Nilikuwa nanunua fufu pale mataani, nikiwa nasubiri chenji yangu, nikamuona mwanamke anatembea na mtoto lakini mtoto anatembea kwa kasi kuliko mama yake. Ghafla mwanamke akapaza sauti akasema... “Degree!! Ningoje!”
Kwa kweli nilishangaa sana kusikia hilo jina. Ili kutuliza shauku yangu, nikamsogelea yule mama nikamuuliza, “Mama, mbona unamwita huyu mtoto mdogo Degree?” Mama akacheka kisha akaniambia, “Mwanangu, nilimtuma binti yangu chuo kikuu, na hiki ndicho alichoniletea nyumbani!”