Uzi wa Vijana wa CCM tu

Uzi wa Vijana wa CCM tu

lete rimoti

Senior Member
Joined
Aug 24, 2021
Posts
159
Reaction score
202
Habari zenu Macomrade. Bila Shaka Kila Mmoja anaendelea na Mapambano ya Maisha yake.

Uvccm Ina pande mbili

1. Wapo vijana wazalendo ila ni Waoga.
Hili ni kundi la vijana Wasomi lakini wamejawa na Uoga. Wanatambua Wajibu wao lakini hawataki Kutimiza kwasababu ya Uoga. Wananyimwa Fursa pia Kwasababu ya UAkili Zao kuonekana kubwa.


2. Machawa (kundi hili Lina vijana wasiojua kwanini wapo kwenye Chama, vijana machawa na wanafki, na vijana ambao wao husubiria Fursa tu zitokee na waendelee na Maisha Yao. Siasa haiwi sehemu ya Harakati Zao. Wana uwezo wa kusimama kuropoka na kutukana Watu Bila Kuangalia athari za Baadae.

Nimefungua Uzi Huu ili Vijana wazalendo wa kweli mpate Kuonyesha Kwenye Akili zenu Kuna Vitu Gani.


Nina Nia ya kugombea Uongozi niibadilishe jumuiya hii. Nataka iwe Ile ambayo Nyerere aliitaka, Jumuiya ya Vijana ambao watakuwa Tayari kuhoji Vitu vyenye Athari chanya katika Taifa. Jumuiya ambayo hata Rais wa nchi mwenyewe ataiogopa. Hatuwezi Kuwa Watu wakulalamika wakati Sisi wenyewe tunao uwezo wa kubadilisha Vitu.

Yaani Mwenyekiti Wetu analalamika na kuongea Kwa uchungu kuhusu Watu Wanaokula Pesa ya Serikali alafu, vijana tupo na tena tupo kimya tu. Hakuna hata mashinikizo tunayoyatoa huu unyonge hauhitajiki. Kuna Siku Hawa wananchi watachoka na Hali itakuwa Mbaya Zaidi.

Karibuni Vijana wazalendo, karibuni tuonyeshe kwamba Watu wema Bado wapo, lakini pia muwe Tayari hata kukosoa pale mnapoona Kuna mabaya yanatendeka katika Jumuiya au Chama Kwa Ujumla.

Na wahakikishia Huu, Uzi unasomwa na Wakuu wa idara nyingi katika chama. TUNAPOELEKEA ni lazima watahitaji vijana wenye Akili wakaongoze Taasisi za nchi. Sasa kama tutakaa kimya Bila Kuonyesha Nini tunacho katika Akili zetu basi Kila kukicha watawachukua vijana wa Vyama vingine wake watusaidie Kazi.

Lakini Pia Nakaribisha Maoni, Ushauri na ikiwezekana hata Matusi Kwa Watu ambao mmechoshwa na CCM nataka Kutumia Hoja Zenu Hapo Baadae nirekebishe mfumo Huu.

#TanzaniaKwanza[emoji120]
 
Kwa mara ya kwanza tangu nizaliwe,
Nimeamua Rasmi kujiunga na chama Cha mapinduzi (CCM)

Huwezi amini sijawai kuwa mwanachama wa chama chochote TZ
 
Naungana na ww ndugu yangu mabadiliko yanaanzia kwetu vijana, sisi ndio nguvu kazi ya taifa inapaswa tujitambue na tuwe wazalendo kwa maslahi ya taifa letu.
Kuna Siku Nitakapopata Nafasi ya kusimama Jukwaani. Nitahakikisha Nikirudi chini ni mfumo unabadilishwa au waniue Tu. Ila Hali ndani ya Chama sio nzuri. Sisi sio vijana ambao Nyerere alikuwa anahitaji
 
Haya tumefika..

