MTANGANYIKA M
Member
- Mar 19, 2014
- 8
- 19
Watanzaia wengi na hata nchi jirani mtakuwa mmewahi kusikia pambio za sifa kutoka kwa wanasiasa na uongozi wa awamu ya nne, hasa wa kutoka mrengo wangu wa kulia, juu ya uwekezaji wa kiwanda cha saruji cha tajiri namba moja wa Afrika, Mnigeria Aliko Dangote mkoani mtwara. Binafsi niliposikia baadhi ya wanasiasa na hasa mkuu wa kaya enzi hizo akiimba na kusifu ujenzi wa kiwanda hicho cha saruji, nilitaka kuingia kwenye mtego wa kuwaamini watu wa mrengo wangu wa kisiasa, hususani tulipoambiwa kwamba kiwanda hicho kikikamilika kitaweza kutoa ajira takribani elfu kumi 10,000 kwa watanzania. Nilishituka sana, lakini kwa akili ya haraka haraka nikajiongeza kufikiri kwamba aaah hiyo idadi si inajuisha wafagiaji wa magodown ya mawakala watakaokuwa pale wilayani kwetu kasulu? Nikajiongeza kuvuta kumbukumbu ya ahadi ya ajira millioni moja kwa vijana iliyotolewa mwaka 2005, na hatimaye majibu yaliyotolewa baadaye kwenye hotuba ya mwanasiasa namba moja mwaka 2010 wakati akiomba ridhaa tena ndipo nilipofunguka akili zaidi na kuona katika fikra, binamu yangu ambaye aliishia darasa la saba akibeba mfuko wa saruji kumpelekea mnunuzi nyumbani kwake nikajua tayari nayeye amejumuishwa kwenye idadi ya ajira elfu kumi. Hilo halikunisumbua sana, nilijua siasa inafanya kazi yake ingawa niliamini kwa sehemu kwamba uwekezaji huo utatunufaisha watanzania kwa kutoa ajira na hata kujenga uwezo wa kiteknolojia na uzoefu kwa wale watakaopata fursa ya kufanya kazi na uwekezaji huo.
Mwishoni mwa mwaka jana 2015 nilipata neema ya mwenyezi Mungu ya kusogea karibu na uwekezaji huo. Kabla sijaanza kuchunguza namna Watanzania hasa wananchi wa Mtwara wanavyonufaika na uwekezaji huu, nilipigwa na butwaa kwa mwenendo ambao sikuuelewa uliohusu ukaribu wa mkuu wa kaya na wanasiasa wake wateule na waandamizi kwa mradi huu. Mara kwa mara niliona magari ya serikali na wakuu mbalimbali wakipishana kwenye geti la mradi kana kwamba ndio mahali pao pa kazi ( ikulu Fulani hivi). Kwakweli naamini msisimko wa jamii uliotokana na kelele za kisiasa kuhusu mradi huu, ulichangia mabadiliko makubwa kiuchumi, ikiwa ni pamoja na kupanda kwa gharama za maisha hususani nyumba, mavazi na maeneo ya kufanyia biashara kusiko na ulazima matokeo yake maumivu yameegemea kwa maskini wa hali ya chini.
Kilichonisukuma kuandika Makala hii, si kutaka kukosoa uhusika wa mrengo wowote wa kisiasa katika mchakato wa uanzishwaji wa mradi huu, wala si usaliti kama ambavyo tumezoea kuambiwa huko nyuma sisi watu wenye mawazo huru ndani ya taasisi zetu za kisiasa, katika hili nalazimika kuamini katika usemi wa kila zama na kitabu chake, kwa sababu hata nikisema kwamba, kwa udhaifu wa uwekezaji huu ambao nitauzungumzia hapa chini waliohusika kutufikisha hapa hawachomoi, wao watakuja na majibu ya mzaha na matusi bila kujali hadhira, umri na nafasi zao kwamba ‘’aaaah sijachomeka popote bwana!’’.
Katika kichwa cha habari nimeomba uwekezaji huu uangaliwe kwa sababu ya mienendo inayondelea katika kiwanda hiki ambapo bila serikali kuingilia kati nchi yetu itaendeleaa kudharaulika na kuwa shamba la bibi miaka yote, na pia watanzania wataendelea kutawaliwa na wakoloni wa ki Assia wakati serikali ikichangia uangamizaji wa taifa kwa kutetea na kuaminisha watu kwamba huu uwekezaji una tija kwa taifa. Mathalani, nitazungumzia maeneo makuu manne yenye msukumo muhimu ambayo ni, nafasi za ajira, masrahi, unyanyasaji na usalama kazini kwa watanzania.
