyo ni kufuru au sio kufuru.
Ni sawa mkuu,lakini sio niliyoongelea nimejikita kwenye kumkufuru Roho Mtakatifu,by the way tunaposogea kwa ibada huwa tunajihoji,Yesu mahali fulani anasema hata Kama una neno na ndugu yako hamjasameheana na umeshika sadaka usiitoe mpaka umeenda kutengeneza kwanza uhusiano wenu kwa msamaha(toba).Moyo ni kibebeo cha ibada kama moyo hauko safi ni kelele,anasema niondoleeni kelele za vinywa vyenu.
Miaka ya 1980's kuna dini fulani ulikuwa ukijaribu kutaka kuingia Kanisani na huko vizuri moyoni ulikuwa unaanguka mlangoni,was very serious.
So before going to church ilikuwa lazima utubu kama kuna mahali ulikosea nguvu za Mungu was revealed isivyokawaida kiasi kama kipindi cha Anania na Safira in the book of Acts
 
.... Ni kweli, zamani things was very Serious... kuna Kanisa kule Tosamaganga - Iringa Padre alikemea tabia ya watu wanaosemekana kuwa ni washirikina wasiende kukomunika baadhi ya watu hao wakapuuza... siku hiyo akasema nimefunga Novena ya siku 9 ninaomba ambaye ni mshirikina na hajaungama asije kukomunika leo wale watu wakaleta ubishi wakaelekea kukomunika muda wa komunio...mtu wa kwanza alipofika kaanguka kabla ya kukomunika, wapili naye baada ya muda kafika kaanguka, watatu naye kafika kaanguka ghafla wakaona watu wengine wawili wakichomoka kwenye foleni ya kukomunika na kutimka mbio kuelekea nje.. Lilikuwa fundisho tokea siku hiyo na watu wale wakanyolewa nywele na wazee wa kimila wakaenda kuungama.!
 
πŸ˜€πŸ˜€ bro kumbe wewe wa zamani,hizi mambo bwana siku hizi zimekuwa adimu,watu wanawanga mpaka mimbarini.Sijui ndio siku za mwisho au moto umezimika?
Lakini Mungu hadhihakiwi siku ya kikiumana ni hatari.
 
Nakubaliana na bandiko lako mm mwenyew nimeonywa San Jua ya uzinzi na adhari zake kwangu mm
 
πŸ˜€πŸ˜€ bro kumbe wewe wa zamani,hizi mambo bwana siku hizi zimekuwa adimu,watu wanawanga mpaka mimbarini.Sijui ndio siku za mwisho au moto umezimika?
Lakini Mungu hadhihakiwi siku ya kikiumana ni hatari.
Imani zamani ilikuwa juu sana, kuna wimbi la Church Business limekuja-interfere mambo ya kiimani hapa katikati... ila Kanisa litasimama tena maana siku za Unyakuo zinakaribia kulingana na utungu wa mambo kama ilivyotabiriwa na manabii na kuandikwa na waandishi.
 
Amen ubarikiwe mtu wa Mungu, Ila dhambi ya kumkufuru roho mtakatifu kadiri ya ufafanuzi wa andiko kwa andiko na wanatheolojia mbali mbali ni kile kitendo cha kuikata sauti ya huyo roho inayokuhimiza kuacha matendo maovu kila leo hadi inafikia hatua unazoea kuishi ktk hiyo dhambi bila hatia moyoni na kuwa jambo la kawaida kwa muhusika then inatokea mauti yanakukuta bila ya toba pia hakuna dhambi isiyosameheka na toba ya kweli na dhati ni ombi linalojibiwa sekunde hiyo hiyo... Ila huyu anaemkufuru roho hasamehewi kwa mantiki ya kwamba haoni hatia ya dhambi ivyo moja kwa moja anakuwa haifanyii toba hadi mauti yanamkuta ila akipata neema ya kuitubia kabla ya mauti anasamehewa...

Binafsi napitia changamoto ya uzinzi si kwamba nazini ovyo, hpn, Ila naishi na mwanamke bila ya ndoa na ni huyo huyo pekee sizini nje na si kwamba namkufuru roho Ila ninamuomba Mungu aniwezeshe tufanye toba na kuiombea baraka ndoa hii isiyo rasmi ili tuirasimishe kwa kubatizwa upya na kuanza maisha ya ukristo upya ishara ya kuuvua utu wa kale na kuzaliwa upya Kwa kifupi hapa sifungi ndoa ila tunaombewa toba na kuombewa baraka maana tulipofika kuachana ni vigumu japo cheti cha ndoa tutapewa...

NB: Mimi ni msabato na kwetu ni tofauti ilivyo ktk baadhi ya madhehebu mengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…