atlas copco
JF-Expert Member
- Jun 15, 2015
- 8,292
- 9,390
Mwaka 2003 nilikutana na dada mmoja wa kinyakyusa alikuja Arusha na alikua anaenda monduli kwenye mahafali,huyo dada nilikutana nae stand ya kilombero na kwa maelezo yake wakati anatoka dar walikubaliana na wenzake wakutane stand ya ubungo wapande gari moja,ila alipofika stand rafiki zake walikua hawajafika hivyo alipanda basi la Amazon,baada ya kufika Arusha alibaki ndani ya basi akiwasubiri hao rafiki zake na alikua anawasiliana nao kupitia sim ya kondakta wa basi sababu yeye hakua na sim zaid ya no ya baadhi ya ndugu zake akiwemo huyo aliekua ana graduate huko Monduli, huyo kondakta wa hilo alikua mshikaji wangu,so baada ya binti kukaa pale zaid ya masaa mawili rafiki zake hawapatikani wala yule nduguye wa monduli yule mshikaji wangu kondakta aliamua kunipa majukumu ya kuhakikisha huyo binti anapata sehemu salama ya kulala ili kesho yake aelekee monduli,bahat nzuri na mimi kuna dada nilikua nafahamiana nae anafanya monduli kwenye ile supermarket ya jeshi so sikuwaza kwa kumpeleka zaid ya hapo kwa huyo sister,ikabid niondoke na yule dada kwa majina yake aliniambia anaitwa Mage ila sasa alikua na wasiwasi hatar,nilijaribu kumtoa hofu lkn bado alikua na wasiwasi,imagine tumetoka kilombero kwa miguu kuja kupanda daladala za sakina maeneo ya stand ndogo tulipofika chini mti maeneo idara ya maji aligoma kuendelea na safari,akaniambia kama vip tuchukue chumba maeneo haya tulale huko unapotaka twende siende je? Mkienda Kunibaka mtungo si heri mtu mmoja ambae ni mimi kuliko wengi,nikamwambia umewaza mbali sana ila sina mawazo hayo wewe ni kama dada yangu siwezi kukufanyia uhuni,nilitumia nguvu za ziada mpaka akakubali tuendelee na safari,tumefika stand tumepanda kidala safari ya kuelekea sakina imeanza kufika maeneo ya mianzini si akashuka kwenye gari amegoma tena kuendelea na safar na muda huo ni saa moja moja usiku kuelekea saa 2,mmh na mm ikanibidi nishuke nikawa mkali kwake kiaina nikamwambia hapa ulipoteremkia ni pabaya usije ukanilaumu ukidhurika,dah kwa ikabidi arudi kwenye gari kishingo upande,tumefika maeneo ya morovian tukashuka tukaelelea anapoishi yule dada.Tumefika nikamtambulisha vizur kwa yule dada bahat nzuri yule dada nae kumbe anafahamiana na yule mjeshi anaegraduate,dah binti alishusha pumzi moja ya furaha akapewa maji akaenda kuoga,baada ya hapo akapata msosi baada ya msosi akaniomba nimpeleke sehemu akapate huduma ya kupiga sim,kipindi hicho sim tunapigia kwenye vibanda wenye sim walikua watu wachache.
Aliniambia anaitwa Magreth au Mage kwa kifupi ubini wa baba yake nimesahau na alinipa no za kaka yake huyo baada ya pale nimekua nikimtafuta bila mafanikio,kabila lake ni mnyakyusa ila wazaliwa wa Dar es salaam.
Kuna uwezekano kaka yake au yeye ni member wa jf so wapatapo huu ujumbe au wale marafiki zake lazima watakumbuka tukio lilivyokua,pls wasisite kunicheki pm ni zaid ya miaka 20 sasa
Aliniambia anaitwa Magreth au Mage kwa kifupi ubini wa baba yake nimesahau na alinipa no za kaka yake huyo baada ya pale nimekua nikimtafuta bila mafanikio,kabila lake ni mnyakyusa ila wazaliwa wa Dar es salaam.
Kuna uwezekano kaka yake au yeye ni member wa jf so wapatapo huu ujumbe au wale marafiki zake lazima watakumbuka tukio lilivyokua,pls wasisite kunicheki pm ni zaid ya miaka 20 sasa