Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,929
- 828,581
Zipo taarifa za uhakika kuwa katika jitihada za vyombo vyetu kutafuta ushahidi, vinatumia mateso na udhalilishaji (torture) ili kuwalazimisha watuhumiwa waseme ukweli. Baadhi ya mbinu wanazotumia ni:
- kuwavua nguzo zote watuhumiwa
-Kuwalawiti au kuwafira
-kuwapiga picha
-kuwaunguza kwa pasi za umene
-kuwapiga korodani (wanaume) na matiti (wanawake)
-kuwaninginiza kwenye kamba kichwa chini na miguu juu
-kuwalisha vinyesi na mikojo yao nk
Kwa picha zinazoonekana, inaonyesha kuna ukweli. Kwa simulizi za waliokutwa na mambo hayo, pia kuna ukweli. Wakati hayo yanatokea, mahakama ziko kimya na viongozi wetu wako kimya. Vitendo hivi vinavunja katiba, sheria na haki za binadamu.
Serikali zetu zinatumia fedha nyingi kusomesha wana usalama wetu ili wajifunze kupata ushahidi bila kutesa na kutweza utu wa binadamu yeyote. Vitendo hivi vinafanya iwe vigumu kwa wana diplomasia wetu kulitetea taifa mbele ya jumuia ya kimataifa. Matokeo yake, wana diplomasia wetu wanaonekana vichekesho, waongo na wababaishaji.
Tume ya HAKI JINAI ilitoa ushahidi wa haya mambo na kushauri hatua za kufanya. Tuheshimu hiyo ripoti. Hatuwezi kuwa na mifumo miwili sambamba ya utoaji haki nchini.
Mateso kwa watuhumiwa ni kielekezo kibaya cha serikali yoyote. Tuone aibu kufira ili kupata ushahidi. Ushahidi haufichwi kwenye kinyeo😓😭😭
Kichaka cha mbinu hii ni sheria inayowapa kinga watesaji. Sheria hii inastawisha uvivu wa kufikiri katika vyombo vyetu.
HATA GUANTAMANO WAMEACHA.
- kuwavua nguzo zote watuhumiwa
-Kuwalawiti au kuwafira
-kuwapiga picha
-kuwaunguza kwa pasi za umene
-kuwapiga korodani (wanaume) na matiti (wanawake)
-kuwaninginiza kwenye kamba kichwa chini na miguu juu
-kuwalisha vinyesi na mikojo yao nk
Kwa picha zinazoonekana, inaonyesha kuna ukweli. Kwa simulizi za waliokutwa na mambo hayo, pia kuna ukweli. Wakati hayo yanatokea, mahakama ziko kimya na viongozi wetu wako kimya. Vitendo hivi vinavunja katiba, sheria na haki za binadamu.
Serikali zetu zinatumia fedha nyingi kusomesha wana usalama wetu ili wajifunze kupata ushahidi bila kutesa na kutweza utu wa binadamu yeyote. Vitendo hivi vinafanya iwe vigumu kwa wana diplomasia wetu kulitetea taifa mbele ya jumuia ya kimataifa. Matokeo yake, wana diplomasia wetu wanaonekana vichekesho, waongo na wababaishaji.
Tume ya HAKI JINAI ilitoa ushahidi wa haya mambo na kushauri hatua za kufanya. Tuheshimu hiyo ripoti. Hatuwezi kuwa na mifumo miwili sambamba ya utoaji haki nchini.
Mateso kwa watuhumiwa ni kielekezo kibaya cha serikali yoyote. Tuone aibu kufira ili kupata ushahidi. Ushahidi haufichwi kwenye kinyeo😓😭😭
Kichaka cha mbinu hii ni sheria inayowapa kinga watesaji. Sheria hii inastawisha uvivu wa kufikiri katika vyombo vyetu.
HATA GUANTAMANO WAMEACHA.