NAFASI ZA AJIRA.
Katika idara takribani kumi na mbili ambazo ni: Rasilimali watu, Manunuzi, stores, usafirishaji, Fedha, Mechanical, Electrical, Uchakataji, Instrumentation, uchimbaji(mines), ulinzi na karakana, ni idara mbili tu kati ya hizo ndio zinaongozwa na watanzania ambazo ni idara ya Ulinzi na Rasilimali watu, ambapo hata hivyo hii ya rasilimali watu inaongozwa na Mzee mmoja ambaye hana tofauti na raia wa Assia kwa uongo, Rushwa na ujanja ujanja. Pia katika idara zote hizo unaweza kukuta wasaidizi mpaka wa nafasi ya nne kushuka chini ni wahindi, maana yake ni kwamba kila idara inaongozwa na wahindi kwa mtiririko hadi wanapoisha ndipo Mtanzania anafuata. Kitu cha ajabu ni kwamba, hawa wahindi katika idara unaweza kumkuta mmoja tu mwenye taaluma husika, wengine ni ndugu zao tu ambao hawana vigezo, kuna watu pale wametoka India wamekuja kutunza kumbukumbu za motor reading na data entry ambazo hata mtu aliyepitia veta mtanzania anaweza kuzifanya kwa ufasaha kabisa, hawa wanajumuishwa na kuitwa wataalam (experts) pindi afisa wa kazi anapokwenda kukagua. Sitaki kuzungumzia sana vibali vyao maana nasikia pale TIC ukienda unatoa hela tu unapewa, nashukuru sasa kazi hiyo imerudi kwa mamlaka moja . Wapo watanzania wenzetu kama yule mzee anayejiita senior HR na mwenzake mwarabu, wanaotumika kuwapa mbinu na kuwaficha hawa wahamiaji haramu wa kihindi kwa malipo.
Katika kiwanda hiki huwezi kupata Mtanzania mwenye uzoefu au mhandisi mwenye uzoefu, na wao hawadhubutu kuajiri watanzania wa namna hiyo maana hizo ni nafasi za wahindi, hata wakitangaza nafasi hizo wanaweka vigezo ambavyo viko India tu (mfano mtu awe na uzoefu wa miaka kumi na tano kwenye kiwanda cha saruji) na hata ikitokea mtu amepatikana kutoka viwanda vingine vya saruji hapa Tanzania wanamwambia wampe mshahara ambao ni mdogo ambao hawezi kukubali ili kuonyesha kwamba watanzania hawataki kazi, mfano engineer ana uzoefu wa miaka kumi anaambiwa apewe laki tisa kwa mwezi,wakati alipotoka alikuwa anafanya kazi hizo hizo kwa ufasaha na analipwa vizuri. Hata hivyo, ajira zenyewe zimegubikwa na mazingira ya Rushwa na magumashi ya hali ya juu. mfano Zipo nafasi zimetangazwa wiki kama mbili zilizopita, ikiwemo nafasi ya stores manager, lakini kabla hata watu hawajaitwa kwenye usaili kuna mhindi kutoka India ameshaanza kazi wiki iliyopita kwenye nafasi hiyo.
Kiwanda kiliwachukua vijana wa kitanzania kutoka vyuoni (fresh graduates) wa uhandisi kwa ahadi ya kuwapeleka kwenye mafunzo kwa miezi sita katika nchi ya Nigeria, kwa kuwalipa posho kidogo, na baada ya hapo wakimaliza mwaka wataajiriwa kama wahandisi kiwandani vijana walihangaika kutafuta passports kwa kasi na kujiunga na kampuni ambapo baada ya kufika kiwandani zile posho zikageuka kuwa mishahara na safari ya mafunzo ikawa haipo tena zikaanza figisu figisu za kihindi nyingi, baada ya kelele nyingi wakaamua kuwachukua vijana hao wahandisi 20 kati ya 100 waliosemwa kwenye ripoti, kuwapeleka Nigeria kwenye kiwanda cha saruji kufanya kazi kwa miezi miwili na hiyo ndiyo ikawa imetoka, na hiyo habari ya mafunzo haipo tena hapo kiwandani na hata baada ya mafunzo hao ishirini waliohudhuria Nigeria hawashirikishwi hata kwenye mikutano ya kiufundi wao wanaagizwa kwenda kusimamia usafi na kurekodi data kwenye substatations.
