Wakuu naombeni maelekezo juu ya hili, mimi nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni binafsi baadae nikaacha kwa hiari yangu, kwenye account yangu ya NSSF kuna kiasi changu kadhaa cha pesa, sasa nahitaji nijue nifuate utaratibu gani ili kuipata, na naweza kuipata ndani ya muda gani kama nikianza mchakato??
Zamani tulikuwa tunawasilisha barua ya kutoka kwa mwajiri wako ulikotoka ya kuacha au kuachishwa kazi,
ukiacha kuna barua unamwandikia mwajiri na yeye anakujibu. Au ukifukuzwa kuna barua unapewa na mwajiri.
Walikuwa wanashauri usubiri miezi 6 ili kuona kama utapata ajira nyingine.
Hiyo barua ndo unaipeleka NSSF nao wanakupa fomu ambazo unampelekea mwajiri wako,
ambaye anakujazia kuonyesha alivyokuchangia kwa kuonyesha namba za lisiti za mlipo aliyopelekea michango
yako. Hiyo fomu ikishajazwa unairudisha NSSF wanakwambia muda wa kusubiri ili malipo yako yawe yameandaliwa.
Huo muda ukifika unaenda unapewa cheki yako.
Baada ya zile figisu za yule mkurugenzi aliyetumbuliwa na mh.JPM na sheria kandamizi
zilizotungwa baada ya hapo,sijui taratibu kama zimebadilika au bado ni zile zile.
Mimi kwa utaratibu wa hapo juu nilifanikiwa kuchukua mafao yangu mara mbili,
kabla ya kufikisha umri wa miaka 45.na nikiri kwamba utaratibu ule ulikuwa unasaidia sana
kwa wapambanaji tunaobebwa na juhudi zetu binafsi.