Uwongo Unanitokea Puani

Uwongo Unanitokea Puani

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
63,064
Reaction score
126,658
Kwanza Naanza Kusema Rasmi Kuwa UWONGO Kwangu Mwisho Leo Na Nimekoma Na Hizi Simu Za Mkononi Hakika ZITATUKOMESHA Hadi TUJUTE Kwanini TUMEKUBALI Utandawazi Uje Tanzania.

Kulikoni?

Nimekuja Mara Moja Hapa Mkoani Dodoma Ktk Harakati Zangu Za Kutafuta Pesa Na Ktk Shughuli Zangu Nyingi Huwa Nakuwa Nashirikiana Sana Na Mwenzangu Ambaye Kwa Tamaa Zangu Na Kutaka Kupiga Dili Nililoliijia Huku Mwenyewe Sikumuaga Jana Wakati Natoka Dar Kuja Huku Na Hata Mara Ya Mwisho Jana Usiku Aliponipigia Simu Saa 5 Asubuhi Alijua Kuwa Mwanamume Nipo Jijini Kumbe Mwenzake Huo Muda Ndiyo Nilikuwa Naitafuta Morogoro Na Basi La KIMBINYIKO.

Kwa Kujua Kuwa Jamaa Yangu Huyu Muhimu Kweli Ktk Shughuli Zetu Sijamuaga Jana Na Mimi Nikaamua Kuuchuna Ili Tu Asijue Kama Nipo Nje Ya Dar. Sasa Uone Kwamba Dawa Ya Mwongo Ni Fupi Leo Saa 3 Kanipigia Simu Na Mimi Bila Kujua au Kushtuka Nikapokea Kwa Mikogo Na Bashasha Zote Na Kuanza Kuzungumza Nae. Jamaa Akaniuliza Nipo Wapi Sasa Nikamjibu Kuwa Nimekuja Mara Moja Tu Dodoma Ila Mchana Wa Leo Nageuza Kurudi Dar Nia Na Madhumuni Nimfiche Asijue Kuwa Nimekuja Kupiga DILI Huku Safari Hii Bila Kumshirikisha Yeye. Wakati Nikiendelea Kumjibu Na Yeye Akadakia Na Kusema Kwamba Hata Yeye Ametua Na Ndege Dodoma Muda Si Mrefu Hivyo Kama Vipi Nimwambie Nipo Wapi Ili Anifuate Na Gari Ili Mchana Huo Turudi Wote Dar.

Ili Kumzuga au Kuua So Kwa Aibu Baada Ya Kuona NIMEBUMBULIKA Nikajifanya Namwambia Kuwa Simsikii Vizuri Na Ghafla Nikamkatia Simu. Wakati Nikiwa Nimemkatia Simu NIKITAFAKARI Jamaa Akanitumia Meseji Kuwa Amekuja Na Yeye Mara Moja Kuonana Na Bosi Fulani Ila Jamaa Akaniambia Kuwa Kama Deal Ikiwa Done Basi Atanishirikisha 100%, Wakati Kumbe Na Mimi Ndiyo Nimekuja Kuonana Na Bosi Huyo Huyo Ili Niingie Nae MKATABA Wa DILI Fulani La Hela Ndefu Bila Kumshirikisha Huyu Mwenzangu.

Jamani Nimechanganyikiwa Kwani Sasa Sijui Nifanyeje Kwani:


  • Nikikionana Nae Ataniona Mimi Siyo MWAMINIFU Kwake.
  • Nikiuchuna Inamaana Hilo DILI Atalipiga Mwenyewe.
  • Na Nikisema Nirudi Dar Kimya Kimya Nitakuwa Nimeingia Hasara.
  • Nisipoonana Na Huyo Bosi Inamaana Nakosa Hata Nauli Ya Kurudia Dar Ambayo Alinihaidi.

WADANGANYIFU Wenzangu Naombeni Msaada Wenu TAFADHALI Ila Najiandaa Nikirudi Tu Dar Niende Kwa Baba Paroko NIKATUBU Dhambi Hizi Za UWONGO Wa Kutumia SIMU Na Vile Vile Amlaani ALIYETENGENEZA Simu Hizi Kwani ZINATUSABABISHIA Mno Matatizo Na DHAMBI Za MAKUSUDI Ambazo Kwa Hali Ngumu Ya Maisha Ya Sasa Ni Ngumu KUEPUKIKA.

Nawasilisha Na Jamaa Bado Tu Anaendelea Kunipigia Simu ILA Naogopa KUPOKEA Kwani SIJUI Nitamjibu Nini. Msaada Tafadhalini Jamani!
 
