UMOJA wa Vijana wa CCM (UVCCM), umesema hautasita kumuengua mgombea yeyote atakayebainika kutumiwa na makundi yanayodaiwa kuwania urais ndani ya chama hicho mwaka 2015.
Katibu Mkuu wa Umoja huo, Martin Shigela alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya CCM mjini hapa na kubainisha kuwa iwapo kuna mtu aliyeingia kwa lengo hilo, ajiondoe mapema kabla hajabainika.
"Hatutasita kumuengua mgombea yeyote atakayebainika kutumiwa kugombea nafasi ya uongozi ndani ya UVCCM na makundi yanayodaiwa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015," alisema Shigela.
Hivi sasa kunaendelea usaili na kupitia fomu za wagombea wa nafasi mbalimbali za jumuiya hiyo, huku kukiwa na tetesi kuwa baadhi ya wagombea wanawania nafasi katika umoja huo kwa lengo la kutumiwa na baadhi ya vigogo wa CCM wanaotajwa kuwania nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Shigela alisema Kamati ya Utekelezaji inakutana mjini hapa kwa lengo la kuchuja wagombea na anaamini kazi hiyo itakwenda vizuri kama walivyotarajiwa kwani katika uchaguzi wa ndani wa CCM kuanzia ngazi ya Kata hadi Wilaya, ulifanikiwa kwa asilimia 90 na zitakamilika kwa kipindi kifupi kijacho.
Alisema watakuwa wakiweka alama kulingana na sifa, historia ya mgombea na uwezo wake wa uongozi ndani ya chama kwa lengo la kuhakikisha wanapata viongozi wazuri watakaokisaidia chama.
"Kazi kubwa inayofanyika hapa ni kupitia fomu za wagombea na pili kuwahoji kwa miaka mitano ijayo watakifanyia nini chama na majina yote tutayapeleka Halmashauri Kuu pamoja na alama zake" alisema.
Alisema vijana wengi wamejitokeza kugombea nafasi mbalimbali ngazi ya Mkoa na Taifa na kazi inayoendelea ni kuweka alama kwa ajili ya kuwapendekeza wagombea kwenye kikao kitakachokaa Septemba 12 na 13 mwaka huu na majina hayo yatapelekwa Baraza Kuu.
Alisema baada ya Baraza Kuu kupitia itatoa mapendekezo, Halmashauri Kuu ambayo itatoa majina kwenda kwenye Mkutano Mkuu wa UVCCM ambao utafanyika Oktoba.
CHANZO: GUMZO LA JIJI
Katibu Mkuu wa Umoja huo, Martin Shigela alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya CCM mjini hapa na kubainisha kuwa iwapo kuna mtu aliyeingia kwa lengo hilo, ajiondoe mapema kabla hajabainika.
"Hatutasita kumuengua mgombea yeyote atakayebainika kutumiwa kugombea nafasi ya uongozi ndani ya UVCCM na makundi yanayodaiwa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015," alisema Shigela.
Hivi sasa kunaendelea usaili na kupitia fomu za wagombea wa nafasi mbalimbali za jumuiya hiyo, huku kukiwa na tetesi kuwa baadhi ya wagombea wanawania nafasi katika umoja huo kwa lengo la kutumiwa na baadhi ya vigogo wa CCM wanaotajwa kuwania nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Shigela alisema Kamati ya Utekelezaji inakutana mjini hapa kwa lengo la kuchuja wagombea na anaamini kazi hiyo itakwenda vizuri kama walivyotarajiwa kwani katika uchaguzi wa ndani wa CCM kuanzia ngazi ya Kata hadi Wilaya, ulifanikiwa kwa asilimia 90 na zitakamilika kwa kipindi kifupi kijacho.
Alisema watakuwa wakiweka alama kulingana na sifa, historia ya mgombea na uwezo wake wa uongozi ndani ya chama kwa lengo la kuhakikisha wanapata viongozi wazuri watakaokisaidia chama.
"Kazi kubwa inayofanyika hapa ni kupitia fomu za wagombea na pili kuwahoji kwa miaka mitano ijayo watakifanyia nini chama na majina yote tutayapeleka Halmashauri Kuu pamoja na alama zake" alisema.
Alisema vijana wengi wamejitokeza kugombea nafasi mbalimbali ngazi ya Mkoa na Taifa na kazi inayoendelea ni kuweka alama kwa ajili ya kuwapendekeza wagombea kwenye kikao kitakachokaa Septemba 12 na 13 mwaka huu na majina hayo yatapelekwa Baraza Kuu.
Alisema baada ya Baraza Kuu kupitia itatoa mapendekezo, Halmashauri Kuu ambayo itatoa majina kwenda kwenye Mkutano Mkuu wa UVCCM ambao utafanyika Oktoba.
CHANZO: GUMZO LA JIJI