Uwazi katika mahusiano

Uwazi katika mahusiano

FERTILIZER

Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
60
Reaction score
5
Ndugu wapendwa katika bwana,

Ila nina ombi moja kwenu naomba msaa wa kimawazo kwamba hivi nini kinacho sababisha mtu[ mwanamke] anaficha baadhi ya mambo yanayo husu ukweli wamaisha yake.

Kwamfano; mtu alimaliza kidato channe akafeli alafu akaanza tena upya kidato cha kwanza labda unamkuta yuko kidato cha tatu (private) alafu ukimuuliza anashindwa kusema ukweli.

Mungu awabariki sana
 
Kuna baadhi ya story ni bora kuwa untold
 
Hata hivo baadhi ya mambo ni binafsi sana na hayana uhusiano wowote na suala la mahusiano, sasahata kama alifeli akarudia tena wewe unataka akwambie ili mmlipie ada au???? angahika kama umefichwa jambo lenye athari katika mahusiano ila masuala mengine sio muhimu

lakin vilevile kwenye mahusiano kila mnapopata chansi mnasimuliana jambo fulani au wewe unataka mtu akusimulie kama yupo kizimbani???????????, kwa kweli habari yakutaka muambiwe yoteeeeeeeeeeeeee, basi inabidi tuwe tunaandika kitabu kabisa ili baada ya nyie kusoma kiingie sokoni tupate kipato, maana maisha ya mtu kwa miaka hata 7 unaweza andika page 500.
 
Akufiche ya ndani kwao ila sio kwenye ndoa yenu, Na mambo hayo yakujielez kuhusu kupanda na kushuk kielm kwan anatafta ajira?. Kaka c wanawake tu hata boy we mwambie mshahara unapata ngap? Ugomv utaozuka n kaz sana!.
 
Unaweza kuuliza mambo ya maisha yake ambayo yana maana tu kwa wakati huo na hata kwa baadae, kuna maswali mengine kuulizana ni kuchoshana tu, na ujue kuna watu hawapendi maswali yasiyo na tija.

Mf; Umenikuta nina kazi yangu nzuri tu, labda ukaniuliza nilihitimu chuo gani hiyo fani ninayofanyia kazi, hili swali siyo baya mi nakujibu tu shoti UDSM. Sasa kimbembe kinakuja unaongeza maswali, eti ukuwahi kurudia darasa? ulipitia qt? 4m 1 umesoma mara ngapi, Umerisiti 4m 4 mara ngapi? Nianze kukuelezea historia du! Akipenda kukwambia mwache aeleze mwenyewe asipopenda kausha
 
kuna mambo mengine ni vema yakabaki kuwa binafsi zaidi...kama hayupo tayari kushare usilazimishe!!!
 
kawaida sana hata mungu tunamdanganya sembuse wewe???
 
Ndugu wapendwa katika bwana,

Ila nina ombi moja kwenu naomba msaa wa kimawazo kwamba hivi nini kinacho sababisha mtu[ mwanamke] anaficha baadhi ya mambo yanayo husu ukweli wamaisha yake.

Kwamfano; mtu alimaliza kidato channe akafeli alafu akaanza tena upya kidato cha kwanza labda unamkuta yuko kidato cha tatu (private) alafu ukimuuliza anashindwa kusema ukweli.

Mungu awabariki sana

Maana yake na umri umepunguzwa kwa miaka mitatu. Mpe moyo, mwambie kwamba hayo sio issue kwako kama unampenda! Watu wanaona barmaid bila shida yoyote provided wamekubaliana na hali halisi.
 
Kuna mambo sio lazima wewe uyajue, hasa kama uhusiano wenu bado mchanga au hauna future yoyote. Lakini kadri mda unavyozidi kwenda na mnavyozidi kuwa karibu, yapo mambo ambayo wala hutauliza na utayafahamu tu.

Vitu muhimu kwangu ni kama umri, lazima nijue umri wake mapema..watu siku hizi ni wataalam wa kupunguza umri, waweza engage na mtu ukidhani ni mdogo kumbe kashakula na kumaliza ujana wake.
 
Jizoeshe kusema ukweli, jizoeshe kutenda na kutoa kulingana na uwezo, zuia hasira na fahari kwa malengo ya kujionyesha kwa watu una hali nzuri.
Ukiweza haya basi utaishi maisha yako kwa amani na hautoona shida kumwambia mtu stori yako ya maisha, sababu kwa kufanya hivyo unajenga mahusiano mazuri na jamii pamoja na rafiki au hata mpenzi wako. Ukiweza hivyo utaishi maisha ya amani na furaha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom