Kuna kiongozi na Meneja
Unaweza ukawa meneja mzuri sana lakini ukawa kiongozi dhaifu, na unaweza ukawa kiongozi mzuri sana lakini ukawa meneja dhaifu.
Mwalimu Nyerere alikuwa ni kiongozi mzuri sana, lakini hakuwa meneja mzuri
Mkapa alikuwa half-half , Kiongozi wa uzuri wa wastani lakini pia meneja wa uzuri wa wastani
Kikwete alikuwa ni bonge la kiongozi, lakini hakuwa meneja mzuri
(ndiyo maana alianzisha na pia kuendeleza mambo ya msingi sana kama mabarabara, shule za kata, umeme kila kijiji, demokrasia pana, kuwezesha kina mama, kujenga na kutransform vyuo vikuu, kujenga mkongo wa taifa, kuanzisha taasisi kama TCRA, kuboresha afya kupitia mpango wa malaria, kujenga vituo vya moyo, kupatikana kwa ARV, kutoa pesa za kiutafiti kupitia incubator programs za COSTECH, mradi wa kuvuta maji kutoka Ruvu chini, mradi wa gesi, madaraja makubwa kwa madogo, Diplomasia ya hali ya juu etc). haya mambo ni mfumo wa kitaasisi ambao tutaendelea kunufaika nao miaka hata miaka
hata hivyo usimamizi wake wa mambo haukuwa mzuri, ndiyo maana kuna wafanyakazi hewa, twiga wanatoroshwa, Watu wanaiibia serikali, safari zisizo na maana wakati mwingine, n.k
Mimi naamini kama serikali ya sasa Itajifunza Leadership techniques za Jakaya Kikwete kisha Ikachukua Manegement Skills za Raisi wa sasa Tutapiga hatua kubwa