Utata Kuhusu Taarifa Tuzo Za Mandela, 2017

Utata Kuhusu Taarifa Tuzo Za Mandela, 2017

CHA The GREAT

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2010
Posts
651
Reaction score
854
Kuna taarifa zimeenea kuanzia jana kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John P. Magufuli ametunukiwa tuzo ya amani na taasisi ya Nelson Mandela. Mbali na Rais Magufli wengine waliotunukiwa tuzo toka taasisi hiyo ni pamoja na Pierre Nkurunzinza ambaye ni Rais wa Burundi na Uhuru Kenyatta.

Kuna mashaka na taarifa hiyo kwa sababu zifuatazo kama zilivyoainishwa:

Kwanza, chanzo cha taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa facebook, ni chanzo ambacho hakijahakikiwa (verified) kama ilivyo vyanzo vingi vya kuaminika.

Pili, hakuna chombo kingine cha habari kilichoripoti habari hiyo licha ya umuhimu wake.

Tatu, website: www.institutmandela.com ambayo ndiyo inayoonesha kuhusiana kwa ukaribu na tuzo za taasisi ya Mandela, haina taarifa kama hiyo kuhusiana na utolewaji wa tuzo hizo.

Nne, kwa mara ya mwisho, tuzo hizo zilitolewa mwezi November, 2017. Inakuwa vigumu kuamini kwamba taasisi moja inaweza kutoa tuzo mara mbili kwa mwaka huo huo (mtanisahihisha kama nakosea).

Kama kuna mtu ana chanzo cha kuaminika na atuletee hapa ili kuondoa sintofahamu hii kwa ajili ya kutoa taarifa zilizo sahihi na zisizo na mashaka.

Tukio la wanahabari wa TBC miezi kadhaa iliyopita kutangaza habari ya uzushi kwamba, Rais Donald Trump amesifu jitihada za Rais Magufuli, zinafanya sintofahamu hii kuibuka kutokana na kutokuonekana kwenye vyombo vya habari vingine.
 
Gazeti la daily nation la Kenya limeripoti tuzo hizo kama ni uongo basi east Africa nzima imetekwa, tusubiri tu uthibitisho kutoka kwa tasisi husika otherwise tukae kimya
 
Hata ilipofikia majira yale ya kuzaliwa Masihi na tazama kuhani mkuu alipanda madhabahuni kuhubiri kama ilivyo desturi

Huku akiwa amejawa ujasiri na nguvu toka kwa bwana akasema ewe mfalme simama utubu kwa kuwa umewafanyia watu taifa lako machukizo makubwa mbele za uso wa Mungu
Wenye haki umewatia jeraha wasionda njia uiendayo umewasota jela na taifa lote limejaa hofu

Ndipo wale makada wakachukizwa sana wakasemezana imempasa hadhabu huyu kuhani

Basi wakapanga ni kwa jinsi gani wamkamate wampeleke barazani kwa watesaji kumshtaki kwa nini na kwa amri ya nani aseme mfalme atubu je haoni anatia najisi siasa na dini

Habari hiyo ikaenea pande zote za nchi hata nchi ya ugenini wakajitokeza makuhani kila kona ya nchi hata pande zile za ziwa wakapaza sauti zao juu ya makada wakisema mababu zetu walichanganya siasa na nyie makada hamkupinga je leo imekuwa haramu

Kakobe 17: 25-31
 
Gazeti la daily nation la Kenya limeripoti tuzo hizo kama ni uongo basi east Africa nzima imetekwa, tusubiri tu uthibitisho kutoka kwa tasisi husika otherwise tukae kimya
Link tafadhali, ili kujiridhisha na kufunga mjadala.
 
kama hyo tuzo ipo basi wanaoitoa na wanaoipokea wote ni wehu !!!!
 
Gazeti la daily nation la Kenya limeripoti tuzo hizo kama ni uongo basi east Africa nzima imetekwa, tusubiri tu uthibitisho kutoka kwa tasisi husika otherwise tukae kimya

Tunaomba 'link' ya hiyo Daily Nation. Maana nimeenda kwenye hiyo tovuti yao, hakuna kitu kama hicho. Sanasana vyanzo vingine visivyoaminika, vinakupa hata link ya video ila uki-play, unaambiwa 'video not available'.
 
Hata ilipofikia majira yale ya kuzaliwa Masihi na tazama kuhani mkuu alipanda madhabahuni kuhubiri kama ilivyo desturi

Huku akiwa amejawa ujasiri na nguvu toka kwa bwana akasema ewe mfalme simama utubu kwa kuwa umewafanyia watu taifa lako machukizo makubwa mbele za uso wa Mungu
Wenye haki umewatia jeraha wasionda njia uiendayo umewasota jela na taifa lote limejaa hofu

Ndipo wale makada wakachukizwa sana wakasemezana imempasa hadhabu huyu kuhani

Basi wakapanga ni kwa jinsi gani wamkamate wampeleke barazani kwa watesaji kumshtaki kwa nini na kwa amri ya nani aseme mfalme atubu je haoni anatia najisi siasa na dini

Habari hiyo ikaenea pande zote za nchi hata nchi ya ugenini wakajitokeza makuhani kila kona ya nchi hata pande zile za ziwa wakapaza sauti zao juu ya makada wakisema mababu zetu walichanganya siasa na nyie makada hamkupinga je leo imekuwa haramu

Kakobe 17: 25-31

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha!
 
599932225074e475c146a3f1ad01c8eb.jpg
 
Hata ilipofikia majira yale ya kuzaliwa Masihi na tazama kuhani mkuu alipanda madhabahuni kuhubiri kama ilivyo desturi

Huku akiwa amejawa ujasiri na nguvu toka kwa bwana akasema ewe mfalme simama utubu kwa kuwa umewafanyia watu taifa lako machukizo makubwa mbele za uso wa Mungu
Wenye haki umewatia jeraha wasionda njia uiendayo umewasota jela na taifa lote limejaa hofu

Ndipo wale makada wakachukizwa sana wakasemezana imempasa hadhabu huyu kuhani

Basi wakapanga ni kwa jinsi gani wamkamate wampeleke barazani kwa watesaji kumshtaki kwa nini na kwa amri ya nani aseme mfalme atubu je haoni anatia najisi siasa na dini

Habari hiyo ikaenea pande zote za nchi hata nchi ya ugenini wakajitokeza makuhani kila kona ya nchi hata pande zile za ziwa wakapaza sauti zao juu ya makada wakisema mababu zetu walichanganya siasa na nyie makada hamkupinga je leo imekuwa haramu

Kakobe 17: 25-31
Well said
 
Magufuli anapenda sifa kupita maelezo.
Mkimuhakikishia kuwa akisaula hadharani mtamsifi kwa nderemo na vifijo ninauhakika atazivulia jukwaani.
Hahahaha....watu mna matusi sana..
 
Back
Top Bottom