Tuanze na hili, Kwa Afrika Tanzania imo miongoni mwa nchi zinazoendekeza mfumo wa kupendelea chama kimoja (Chama cha majizi) sasa je...

1-Tunaweza kweli kukitoa madarakani bila fujo.

2-Je tutaendelea kuvumilia huu wizi hadi lini?.

3-Je ni kweli anapopatikana raisi anayewapinga wanamuua.?

4-Je C.A.G anavyowaumbua (abarikiwe) hawawezi chukia wakatafuta namna ya kumnyamazisha milele.?.

5-Je kunakipindi deni la taifa lililipwa au tulijaribu kulipa likashindikana.?.

6-Je wameisha tuandalia pa kukimbilia baada ya hii nchi kuuzwa au kila mbuzi na urefu wa kamba yake (SSH).?.
 
Ccm ni ukoo wa panya
Hata uende ukiwa msafi kama theluji baada ya muda tu umeshafanana


Hii ni aibu kwa taifa
Wapigaji wapo ushahidi upo Ila bado wapo ofisini na wakipiga tena wataamushwa wakaendelee kupiga huko pia

Njia sahihi ya kumaliza haya yanayondelea ni katiba mpya yenye vipengele vya kuwafilisi na kiwafunga wapiga hela wote Siyo ccm wala vyama vingine
Kila siku nchi inaliwa na wachache ukigusa hapa utasikia huyo alikuwa mdhamini wa kampen
Mara mdhamini wa rasilimali watu kwenye ulinzi wa chama
Mara huyo ni mtoto wa Fulani

Hatutafika
Ondoa hii katiba ya kikolon
Weka katiba ya maslahi ya Tanzania na watanzania
 
Ccm ni ukoo wa panya
Hata uende ukiwa msafi kama theluji baada ya muda tu umeshafanana


Hii ni aibu kwa taifa
Wapigaji wapo ushahidi upo Ila bado wapo ofisini na wakipiga tena wataamushwa wakaendelee kupiga huko pia

Njia sahihi ya kumaliza haya yanayondelea ni katiba mpya yenye vipengele vya kuwafilisi na kiwafunga wapiga hela wote Siyo ccm wala vyama vingine
Kila siku nchi inaliwa na wachache ukigusa hapa utasikia huyo alikuwa mdhamini wa kampen
Mara mdhamini wa rasilimali watu kwenye ulinzi wa chama
Mara huyo ni mtoto wa Fulani

Hatutafika
Ondoa hii katiba ya kikolon
Weka katiba ya maslahi ya Tanzania na watanzania
Ukoo wa panya🤣
 
Nikiwa kama mwanaccm tunahitaji kuwa na katiba mpya ya chama

Mwenyekiti ana madaraka makubwa sana

Tukishamaliza ndio tuje kwenye katiba ya nchi
 
Haya tumefika..

Tuanze na hili, Kwa Afrika Tanzania imo miongoni mwa nchi zinazoendekeza mfumo wa kupendelea chama kimoja (Chama cha majizi) sasa je...

1-Tunaweza kweli kukitoa madarakani bila fujo.

2-Je tutaendelea kuvumilia huu wizi hadi lini?.

3-Je ni kweli anapopatikana raisi anayewapinga wanamuua.?

4-Je C.A.G anavyowaumbua (abarikiwe) hawawezi chukia wakatafuta namna ya kumnyamazisha milele.?.

5-Je kunakipindi deni la taifa lililipwa au tulijaribu kulipa likashindikana.?.

6-Je wameisha tuandalia pa kukimbilia baada ya hii nchi kuuzwa au kila mbuzi na urefu wa kamba yake (SSH).?.
Mkuu umeuliza Maswali Mazuri kweli. Ndani ya CCM Tupo Watu tunatamani Kuona nchi inasonga mbele lakini nikifikiria namna Ambavyo Watu wanaweza kukufanya nabaki na maumivu sana
 
Back
Top Bottom