mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,410
- 4,988
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dodoma, Abdulhabib Mwanyemba, amesema kuwa vyama vya upinzani havina uwezo wa kushika dola kutokana na kutokuwa na misingi imara ya kiuchumi ya kuwahudumia wananchi. Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kuiamini CCM kwa kuwa ndicho chama chenye dira ya kweli ya maendeleo.
Akiwa katika hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi kwa baadhi ya wilaya za mkoa huo, Mwanyemba alisisitiza kuwa CCM haiwahangaishi wananchi kwa michango ya mara kwa mara, kwani inaamini kuwa raia wanapaswa kutumia muda wao katika shughuli za kujiletea maendeleo badala ya kuwa sehemu ya maombi ya misaada yasiyo na tija.
Vifaa hivyo vya ujenzi ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi aliyoweka pamoja na kamati ya utekelezaji ya mkoa, kufuatia ziara yao ya kutembelea wilaya zote za Dodoma. Lengo kuu ni kusaidia kukamilisha miradi ya ujenzi wa nyumba za UVCCM katika wilaya husika.
Katika awamu ya kwanza ya zoezi hilo, wilaya za Mpwapwa, Kongwa, Chamwino, na Bahi zimepokea vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi 500,000 kwa kila wilaya, fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani ya mkoa.
Mwanyemba pia ameahidi kuwa utaratibu huo utaendelea hadi wilaya zote zitakapofikiwa, huku akiahidi motisha kwa zile zitakazojitokeza kwa bidii zaidi katika kukamilisha ujenzi wa miradi hiyo.
----
Maoni ya wadau
Akiwa katika hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi kwa baadhi ya wilaya za mkoa huo, Mwanyemba alisisitiza kuwa CCM haiwahangaishi wananchi kwa michango ya mara kwa mara, kwani inaamini kuwa raia wanapaswa kutumia muda wao katika shughuli za kujiletea maendeleo badala ya kuwa sehemu ya maombi ya misaada yasiyo na tija.
Vifaa hivyo vya ujenzi ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi aliyoweka pamoja na kamati ya utekelezaji ya mkoa, kufuatia ziara yao ya kutembelea wilaya zote za Dodoma. Lengo kuu ni kusaidia kukamilisha miradi ya ujenzi wa nyumba za UVCCM katika wilaya husika.
Katika awamu ya kwanza ya zoezi hilo, wilaya za Mpwapwa, Kongwa, Chamwino, na Bahi zimepokea vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi 500,000 kwa kila wilaya, fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani ya mkoa.
Mwanyemba pia ameahidi kuwa utaratibu huo utaendelea hadi wilaya zote zitakapofikiwa, huku akiahidi motisha kwa zile zitakazojitokeza kwa bidii zaidi katika kukamilisha ujenzi wa miradi hiyo.
----
Maoni ya wadau
Jukumu la msingi la kuhudumia wananchi kupitia huduma za afya, elimu, miundombinu na ustawi wa jamii ni la serikali na si chama chochote cha siasa.
Serikali hupewa mamlaka na wananchi kupitia sanduku la kura, si kwa uwezo wa kifedha wa chama fulani.
Kupima uwezo wa kuongoza kwa kigezo cha uwezo wa kifedha wa chama ni kupotosha maana halisi ya uongozi wa kidemokrasia.
Mwamba kakengeuka sana.