Utenguzi na uteuzi huu haujaleta Hasara?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,301
33,920
Tarehe 7/7/2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania aliteua Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa, miji na wilaya wapatao 185. Kati ya hao 120 walikuwa ni wapya wakati 65 wakiwa ni wa zamani. Wale waliokuwa wamefikia umri wa kustaafu walistaafu lakini wale waliokuwa hawajafikia umri wa kustaafu walielekezwa kuripoti kwa Maafisa Tawala wa mikoa waliyopo.

Swali langu kama taifa tumepata hasara kiasi gani kwa kuwa na watu wanaolipwa mshahara bila ya kuwa na kazi maalum ya kufanya? Lakini pia wapo vijana wengine wakiwa na miaka chini ya 40 wakiteuliwa kuwa Wakurugenzi jambo ambalo litaleta shida huko mbele ya safari.

Hawa vijana walioteuliwa kushika nafasi za Uafisa uandamizi (Senior Officer) maana yake wataanza mishahara yao kwenye ngazi hiyo na hakuna jinsi ya kuwashusha labda wawe wamefanya makosa makubwa sana ya kimaadili.

Maana yake kama wangeteuliwa watu ambao walikuwa kwenye utumishi wa umma kwa muda mrefu, ingekuwa ni nafuu kwa nchi kwani wasingekaa sana kwenye nafasi hizo au za juu yake. Kuna wengine hawajawahi hata kuwa wakuu wa idara wala vitengo lakini wamepewa nafasi hizo za uafisa uandamizi. Maana yake itachukua muda mrefu sana kuwalipa wakiwa kwenye nafasi hizo za uandamizi kuliko kama walioteuliwa wangekuwa ni watu ambao angalau wamedumu kwenye utumishi umma kwa muda mrefu na wanaelekea kustaafu.
 
Ndio maana matumiz yamepanda kutoka bilioni 520 mpaka 570 kwa malipo ya mshahara hali ya kuwa tumeondoa wafanyakazi hewa 16000.badala ya kushuka yamepanda. kwahiyo tumetengeneza wafanyakaz hewa wengine tena wenye mishahara mikubwa
 
Ndio maana matumiz yamepanda kutoka bilioni 520 mpaka 570 kwa malipo ya mshahara hali ya kuwa tumeondoa wafanyakazi hewa 16000.badala ya kushuka yamepanda. kwahiyo tumetengeneza wafanyakaz hewa wengine tena wenye mishahara mikubwa
Kuna watu walidhani kwamba wale wakurugenzi waliotenguliwa wamefukuzwa kazi, kumbe wameondolewa tu kwenye nyadhifa zao lakini bado ni waajiriwa wa serikali lakini wasio na kazi ya kufanya!!
 
Kuna watu walidhani kwamba wale wakurugenzi waliotenguliwa wamefukuzwa kazi, kumbe wameondolewa tu kwenye nyadhifa zao lakini bado ni waajiriwa wa serikali lakini wasio na kazi ya kufanya!!
JAMANI HAWA WAKURUGENZI,MADC,MARC TULIKUWA TUNAWALALAMIKIA SANA KWA KUJIFANYA MIUNGU WATU.JE MLITAKA WABAKI PALEPALE KISA KUSAVE COSTS??
 
JAMANI HAWA WAKURUGENZI,MADC,MARC TULIKUWA TUNAWALALAMIKIA SANA KWA KUJIFANYA MIUNGU WATU.JE MLITAKA WABAKI PALEPALE KISA KUSAVE COSTS??
Gharama ya kuwa nao bila ya kuwa na kazi ya kufanya nani analipa. Halafu unadhani hao walioteuliwa hawatakuwa miungu watu kama mfumo wa kuwepo kwao hautabadilishwa?
 
Ameondoa watumishi halafu ametengeneza watumishi hewa, na hii ndo imesababisha ashindwe hata kuajiri maana tayari ananutirir wa watu wanao lipwa mishara bila ya kufanya kazi. Nitaunga mkono juhudi zako za kupambana na ufisadi pekee lakini mengine jitathimini.
 
Ameondoa watumishi halafu ametengeneza watumishi hewa, na hii ndo imesababisha ashindwe hata kuajiri maana tayari ananutirir wa watu wanao lipwa mishara bila ya kufanya kazi. Nitaunga mkono juhudi zako za kupambana na ufisadi pekee lakini mengine jitathimini.
Mtu anaamka asubuhi anakwenda kwa RAS anaripoti anapitia kununua Gazeti anarudi nyumbani, mwisho wa mwezi analipwa!!
 
Mkurugenzi aliyetenguliwa uteuzi wake wa hapa Iringa Manispaa bwana Ahmad Sawa CCM walimshutumu sana kwamba alimsadia Msigwa "kuiba" kura mpaka mgombea wao Fredrick Mwakalebela pamoja na wagombea wao udiwani kwenye Kata 14 kati ya Kata 18 kushindwa uchaguzi. Wenye kuwajua CCM walivyo tukajua Sawa hana maisha marefu kwenye nafasi yake, ndivyo ilivyotokea, ametenguliwa!!
 
Back
Top Bottom