Siku zote hapo kiwandani wahindi wanafanya kazi ya kuhakikisha watanzania hawajifunzi kitu ili mwisho waonyeshe kwamba watanzania hawawezi, nilishangaa sana kuona kwamba hata wachina walioko kiwandani kwa ajili ya kuendesha kiwanda kwa guarantee ya miaka miwili hawaruhusiwi kuwafundisha Watanzania, wanazuiliwa na wasimamizi wa mradi ambao ni wahindi.
Najiuliza, nini faida ya uwekezaji huu katika taifa, maana mwekezaji amepewa maeneo ya kuwekeza bure, mpaka eneo la kujenga bandari amepewa bure kwa kushirikiana na seriakli iliyokuwepo madarakani kurubuni wananchi kwa kuwaambia kwamba watafaidika na uwekezaji wa Dangote. Pia amepewa msamaha wa kodi kwa miaka mitano, ni nini fadhila yake kama haikuwa kuwaajiri na kuwajengea uwezo watanzania ? hatua gani zinachukuliwa na usalama wa taifa kuhusu hili? Naamini wapo pale, je wanapeleka taarifa hizi?
MASRAHI
Ni dhahiri kwamba mtanzania yeyote au hata mtu wa nje ya nchi akisikia mtu unafanya kazi kwa Dangote Tanzania, picha inayokuja kichwani kwa mtu huyo ni kwamba masrahi yako ni mazuri maana unafanya kazi na kampuni ambayo kwanza ni ya kimataifa na kwa sababu ya jina lenyewe basi ataamini kwamba uko vizuri tofauti na viwanda vingine vya ndani. Lakini mambo sivyo, yalivyo baada ya kufuatilia maisha na masrahi ya watu pale ninaamini kwamba huyu ndugu yetu mwafrika mwenzetu anapaswa kuitwa mafia, wafanyakazi wake wanalipwa ujira mdogo sana kiasi kwamba ni vigumu kuamini wakati mwingine kama wanafanya kazi kwa Dangote.
Lakini kubwa Zaidi ni tofauti kubwa iliyopo ya kimasrahi kati ya wahindi na watanzania, wahindi wote wamepewa usafiri, allowances nyingi na wanaishi hotelini muda wote kwa gharama ya kampuni, kila kitu na bima ya afya ya kiwango cha juu na mishahara yao hakuna mtanzania anayejua inalipwa kwenye akaunti zipi, lakini watanzania kila kitu wanafanya kwa shida, wanasafiri kwa kugombania daladala na kuning’inia kama maembe. Watu wanapewa bima ya afya AAR iliyoandikwa kwenye vikaratasi ya mwezi mmoja, hata hivyo wakienda hospitali hazikubaliwi. Mikataba inayotolewa ni mwaka mmoja mmoja kinyume na sheria ya Tanzania, Hakuna huduma yoyote ya motivation kwa mfanyakazi, hata maji ya kunywa unayapata kwa kuhonga rushwa ya salamu kwa mhindi, akijisikia anazuia watu kunywa maji. Watu wanakula kwenye vibanda vya mama ntilie mazingira amabyo si salama kabisa, ukipita Dangote barabani mchana unaweza kuona kundi kubwa la watu kwenye vibanda umiza kwa akina mama ntilie ukafikiri labda hao ni vibarua kumbe kuna maafisa rasilimali watu, fedha, manunuzi na wahandisi ndani ya vibanda hivyo wakati wahindi wana wapishi wao maalumu wanaowapikia nyumbani kwao na kuwaletea huduma kazini kwa gharama ya kampuni.
Wapo madereva kama mia tatu walifanyiwa usahili, kwa ajili ya kuendesha malori ya saruji, tena walikuwa wanaitwa baada ya kutoa rushwa, na baada usaili walipoambiwa mshahara hakuna hata mtu mmoja aliyebaki, wote waliondoka na kampuni ikaajiri wakala mwingine mhindi mtanzania anayeleta madereva vibarua pale kazi inapojitokeza.
Tujiulize, huu ndio uwekezaji tunaoruhusu uje kuuwa viwanda vingine vya saruji vinavyoa ajira zenye tija kwa watanzania?
UNYANYASAJI
Katika hili watanzania wanapata shida sana kwenye kiwanda hiki, watu wanaishi kama watumwa, si ajabu sana kuona Mtanzania mfanyakazi wa hali ya chini mfano wafanya usafi wakifukuzwa kazi kwa kosa la kucheka, mikataba yao wengi ni ya mwezi mmoja mmoja na hawalipwi kwa muda wakidai wanafukuzwa wanaletwa wengine, si watanzania wana shida?
