UVCCM yawasha moto Mbeya mjini

UVCCM yawasha moto Mbeya mjini

the horse

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
652
Reaction score
442
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Mbeya- Ndugu Amani Kajuna amezindua mashina ya wakereketwa na wanachama wa UVCCM Mbeya mjini.

Harakati hizo za Mwenyekiti huyo wa Vijana zinaashiria kutekelezwa kwa mkakati wa "fukuza Sugu, dumisha Amani Mbeya" ambao umeasisiwa na Vijana wa Mbeya chini ya uratibu wa Mwenyekiti huyo wa UVCCM.

Matawi hayo yatakayozinduliwa kila mtaa wa Mbeya mjini yatakuwa ni vituo maalum vya utekelezaji wa mkakati wa kulirudisha jimbo la Mbeya mjini kwa Chama Cha Mapinduzi.

Tangu kuanza kwa utekelezaji wa Mkakati huo, tayari mashina zaidi ya kumi na tano (15) yameshazinduliwa na kwamba vijana wameshajiweka vyema kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kunalirudisha jimbo hilo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Kwa jinsi hali ilivyo kwa sasa Mbeya mjini, inaonyesha kila dalili ya kuwa mwisho wa zama za Sugu na Nondo ndani ya Mbeya zimeisha.

CIWDJoeWsAAm9aq.jpg

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndugu Amani Kajuna akifungua tawi la Mpugusu la wakereketwa wa Umoja huo Mkoani Mbeya.

CIWDnm7WcAEPygN.jpg

Hivi ndivyo hali ilivyo katika mitaa ya Mbeya mjini, Vijana watanda mitaa yote wakihamasisha Amani na kuonyesha Ukakamavu wa Vijana wa CCM.

CIWEJT3WEAEkAPf.jpg

Wananchi wa Mbeya wakiwa wamejitokeza kwa wingi kumsikiliza Mwenyekiti wa Vijana wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Amani Kajuna. Hakika Mbeya imesimama na Amani.
 
Sugu kazi anayo mwaka huu, huku uchaguzi, kule Faiza Ally.
 
Vijana hatundanganyiki!!
 

Attachments

  • 1435311358215.jpg
    1435311358215.jpg
    7.9 KB · Views: 594
nasikia na wanawake wameapa kumpiga chini kwa kitendo alichomfanyia mke wake.
 
Hata akisimama rais mstaafu unayemjua wewe kwa tiketi ya ssm mby mjn hapiti

Takwimu za wanachama wa CCM Mbeya mjini yanaonyesha wazi kuwa wanaccm ni wengi kuliko kumdi lingine lolote katika wakazi wa Jiji la Mbeya. Hivyo ushindi wa CCM Mbeya mjini sio jambo la kushangaza, ni maamuzi tu ya kawaida ya wanacCM yataliridisha jimbo kwa CCM.
 
Sugu kazi anayo mwaka huu, huku uchaguzi, kule Faiza Ally.
Vyanzo vya karibu na mbunge huyo vinasema kuwa ameshapoteza matumaini na kwamba anajipanga kutogombea tena jimbo hilo ambapo kuna kila dalili kuwa atapoteza pesa yake na Vijana wameshaamua kumpinga.
 
Vijana wa Mbeya tumeshaamua na tumejipanga...waswahili wa sasa wana msemo wao maarufu, unasema "Ngariba haogopi Mkojo" na hivyo ndivyo tunavyosema Vijana wa Mbeya..
 
Vijana wa Mbeya tumeshaamua na tumejipanga...waswahili wa sasa wana msemo wao maarufu, unasema "Ngariba haogopi Mkojo" na hivyo ndivyo tunavyosema Vijana wa Mbeya..

msidhulumiane posho .
 

Attachments

  • attachment-10.jpeg
    attachment-10.jpeg
    9.5 KB · Views: 1,035
Wakati fulani tutumie na akili zetu.Katika jiji la Mbeya lenye mitaa 181 hakuna mtaa unaitwa MPUGUSO...hizo picha kapiga Ushirika kilomita 90 toka Mbeya mjini na mnasema hizo ni Mbeya Mjini?WANA CCM MKOJE?
Huyo mnayemwita Kajuna.alianzisha ligi KAJUNA CUP.kwenye viwanja vya S/M Mbata ameshindwa kuimaliza kwa kisingizio hana hela,alianzisha ya nini?NDUGU ZANGU MSISIKIE YA HAWA MAZEZETA..SUBIRINI TAR 25/10
 
Acheni ndoto za mchana jimbo haliwezi kwenda CCM! kafanyeni kazi zingine siasa imewashinda MBEYA!
 
Mbeya ipi??? Mbeya huwa hawadanganyiki hawashabikii ufisadi, hayo mashina anayafungua ili aweze kuwapiga vizuri
 
hizo kadi za chama au karata kadi gani zimekaa kama karata na kawaida iringa mjini mbeya mjini na arusha mjini upinzani hupewa msimu mmoja mpaka baada ya miaka 20
 
Back
Top Bottom