MSWATI III
Member
- Nov 16, 2010
- 90
- 63
Ijumaa kareem wadau! Kuna jamaa yangu alikutana na binti wa kisukuma kwenye bendi ya Akudo Impact. Wakapeana namba za simu tu usiku ule kwa sababu binti hakuleta ushirikiano wa kutosha pamoja na juhudi za huyu ndugu yangu kutoa offer. Baadae walianza kuwasiliana on & off na binti akawa anamzingua mshikaji sana, ahadi kibao za kuonana likin demu akawa anabadili mawazo last minute. Baada ya mwezi mmoja demu akaanza kujirudu na kutoa ushirikiano wa kutosha. Till this moment hawa watu ni wapenzi na muda mwingi huyu demu analala kwa mshikaji. Jamaa yangu kaja kwangu na kuomba nimshauri juu ya mambo kibao. Anadai kila kukicha anazidi kugundua kua huyu binti hajatulia kwa sababu zifuatazo: 1. Huyu binti bado anawasiliana na x boyfriend wake na hataki kuacha. 2 . Kapata mimba kasha kaitoa kisiri ila jamaa kashtukia baada ya kusoma sms kutoka kwa rafikie aliemsaidia kutoa hio mimba na vile vile demu alianza kulalamika maumivu ya tumbo na kutokwa na damu nyingi. Jamaa alivyombana akakiri kua ametoa mimba. 3. Huyu demu ana tabia ya kurudi nyumbnani kwake/ au kwa mshikaji usiku sana ( saa nne/ tano/sita/saba usiku) akidai kua kuna biashara anafanya na shoga zake. 4. Huyu binti anapenda kutoka out sana na shoga zake na hapendi jamaa awepo. 5. Jamaa yangu ana usafiri mzuri tu, ila kila siku wakiwa pamoja demu hataki kukaa sit ya mbele bali anadai anapenda sit za nyuma (nb: gari iko tinted). 6. simu zote za huyu demu zina passwords na anakua busy hadi mida ya usiku na marafiki zake wengi ni wanaume. 7. Huyu demu haoni aibu kumwambia mshikaji idadi na status za wanaume ambao ametembea nao kabla yake, yaan ni majanga tupu! etc etc etc. Mie binasfi nmemshauri jamaa yangu kua ameingia choo cha kike na ajipange kufa na pressure kama hatoachana na huyu binti. Mbaya zaidi huyu binti kapata mimba nyingine na anaitumia kama sababu ya msingi ya kutoachana coz binti anatishia kujiua na ameshawahi kumueleza jamaa kua anaijiwa na mawazo ya kujiua mara kwa mara, in that case jamaa anaogopa kumuacha binti kisa anaweza jiua. Naombeni ushauri wenu wadau. Jion njema