Wapo vijana wanafukuzwa kazini bila sababu za msingi nilishangaa sana hivi majuzi niliposikia mtu(operator) amefukuzwa kazi na bosi wake mhindi anayeitwa Mr. Manoj kwa kupata pancha ya tairi eneo la mining, wakati huo ikiwa hakuna afisa usalama alieajiriwa ambaye ndio mwenye mamlaka ya kuthibitisha kosa hilo kuwa la maksudi au la, na mwingine ameitwa na huyo mhindi akamuangalia kwa kuwa anafuga ndevu akasema wewe unafanana na alshabaab sikutaki kazini na akamfukuza kazi, vilevile hata ukifukuzwa hupewi barua wakiishakupa taarifa kwa maneno tu ukiendelea kubaki kazini unapoteza muda maana mshahara hutauona. Hapo Kiwandani kila mhindi bila kujali nafasi yake ni bosi popote alipo kwa mtanzania hata kama mtanzania anamzidi elimu, wahindi hapo wana living certificates za sekondari,wengine mafundi Umeme wa grade ya chini kabisa hawajui chochote lakini wanaitwa wataalamu na wanaambiwa wasimamie wahandisi watanzania wenye shahada. Mhindi huyo Akisema yeye hakutaki HR anasema ndiyo bosi na anakufuta kwenye payroll haraka.
Yapo mambo mengi sana ambayo ukiyatazama hautofautishi na mahusiano kati ya mabwana na watumwa ambayo tuliyasoma katika vitabu vya historia zamani tukiwa mashuleni, wakati najiuliza haya nilipata kuzungumza na vijana waliokwenda Nigeria kufanya kazi kwenye kiwanda cha Dangote OBAJANA kilichopo Lagos. Kule wafanyakzi wahindi ni karibu asilimia themanini na wazawa ni kama ishirini tu ,Wahindi wanapewa upendeleo sana kwa sababu wakuu wa kampuni ni wahindi, ndhani hayo ndiyo mambo ambayo mkuu wetu wa kaya awamu ya nne alikuwa analenga yafanyike hapa kwetu hii ndiyo sababu mpaka sasa hawa wahindi hawaamini kwamba wako wachache sana hapa Dangote ya Tanzania hivyo wanataka kuonyesha watanzania hawawezi ili waletwe wengi.
USALAMA KAZINI
Mazingira ya kazi ni magumu sana kwa kuwa ndugu zetu hawa nadhani kwa sababu ya kubana matumizi hawataki kabisa kusikia kwamba kuwekeza katika usalama kazini ni jambo muhimu, vifaa vya kazi (PPEs) wanavyotumia wafanyakazi wa Dangote ukiwaangalia ni kofia tu na viatu ndivyo vinazofanana maana vifaa vingine unajinunulia mwenyewe ukiona vina umuhimu kwako, hata viatu tu ubora wake si wa kudumu miezi mitatu au mitano lakini unaambiwa ukae navyo mwaka mzima. Hakuna alama za tahadhari ya usalama kiwandani, magari yanaendeshwa kwa spidi inayofurahisha madereva na kila kitu kwenye usalama ni cha hovyo hovyo, wahindi wana dharau sana wakiambiwa kuhusu usalama wanawaambia watu waondoke waende wakafanye kazi maeneo salama kwenye viwanda vingine Tanzania, hii yote ni kujaribu kuonyesha kwamba watanzania hawako tayari kufanya kazi. Hakuna maafisa usalama wala mtaalamu wa mazingira hapo, kila kitu kinaendeshwa kienyeji kwa utaratibu wa India.
Nimeandika waraka huu nikiwa na masikitiko makubwa sana kama mtanzania wa kawaida, najua serikali yetu ya awamu ya tano imeanza kushughulikia matatizo haya kwa kasi nzuri, naiunga mkono seriklai na kuipongeza kwa hatua iliyofikia, kwa hapa tulipofikia na kwa jinsi tunavyoendelea nashawishika kuamini kwamba tunaelekea kupata heshima kama binadamu wenye taifa lao. Naiomba serikali iendelee kufanya operations za kuwarudisha hawa wahamiaji haramu makwao, najua ni wabishi sana na wengi wao wanaamini kwamba serikali ya Tanzania haijawahi kuwa na haitakuwa serious kiasi hicho ndiyo maana wengi wanaonekana kugoma goma na kuokuwa na mpango wakuondoka.
Ninamini, watanzania wana uwezo mkubwa wa kufanya mambo makubwa na kuleta maendeleo katika nchi yetu, iwapo taifa likiwekeza katika kuwaendeleza wasomi tulionao, hakuna taifa lililoendelea kwa kutegemea kuendelezwa na watu wa mataifa mengine kama viongozi wavivu wa kufikiri walivyoamini, Serikali iliyopita ililewa madaraka na kuamini katika uzembe, ukarimu wa kijinga pamoja na wizi wa ujanja ujanja, hakuna taifa linaloendelea kwa kujenga msingi wa maendeleo yake katika wizi na ujanja ujanja na matanuzi. Lazima tukubali kuanza kuumia ili kujenga taifa lenye heshima, leo hii ukienda kutafuta Mtanzania anayefanya kazi India humpati, kwanza nani atamruhusu, nenda Kenya, Rwanda na China kama utakuta mtanzania anakalia nafasi ya wazawa, lakini kwetu hapa limekuwa shamba la bibi na sisi tunalia hakuna ajira hata pale tunapopata ajira tunakuwa chini ya raia wa nchi nyingine na tunachekelea tu, Hatuwezi kuwa taifa lenye watu wenye akili timamu tukakubaliana na haya.
Mwishoni mwa mwaka jana 2015 nilipata neema ya mwenyezi Mungu ya kusogea karibu na uwekezaji huo. Kabla sijaanza kuchunguza namna Watanzania hasa wananchi wa Mtwara wanavyonufaika na uwekezaji huu, nilipigwa na butwaa kwa mwenendo ambao sikuuelewa uliohusu ukaribu wa mkuu wa kaya na wanasiasa wake wateule na waandamizi kwa mradi huu. Mara kwa mara niliona magari ya serikali na wakuu mbalimbali wakipishana kwenye geti la mradi kana kwamba ndio mahali pao pa kazi ( ikulu Fulani hivi). Kwakweli naamini msisimko wa jamii uliotokana na kelele za kisiasa kuhusu mradi huu, ulichangia mabadiliko makubwa kiuchumi, ikiwa ni pamoja na kupanda kwa gharama za maisha hususani nyumba, mavazi na maeneo ya kufanyia biashara kusiko na ulazima matokeo yake maumivu yameegemea kwa maskini wa hali ya chini.
Kilichonisukuma kuandika Makala hii, si kutaka kukosoa uhusika wa mrengo wowote wa kisiasa katika mchakato wa uanzishwaji wa mradi huu, wala si usaliti kama ambavyo tumezoea kuambiwa huko nyuma sisi watu wenye mawazo huru ndani ya taasisi zetu za kisiasa, katika hili nalazimika kuamini katika usemi wa kila zama na kitabu chake, kwa sababu hata nikisema kwamba, kwa udhaifu wa uwekezaji huu ambao nitauzungumzia hapa chini waliohusika kutufikisha hapa hawachomoi, wao watakuja na majibu ya mzaha na matusi bila kujali hadhira, umri na nafasi zao kwamba ‘’aaaah sijachomeka popote bwana!’’.
Katika kichwa cha habari nimeomba uwekezaji huu uangaliwe kwa sababu ya mienendo inayondelea katika kiwanda hiki ambapo bila serikali kuingilia kati nchi yetu itaendeleaa kudharaulika na kuwa shamba la bibi miaka yote, na pia watanzania wataendelea kutawaliwa na wakoloni wa ki Assia wakati serikali ikichangia uangamizaji wa taifa kwa kutetea na kuaminisha watu kwamba huu uwekezaji una tija kwa taifa. Mathalani, nitazungumzia maeneo makuu manne yenye msukumo muhimu ambayo ni, nafasi za ajira, masrahi, unyanyasaji na usalama kazini kwa watanzania.
NAFASI ZA AJIRA.
Katika idara takribani kumi na mbili ambazo ni: Rasilimali watu, Manunuzi, stores, usafirishaji, Fedha, Mechanical, Electrical, Uchakataji, Instrumentation, uchimbaji(mines), ulinzi na karakana, ni idara mbili tu kati ya hizo ndio zinaongozwa na watanzania ambazo ni idara ya Ulinzi na Rasilimali watu, ambapo hata hivyo hii ya rasilimali watu inaongozwa na Mzee mmoja ambaye hana tofauti na raia wa Assia kwa uongo, Rushwa na ujanja ujanja. Pia katika idara zote hizo unaweza kukuta wasaidizi mpaka wa nafasi ya nne kushuka chini ni wahindi, maana yake ni kwamba kila idara inaongozwa na wahindi kwa mtiririko hadi wanapoisha ndipo Mtanzania anafuata. Kitu cha ajabu ni kwamba, hawa wahindi katika idara unaweza kumkuta mmoja tu mwenye taaluma husika, wengine ni ndugu zao tu ambao hawana vigezo, kuna watu pale wametoka India wamekuja kutunza kumbukumbu za motor reading na data entry ambazo hata mtu aliyepitia veta mtanzania anaweza kuzifanya kwa ufasaha kabisa, hawa wanajumuishwa na kuitwa wataalam (experts) pindi afisa wa kazi anapokwenda kukagua. Sitaki kuzungumzia sana vibali vyao maana nasikia pale TIC ukienda unatoa hela tu unapewa, nashukuru sasa kazi hiyo imerudi kwa mamlaka moja . Wapo watanzania wenzetu kama yule mzee anayejiita senior HR na mwenzake mwarabu, wanaotumika kuwapa mbinu na kuwaficha hawa wahamiaji haramu wa kihindi kwa malipo.