Mh! kaaazi kweli kweli! Muibukie tu uue so na umshirikishe tu sasa maana hamna namna tena.

hilo ndo jibu na ushauri mzuri. Kula majivuno yako uyameze, uende kumwona na umpe yeye nafasi ya mbele kwenda kwa mwenye kofia.
Ukifika dar usijali kwenda kwa baba Paroko bali nenda moja kwa moja kwako ujiapize hutaki tena uongo kwani hauna faida
 
Cha muhimu hapo wewe nipm mimi hiyo deal nimfuate huyo boss kwa maana nipo Dodoma

halafu hiyo deal mkose wote wewe na jamaa

ila mimi nitakusaidia nauli ya kurudi dar kwa masharti kadhaa
 
ha ha ha jitose

Naona Aibu Sana Dada Yangu Mpendwa Miss Chagga. Leo Ujanja Wangu Wote Umeniishia! Naahidi Kwa Mungu Kuwa SITAONGOPA Tena. Hivi Huyu ALIYETUTENGENEZEA Hizi Simu Alikuwa Na Nia Nzuri Na Sisi Kweli? Hata Simu Nayo Nawaza KUITUPA au KUTOITUMIA Tena Kwani IMENICHUMIA Dhambi Leo.
 
Naona Aibu Sana Dada Yangu Mpendwa Miss Chagga. Leo Ujanja Wangu Wote Umeniishia! Naahidi Kwa Mungu Kuwa SITAONGOPA Tena. Hivi Huyu ALIYETUTENGENEZEA Hizi Simu Alikuwa Na Nia Nzuri Na Sisi Kweli? Hata Simu Nayo Nawaza KUITUPA au KUTOITUMIA Tena Kwani IMENICHUMIA Dhambi Leo.
simu haina kosa ila wewe mtumiaji ndiyo unaitumia kimakosa .. pole sana aiseee
 
Cha muhimu hapo wewe nipm mimi hiyo deal nimfuate huyo boss kwa maana nipo Dodoma

halafu hiyo deal mkose wote wewe na jamaa

ila mimi nitakusaidia nauli ya kurudi dar kwa masharti kadhaa

Ushauri Mzuri ILA Hapo Ktk Masharti Kadhaa Naona Unataka Tugawane Majengo Ya Serikali Wewe Mortuary Na Mimi Ukonga Prisons.
 
simu haina kosa ila wewe mtumiaji ndiyo unaitumia kimakosa .. pole sana aiseee

Nikifanya Mzaha Leo Na Mimi Nalala Ktk Gari Kama Dr. Slaa Kwani Hela Yangu Ya Lodge Imeshakata, Muda Unaenda Na Mpaka Sasa Lunch Nimepiga Free Kick ( Sijala ). Bora Tu Ningebaki Dar Nijilie Zangu Tu Mihogo Ya Kukaanga Kwa Mkopo Kuliko Huku Ugenini Dodoma Ambako Sina Hata Ndugu au Rafiki. Leo Si Ndiyo Mwanzo Wa Kupakatwa Na Wagogo?
 
lowasa akiingia matatizo yote yataisha hautakuwa na wasiwasi wa vidili vidogo km hivyo

Wewe Mimi Nawaza Nitaonana Vipi Na Huyu Bosi Na Nitarudije Dar Unaleta Habari Zako Za Lowassa. Swine!
 
Story nyingine bana.

Yaani unaenda kupiga dili ndefu wakati huna nauli ya kurudi. Paukwa pakawa.

cc BADILI TABIA
 
Last edited by a moderator:
Duu hapo ushalikoroga nenda tu mkaonane

Nikionana Nae Unadhani UAMINIFU Kati Yetu Utakuwepo Tena? Jamani Nimechanganyikiwa Halafu Kibaya Zaidi Nasikia Basi La Kurudi Dar Limebaki Moja Tu Na Nimeulizia Na Wanasema Siti Zimebaki 3 Tu.
 
Story nyingine bana.

Yaani unaenda kupiga dili ndefu wakati huna nauli ya kurudi. Paukwa pakawa.

cc BADILI TABIA

Sasa Nauli Ya Nini Wakati Najua Kuwa Naenda Kukutana Na TAITA Sema Tu Nilikosea Timing! Kwani Wewe Mkuu Ktk Maisha Yako Hujawahi Kukosea Hesabu Za Kimaisha? Mimi Nilijiamini Tu Na Sikujua Kama Huyu Jamaa Nae Atazuka Huku Idodomya.
 
Mkutane tu muyamalize.

Rekebisha Kidogo Kiswahili Chako Mkuu Hasa Sentensi Yako Hiyo Ya Mwisho Kuwa " Tukutane Na Tuyamalize " Humu Kuna Watu Wengi Sana Wa Pwani WANAWEZA Wakatafsiri Vibaya!
 
Lishatokea la kutokea kikubwa pokea cm yake mueleze ulipo kaeni ongeeni na kwa bosi nendeni pamoja ikibidi
 
Back
Top Bottom