UVCCM Arusha wafurahia kuondolewa RC Ntibenda

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,825
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Mkoa wa Arusha,umepokea kwa furaha kuondolewa kwa Mkuu wa Mkoa Ndugu Ntibenda na kuteuliwa kwa Mkuu wa Mkoa mpya Mh.Mrisho Gambo.Furaha hiyo imetokana na UVCCM Arusha kutoa tamko ambapo haujapita hata mwezi na Rais kaweza kuwasikia na kutekeleza ombi la kuondolewa kwa mkuu wa Mkoa.
image.jpeg


Mwenyekiti wa UVCCM Arusha,Lengai Ole Sabaya anasema kuondolewa kwa Mkuu huyo wa Mkoa ni furaha kwa jumuiya yao,kwani Rac huyo alikuwa ni mtu asiyetoa ushirikiano kwenye jumuiya hiyo kiasi cha wao kutuma maombi kwa Rais na kutaka amuondoe ndugu Ntibenda na kuweka mtu mwingine ambaye ataendana na kasi ya Mkoa huyo,ambapo Rais ametekeleza kwa kumteuwa Mh.Gambo ambaye vijana wa Arusha wanaamini watafanya nae kazi na atataendana na kasi ya siasa za mkoa wa Arusha.

Itakumbukwa hivi karibuni UVCCM Mkoa wa Arusha,wakishirikiana na DC wa wakati huo Mrisho Gambo na kwa msaada wa mfanyabiashara maarufu na kada wa CCM waliungana katika kumuomba Rais kuivunja halmashauri ya Jiji la Arusha inayoongozwa na CHADEMA kutokana na kile walichosema ni kushindwa kwa uongozi huo wa upinzani kuongoza Jiji hilo.

Ole Sabaya anasema kuondoka kwa Mh.Ntibenda kutaihuisha Jumuiya hiyo ktk jiji la Arusha ambayo kwa uongozi wa Ntibenda ilianza kuzorota kwa RC huyo kujiweka kando nao.Lakini kwa uteuzi wa kijana Gambo sasa Jumuiya inaenda kuwa imara na thabiti,pia wamemtuhumu Ntibenda kuzembea ktk swala la ulinzi na Usalama kiasi kwamba ndani ya muda mfupi,shule kadhaa katika mkoa wa Arusha zilichomwa moto.
 
Kuna watu kama hawa UVCCM hawana akili hata kidogo. Hivi tangu lini mkuu wa mkoa anayejitambua akawatumikia UVCCM? Huu ni utoto wa kiwango cha hali ya juu.
 
Sidhani mkuu wa mkoa kama ana jukumu la kuhakikisha kuwa jumuia ya UVCCM inakuwa imara. Huu ni ujinga uliotukuka.
 
Sawa, so kama shule zinaunguzwa ndo kusema Ntibenda kashiriki? If is administrative issues mbona kila siku ajari zinatokea na wakuu wa usalama barabarani ni wale wale?
 
Tujaalie Mh raisi iwe kasikia kilio chenu. "Jee mutampatia majimbo mangapi 2020?"

Mumeshindwa kufanya kazi zenu, sasa munaishi kwa majungu tu. Hivyo munamtegemea RC aje aimarishe CCM wakati nyie mulopewa kazi hiyo imekushindeni munabakia kueneza fitina tu sasa.
 
Mshahara wa dhambi ni mauti......!! Gambo na wenzake wasubiri mishahara yao!! Pia tuone kama Gambo atawajibika kwa UVCCM!!
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Mkoa wa Arusha,umepokea kwa furaha kuondolewa kwa Mkuu wa Mkoa Ndugu Ntibenda na kuteuliwa kwa Mkuu wa Mkoa mpya Mh.Mrisho Gambo.Furaha hiyo imetokana na UVCCM Arusha kutoa tamko ambapo haujapita hata mwezi na Rais kaweza kuwasikia na kutekeleza ombi la kuondolewa kwa mkuu wa Mkoa.View attachment 384966

Mwenyekiti wa UVCCM Arusha,Lengai Ole Sabaya anasema kuondolewa kwa Mkuu huyo wa Mkoa ni furaha kwa jumuiya yao,kwani Rac huyo alikuwa ni mtu asiyetoa ushirikiano kwenye jumuiya hiyo kiasi cha wao kutuma maombi kwa Rais na kutaka amuondoe ndugu Ntibenda na kuweka mtu mwingine ambaye ataendana na kasi ya Mkoa huyo,ambapo Rais ametekeleza kwa kumteuwa Mh.Gambo ambaye vijana wa Arusha wanaamini watafanya nae kazi na atataendana na kasi ya siasa za mkoa wa Arusha.

Itakumbukwa hivi karibuni UVCCM Mkoa wa Arusha,wakishirikiana na DC wa wakati huo Mrisho Gambo na kwa msaada wa mfanyabiashara maarufu na kada wa CCM waliungana katika kumuomba Rais kuivunja halmashauri ya Jiji la Arusha inayoongozwa na CHADEMA kutokana na kile walichosema ni kushindwa kwa uongozi huo wa upinzani kuongoza Jiji hilo.

Ole Sabaya anasema kuondoka kwa Mh.Ntibenda kutaihuisha Jumuiya hiyo ktk jiji la Arusha ambayo kwa uongozi wa Ntibenda ilianza kuzorota kwa RC huyo kujiweka kando nao.Lakini kwa uteuzi wa kijana Gambo sasa Jumuiya inaenda kuwa imara na thabiti,pia wamemtuhumu Ntibenda kuzembea ktk swala la ulinzi na Usalama kiasi kwamba ndani ya muda mfupi,shule kadhaa katika mkoa wa Arusha zilichomwa moto.
 
This will takes us about 100+ years to have what we call human development.
 
Back
Top Bottom