Katika kiwanda hiki huwezi kupata Mtanzania mwenye uzoefu au mhandisi mwenye uzoefu, na wao hawadhubutu kuajiri watanzania wa namna hiyo maana hizo ni nafasi za wahindi, hata wakitangaza nafasi hizo wanaweka vigezo ambavyo viko India tu (mfano mtu awe na uzoefu wa miaka kumi na tano kwenye kiwanda cha saruji) na hata ikitokea mtu amepatikana kutoka viwanda vingine vya saruji hapa Tanzania wanamwambia wampe mshahara ambao ni mdogo ambao hawezi kukubali ili kuonyesha kwamba watanzania hawataki kazi, mfano engineer ana uzoefu wa miaka kumi anaambiwa apewe laki tisa kwa mwezi,wakati alipotoka alikuwa anafanya kazi hizo hizo kwa ufasaha na analipwa vizuri. Hata hivyo, ajira zenyewe zimegubikwa na mazingira ya Rushwa na magumashi ya hali ya juu. mfano Zipo nafasi zimetangazwa wiki kama mbili zilizopita, ikiwemo nafasi ya stores manager, lakini kabla hata watu hawajaitwa kwenye usaili kuna mhindi kutoka India ameshaanza kazi wiki iliyopita kwenye nafasi hiyo.
Kiwanda kiliwachukua vijana wa kitanzania kutoka vyuoni (fresh graduates) wa uhandisi kwa ahadi ya kuwapeleka kwenye mafunzo kwa miezi sita katika nchi ya Nigeria, kwa kuwalipa posho kidogo, na baada ya hapo wakimaliza mwaka wataajiriwa kama wahandisi kiwandani vijana walihangaika kutafuta passports kwa kasi na kujiunga na kampuni ambapo baada ya kufika kiwandani zile posho zikageuka kuwa mishahara na safari ya mafunzo ikawa haipo tena zikaanza figisu figisu za kihindi nyingi, baada ya kelele nyingi wakaamua kuwachukua vijana hao wahandisi 20 kati ya 100 waliosemwa kwenye ripoti, kuwapeleka Nigeria kwenye kiwanda cha saruji kufanya kazi kwa miezi miwili na hiyo ndiyo ikawa imetoka, na hiyo habari ya mafunzo haipo tena hapo kiwandani na hata baada ya mafunzo hao ishirini waliohudhuria Nigeria hawashirikishwi hata kwenye mikutano ya kiufundi wao wanaagizwa kwenda kusimamia usafi na kurekodi data kwenye substatations.
Siku zote hapo kiwandani wahindi wanafanya kazi ya kuhakikisha watanzania hawajifunzi kitu ili mwisho waonyeshe kwamba watanzania hawawezi, nilishangaa sana kuona kwamba hata wachina walioko kiwandani kwa ajili ya kuendesha kiwanda kwa guarantee ya miaka miwili hawaruhusiwi kuwafundisha Watanzania, wanazuiliwa na wasimamizi wa mradi ambao ni wahindi.
Najiuliza, nini faida ya uwekezaji huu katika taifa, maana mwekezaji amepewa maeneo ya kuwekeza bure, mpaka eneo la kujenga bandari amepewa bure kwa kushirikiana na seriakli iliyokuwepo madarakani kurubuni wananchi kwa kuwaambia kwamba watafaidika na uwekezaji wa Dangote. Pia amepewa msamaha wa kodi kwa miaka mitano, ni nini fadhila yake kama haikuwa kuwaajiri na kuwajengea uwezo watanzania ? hatua gani zinachukuliwa na usalama wa taifa kuhusu hili? Naamini wapo pale, je wanapeleka taarifa hizi?
