UVCCM: Maandamano ya kumuunga mkono Makonda ni lini?

VIVIANET

JF-Expert Member
Aug 30, 2015
2,129
2,918
Vijana wa UVCCM na BAVICHA wamekuwa na uelewa mdogo sana kiasi kwamba wamefikia hatua ya kuwaza nchi imegawanyika vipande viwili chama tawala na CHADEMA + UKAWA. Kila anayekosoa serikali ya chama cha mapinduzi UVCCM humwita mpinzani au UKAWA na kila anayeipongeza serikali na CCM BAVICHA + UKAWA humwita mawazo mgando ya chama kilicho chakaa CCM, wameshindwa kuelewa kuwa nchi hii ina watu milioni kadha wasiokuwa wanachama wa chama chochote cha siasa.

UVCCM walipoona watu wanakosoa approach mbaya ya Mh. Makonda kuhusu madawa ya kulevya walitangaza kuandaa maandamano ya kumuunga mkono wakimaanisha yupo sahihi na wanaomkosoa wote ni wapinzani wa serikali ya CCM, sasa nataka kujua tarehe rasmi ya hayo maandamano, je kumuunga mkono wanakubaliana na Makonda kuwa alikuwa sahihi na wote waliomkosoa hawakuwa sahihi? Je hata Waziri Mkuu hayuko sahihi?

Tuambieni tarehe ya maandamano UVCCM
 
Stering amekufa kwenye shamba la mchicha!!! Move imekwisha!! Walidhani ataendelea kuonekana shujaa!! Na jana waziri mkuu ndio amegongelea msumeno wa mwisho kwenye jeneza la stering!!!
 
Hawawezi kuandamana, walitaka kupima maji kwa kutumia mguu, mkuu alishasema heli kubaki na wana Kijani na manjano 200 nchi nzima kuluko kuwa na wanakijani milioni sita ambao wanaimba tuimani na EL
 
Hawawezi kuandamana, walitaka kupima maji kwa kutumia mguu, mkuu alishasema heli kubaki na wana Kijani na manjano 200 nchi nzima kuluko kuwa na wanakijani milioni sita ambao wanaimba tuimani na EL



Wamekuwa watu wa kukurupuka sana uvccm kama wakubwa zao
 
Back
Top Bottom