Uzalendo ni Upendo kwa Taifa (video)

kuna hoja ilitolewa jana na hukuijibu badala yake ulibaki kukenua.....una kadi ya ccm? wewe ni mwanachama?
thibitisha kweli ......

kingine wewe nape ni mmoja wa vijana wabovu kabisa taifa la tanzania lilewahi kuwa nao.....wewe ni mbovu sana


wewe ni mzalendo? hapo ulipo una uzalendo na uadilifu? upi nape......anyway aliyekutuma ana akili sana maana kupitia wewe anguko la chama chako litatimia....wengi wenu huko ccm mmeishiwa ubunifu na hivyo mmebaki kubaka sera za chama makin chadema....mzee kuisumo hakukosea wewe na huyo jamaa anayeongea huku akirusha mate (mukama) ni mzigo ndani ya ccm
 
weka hiyo meseji yako uliyokuwa umeiweka mwanzo mbona umeondoa na kubakiza hitimisho la thread yako?
 
kipande cha dakika moja tena hakionyeshi nini hasa unataka kusema ndo unatuweka hapa?
 
Duh!

Nimeangalia hii video sijaelewa kitu! Ufafanuzi wa maandishi ni muhimu!

'Tis ill sitting at Rome and striving with the Pope.
 
aaahhhh.....huyu jamaa nilikuwa namheshimu sana.......sasa naaamini kweli njaa ni kitu kibaya sana....
Ndugu yangu huyu alipiga sana kelele kipindi fulani(akiwa bado hajapoozwa na ukuu wa wilaya) kuhusiana na issue za ufisadi....na nikiri hapo ndo nilipomfahamia nape tena nikiwa na umri mdogo kabisa..(of abt 17 yrs hivi)....alipopata ukuu wa wilaya(nafikiri kama mkakati wa wakubwa kumziba domo) ndo alianza kutoa kauli za ajabu ajabu ikiwa ni pamoja na kuwaponda sana wapinzani hasa CHADEMA.....kwa kuwa nilikuwa mmoja kati ya wafuasi wa Nape kutokana na siasa zake za kukemea ufisadi(kumbukeni jengo la UVCCM na LOWASA)-Nilikuwa form three kipindi hicho kama sikosei.......

Alipopewa ukuu wa wilaya na kuanza kutoa moshi ili kutetea tumbo lake ndo nilipomuona hovyo kabisa na akaja ku conferm u-hovyo wake baada ya kupewa usemaji wa chama....

hapo sasa ndo rasmi nikiwa chuo kikuu mwaka wa kwanza...nilikamuona katibu wa chama na kuchukua kadi ya CHADEMA namba 0455084 na sijutii uamuzi wangu na sitoujutia kamwe.....!!!

Sasa wanajamvi...jaribuni kufikiria huyu 'mdudu' Nape ametupoteza vijana wangapi hadi sasa.....?

Nape,CCM&Co......go to hell 2015!!
 
Nape, kwa nia njema kabisa ningekuomba utambue ukungu unaoizunguka hii campaign ya uzalendo. Na sababu kubwa ya huo ukungu ni mazingira ya uzinduzi wake. Campaign imezinduliwa jirani na msiba wa mpigania uhuru wa Taifa hili ambaye kwa masikitiko makubwa alitelekezwa wakati wa uhai na hata kwenye safari ya mwisho.

CCM hawana tena moral authority ya kusimama mbele ya watanzania na kutamka neno 'uzalendo'. Dr Kyaruzi sasa hivi is more than jina la muasisi wa Taifa. Kifo chake na response ya CCM kimefunua hata ile robo chembe ya decency iliyokuwa aimebakia. Kwa vijana wengi wa Missenyi wakisikia neno uzalendo jambo la kwanza kukumbuka likakuwa msiba na upweke wa mazishi ya Mzee Kyaruzi. Kwa heshma ya Marehemu Mzee Kyaruzi ningekushauri uachane kabisa na hii campign na hasa matumizi ya hilo neno uzalendo na badala yake tafuta neno jingine.

Ni ushauri tu.
 
kipande cha dakika moja tena hakionyeshi nini hasa unataka kusema ndo unatuweka hapa?

Teh tehe naona anapima kina cha maji kabla ya kuchupa!. Akiona maji marefu humuoni tena.

Actually mimi ninafuatlia kwa makini sana actions za Nape na matarajio yangu ni kuwa atakuja na solutions za kuondoa matatizo ya watanzania ambazo chama chake kama chama chenye kusimamia sera kitazitekeleza. Watanzania hawataki maneno matupu toka CCM, Maneno wamwachie yule anayesubiri kupewa nafasi ya kufanya matendo.

Kama ni uzalendo watanzania ni wazalendo hasa, tatizo ni wale wenye mavazi ya kijani, wao wanatoka vitambi watanzania wabakie kuwa wazalendo. Yaani haiingii akilini kabisa, kama uzalendo tuwe wote. Uzalendo maana yake si kuipenda CCM bali nchi, na watanzania wa leo wanaipenda sana nchi yao ndiyo maana wanapiga kelele kwenye ufisadi na wizi wa mali ya umma unaofanywa under CCM in power.

CCM ilijitia kitanzi baada ya kuwalinda makada wake waliochota pesa BOT na wale walioliingiza taifa kwenye mikataba kama ya Richmond et al. Uzalendo pekee ni kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria na kuwafunga, si tu kuwafikisha.
 
Hii kauli haiwezi kuwa ya CCM itakuwa ya chama kingine kabisa siyo CCM ni CCJ,huyu jamaa hajawahi kuwa mwana CCM.ila tunakushukuru sana kwa kurahisisha kifo cha CCM
 
[video=youtube_share;ZgpWL9nh-uM]http://youtu.be/ZgpWL9nh-uM[/video]

Mi nataka nimwambie nape jambo moja uteuzi wa ngubiagai kuwa katibu wa vyuo vikuu ccm umewaudhi vijana wote wa vyuo kwa sababu ngubiagai hajui mchakato ulanzia wapi wala objective za hiyo project hazijui so hataweza kupata suport yoyote ile.kingine watafute waasisi kama kaena,lusekelo,venture,na wengine wanaojua A-Z hiyo project lasivyo ccm vyuoni inakufa.nakwamia ukweli kwasababu watu wa karibu yako wanakuficha ukweli and wanafiki wanakusifia ili wapate chochote
 
Uzalendo......uzalendo .....uzalendo gani huo????
Wa maneno au vitendo tupu???

Muanzisha uzi kama atarudi hapa itakuwa saafi ili tuchane package ya uzalendo tuone kilichomo
 
Back
Top Bottom