MASRAHI
Ni dhahiri kwamba mtanzania yeyote au hata mtu wa nje ya nchi akisikia mtu unafanya kazi kwa Dangote Tanzania, picha inayokuja kichwani kwa mtu huyo ni kwamba masrahi yako ni mazuri maana unafanya kazi na kampuni ambayo kwanza ni ya kimataifa na kwa sababu ya jina lenyewe basi ataamini kwamba uko vizuri tofauti na viwanda vingine vya ndani. Lakini mambo sivyo, yalivyo baada ya kufuatilia maisha na masrahi ya watu pale ninaamini kwamba huyu ndugu yetu mwafrika mwenzetu anapaswa kuitwa mafia, wafanyakazi wake wanalipwa ujira mdogo sana kiasi kwamba ni vigumu kuamini wakati mwingine kama wanafanya kazi kwa Dangote.
Lakini kubwa Zaidi ni tofauti kubwa iliyopo ya kimasrahi kati ya wahindi na watanzania, wahindi wote wamepewa usafiri, allowances nyingi na wanaishi hotelini muda wote kwa gharama ya kampuni, kila kitu na bima ya afya ya kiwango cha juu na mishahara yao hakuna mtanzania anayejua inalipwa kwenye akaunti zipi, lakini watanzania kila kitu wanafanya kwa shida, wanasafiri kwa kugombania daladala na kuning’inia kama maembe. Watu wanapewa bima ya afya AAR iliyoandikwa kwenye vikaratasi ya mwezi mmoja, hata hivyo wakienda hospitali hazikubaliwi. Mikataba inayotolewa ni mwaka mmoja mmoja kinyume na sheria ya Tanzania, Hakuna huduma yoyote ya motivation kwa mfanyakazi, hata maji ya kunywa unayapata kwa kuhonga rushwa ya salamu kwa mhindi, akijisikia anazuia watu kunywa maji. Watu wanakula kwenye vibanda vya mama ntilie mazingira amabyo si salama kabisa, ukipita Dangote barabani mchana unaweza kuona kundi kubwa la watu kwenye vibanda umiza kwa akina mama ntilie ukafikiri labda hao ni vibarua kumbe kuna maafisa rasilimali watu, fedha, manunuzi na wahandisi ndani ya vibanda hivyo wakati wahindi wana wapishi wao maalumu wanaowapikia nyumbani kwao na kuwaletea huduma kazini kwa gharama ya kampuni.
Wapo madereva kama mia tatu walifanyiwa usahili, kwa ajili ya kuendesha malori ya saruji, tena walikuwa wanaitwa baada ya kutoa rushwa, na baada usaili walipoambiwa mshahara hakuna hata mtu mmoja aliyebaki, wote waliondoka na kampuni ikaajiri wakala mwingine mhindi mtanzania anayeleta madereva vibarua pale kazi inapojitokeza.
Tujiulize, huu ndio uwekezaji tunaoruhusu uje kuuwa viwanda vingine vya saruji vinavyoa ajira zenye tija kwa watanzania?
UNYANYASAJI
Katika hili watanzania wanapata shida sana kwenye kiwanda hiki, watu wanaishi kama watumwa, si ajabu sana kuona Mtanzania mfanyakazi wa hali ya chini mfano wafanya usafi wakifukuzwa kazi kwa kosa la kucheka, mikataba yao wengi ni ya mwezi mmoja mmoja na hawalipwi kwa muda wakidai wanafukuzwa wanaletwa wengine, si watanzania wana shida?
Wapo vijana wanafukuzwa kazini bila sababu za msingi nilishangaa sana hivi majuzi niliposikia mtu(operator) amefukuzwa kazi na bosi wake mhindi anayeitwa Mr. Manoj kwa kupata pancha ya tairi eneo la mining, wakati huo ikiwa hakuna afisa usalama alieajiriwa ambaye ndio mwenye mamlaka ya kuthibitisha kosa hilo kuwa la maksudi au la, na mwingine ameitwa na huyo mhindi akamuangalia kwa kuwa anafuga ndevu akasema wewe unafanana na alshabaab sikutaki kazini na akamfukuza kazi, vilevile hata ukifukuzwa hupewi barua wakiishakupa taarifa kwa maneno tu ukiendelea kubaki kazini unapoteza muda maana mshahara hutauona. Hapo Kiwandani kila mhindi bila kujali nafasi yake ni bosi popote alipo kwa mtanzania hata kama mtanzania anamzidi elimu, wahindi hapo wana living certificates za sekondari,wengine mafundi Umeme wa grade ya chini kabisa hawajui chochote lakini wanaitwa wataalamu na wanaambiwa wasimamie wahandisi watanzania wenye shahada. Mhindi huyo Akisema yeye hakutaki HR anasema ndiyo bosi na anakufuta kwenye payroll haraka.
