Sauti za Wananchi
Senior Member
- Sep 2, 2014
- 113
- 138
Utapiamlo ni miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili Tanzania. Kati ya mwaka 2000 na 2010, zaidi ya watoto 600,000 wenye umri chini ya miaka 5 wanakisiwa kufa kwa kukosa lishe ya kutosha. Takwimu zinaonesha pia 60% ya watoto wa maeneo Mikoa yenye kiwango kikubwa cha uzalishaji wa chakula nchini ikiwemo Iringa na Kagera ndiyo inayoongoza kwa kiwango cha juu cha watoto wenye utapiamlo na udumavu katika umri wa chini ya miaka 5.
Taasisi ya Twaweza imefanya utafiti unaolenga kuonesha uhusiano kati ya utapiamlo na matokeo ya kujifunza uliofanywa mwaka 2015 kati ya mwezi Oktoba na Desemba katika kaya zaidi ya 60,000.
Ripoti ya utafiti huo itazinduliwa siku ya Alhamisi tarehe 22 Desemba 2016 kuanzia saa 8:00 hadi 10:00 mchana katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), School of Education kwenye semina ya JiElimishe iliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Twaweza.
Taasisi ya Twaweza imefanya utafiti unaolenga kuonesha uhusiano kati ya utapiamlo na matokeo ya kujifunza uliofanywa mwaka 2015 kati ya mwezi Oktoba na Desemba katika kaya zaidi ya 60,000.
Ripoti ya utafiti huo itazinduliwa siku ya Alhamisi tarehe 22 Desemba 2016 kuanzia saa 8:00 hadi 10:00 mchana katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), School of Education kwenye semina ya JiElimishe iliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Twaweza.