Yapo mambo mengi sana ambayo ukiyatazama hautofautishi na mahusiano kati ya mabwana na watumwa ambayo tuliyasoma katika vitabu vya historia zamani tukiwa mashuleni, wakati najiuliza haya nilipata kuzungumza na vijana waliokwenda Nigeria kufanya kazi kwenye kiwanda cha Dangote OBAJANA kilichopo Lagos. Kule wafanyakzi wahindi ni karibu asilimia themanini na wazawa ni kama ishirini tu ,Wahindi wanapewa upendeleo sana kwa sababu wakuu wa kampuni ni wahindi, ndhani hayo ndiyo mambo ambayo mkuu wetu wa kaya awamu ya nne alikuwa analenga yafanyike hapa kwetu hii ndiyo sababu mpaka sasa hawa wahindi hawaamini kwamba wako wachache sana hapa Dangote ya Tanzania hivyo wanataka kuonyesha watanzania hawawezi ili waletwe wengi.
USALAMA KAZINI
Mazingira ya kazi ni magumu sana kwa kuwa ndugu zetu hawa nadhani kwa sababu ya kubana matumizi hawataki kabisa kusikia kwamba kuwekeza katika usalama kazini ni jambo muhimu, vifaa vya kazi (PPEs) wanavyotumia wafanyakazi wa Dangote ukiwaangalia ni kofia tu na viatu ndivyo vinazofanana maana vifaa vingine unajinunulia mwenyewe ukiona vina umuhimu kwako, hata viatu tu ubora wake si wa kudumu miezi mitatu au mitano lakini unaambiwa ukae navyo mwaka mzima. Hakuna alama za tahadhari ya usalama kiwandani, magari yanaendeshwa kwa spidi inayofurahisha madereva na kila kitu kwenye usalama ni cha hovyo hovyo, wahindi wana dharau sana wakiambiwa kuhusu usalama wanawaambia watu waondoke waende wakafanye kazi maeneo salama kwenye viwanda vingine Tanzania, hii yote ni kujaribu kuonyesha kwamba watanzania hawako tayari kufanya kazi. Hakuna maafisa usalama wala mtaalamu wa mazingira hapo, kila kitu kinaendeshwa kienyeji kwa utaratibu wa India.
Nimeandika waraka huu nikiwa na masikitiko makubwa sana kama mtanzania wa kawaida, najua serikali yetu ya awamu ya tano imeanza kushughulikia matatizo haya kwa kasi nzuri, naiunga mkono seriklai na kuipongeza kwa hatua iliyofikia, kwa hapa tulipofikia na kwa jinsi tunavyoendelea nashawishika kuamini kwamba tunaelekea kupata heshima kama binadamu wenye taifa lao. Naiomba serikali iendelee kufanya operations za kuwarudisha hawa wahamiaji haramu makwao, najua ni wabishi sana na wengi wao wanaamini kwamba serikali ya Tanzania haijawahi kuwa na haitakuwa serious kiasi hicho ndiyo maana wengi wanaonekana kugoma goma na kuokuwa na mpango wakuondoka.
Ninamini, watanzania wana uwezo mkubwa wa kufanya mambo makubwa na kuleta maendeleo katika nchi yetu, iwapo taifa likiwekeza katika kuwaendeleza wasomi tulionao, hakuna taifa lililoendelea kwa kutegemea kuendelezwa na watu wa mataifa mengine kama viongozi wavivu wa kufikiri walivyoamini, Serikali iliyopita ililewa madaraka na kuamini katika uzembe, ukarimu wa kijinga pamoja na wizi wa ujanja ujanja, hakuna taifa linaloendelea kwa kujenga msingi wa maendeleo yake katika wizi na ujanja ujanja na matanuzi. Lazima tukubali kuanza kuumia ili kujenga taifa lenye heshima, leo hii ukienda kutafuta Mtanzania anayefanya kazi India humpati, kwanza nani atamruhusu, nenda Kenya, Rwanda na China kama utakuta mtanzania anakalia nafasi ya wazawa, lakini kwetu hapa limekuwa shamba la bibi na sisi tunalia hakuna ajira hata pale tunapopata ajira tunakuwa chini ya raia wa nchi nyingine na tunachekelea tu, Hatuwezi kuwa taifa lenye watu wenye akili timamu tukakubaliana na haya.