Utapeli wa 'Kamata Mpunga' ya Vodacom

Utapeli wa 'Kamata Mpunga' ya Vodacom

Eruukada

Member
Joined
Aug 22, 2016
Posts
9
Reaction score
13
Hapo nyuma niliandika kuhusu michezo ya fedha ya makampuni ya simu, nikasema nitaendelea kutafuta ukweli kama wanaanchi wanaibwa ama serikali inaibiwa ama vyote viwili


Maswali ya kujiuliza:-

1. Unaulizwa swali ; timu ya taifa ya wanaume ya tanzania inaitwaje 1)Twiga stars, 2)Taifa stars . Unajibu 2, wanakutumia meseji wanasema umekosea,
unajiuliza kweli huu ni mchezo halali au la?

2. Unatumiwa meseji ya swali unaamuwa kutokujibu, voda wanakutumia meseji wanasema umepatia, we ni mkali kweli unajiuliza nimepatia nini wakati sijajibu?

3. Ukijiunga na bando alafu ukawa huna hela kwenye simu maswali yanakuja kidogo kidogo ukiweka hela maswali yanakuja mara nyingi, unajiuliza huu ni mchezo halali au la?

4. Maswali yanajirudia mara kwa mara , unajiuliza huu ni mchezo halali au la?

Je Gaming board of Tanzania wanafuatilia michezo hii ama hawajali wananchi wanavyoumizwa au ni kazi ya TCRA?

Je hela inayopatikanika inajulikana ni shilingi ngapi na ni kweli wananchi wanashinda na wanapewa hela kulinganisha na mapato wanayopata au ni siri ya voda wenyewe?

Je serikali wanapata kodi kutokana na makusanyo haya au wanatiwa upofu na kodi ya matumizi ya simu ya kawaida wanayopewa? Kwasababu aviusiani kabisa

Huu ni muendelezo...

Voda wana wateja million 6 nchi nzima, tuchukuwe namba ndogo kabisa ya watu 100,000 kwa siku ndio wanacheza hii ni 1.6% ya wateja wa voda

Piga Hesabu: 100,000 x 200/TSh = 20,000,000/TSh kwa siku
20,000,000/TSh x 30 siku = 600,000,000/TSh kwa mwezi



This is a serious amount of money one can make out of poor Tanzanian citizens, and guess what! The game is on for three to four months or so.

The funny thing is that this Mega companies are already making a lot of profit from extremely high rate sms, data and voice tariffs but they don’t have any sympathy on continue milking cash out of poor me and you by deceiving us wit these kind of tricks and unsurprising the government is quiet. Until we have regulators who are committed to working for the public we will always going to be on the losing side

Remember: “HEADS THEY WIN, TAILS WE LOSE”
 
wajinga ndiyo waliwao.
Salio lako likisha kwisha hawakutumii tena Maswali.

Ukiwekatu salio meseji kibao na vijiswali vya kijinga Sms 1 wanakula 150 mpo? "Vodacom kazi ni kwako"
 
Sinaga time na hiyo michezo Yao, siku zote wanaopenda vya dezo ndiyo wanaumizwa.
 
Mi nataka tu waniambie hizo milioni 100 nashinda lini
 
aiseee kumbe wengi wanaliwa hivi! mi nawatia hasara daily yaan sms yao ikiingia nafuta bila hata ya kusoma
 
Huu ni utapeli wa hali ya juu, nilishakataa kushiriki mambo ya ovyo kama haya. Mamlaka zinazohusika sidhani kama wanafuatilia zaidi ya kulala fofofo.
 
Mimi namba wanayonitumia nayo nimeiblock kabisa wanochowaza kutvuna tuu hawa
 
I think it is beyond that... na baadhi ya wa Tanzania wanaelewa kinachoendelea na wanafaidi nalo. It is totally bullshit!
 
Kwani mmelazimishwa kujibu hizo maswali, tamaa tuu zinawasumbua, na wanajua mlivo maskini wa kutambua thus why wanatumia hio nafasi.
 
Ha ha ha leo ukijibu maswali hya utaingia kwenye droo ya kesho kushinda 20mil c danganyiki mm
 
yaan kuna ile ya namba 075....... mmiliki umechaguliwa kushiriki katika draw ya TZS 5........ Yaan SIIPENDI nataman hata niiblock narudia tena hyo msg SIIPENDI kwan nlisema nataka kushiriki
 
''...katika kipindi cha utawala wangu hakuna hela za bure bure tu, hela itapatikana kwa kufanya shughuli au kazi halali tu..'' Mh. John P Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
wajinga ndiyo waliwao.
Salio lako likisha kwisha hawakutumii tena Maswali.

Ukiwekatu salio meseji kibao na vijiswali vya kijinga Sms 1 wanakula 150 mpo? "Vodacom kazi ni kwako"
Huwa nikiona msg zao nafuta haraka lakini hawasikii yaani ni ving'ang'anizi balaa wataendelea kutuma tu
 
Back
Top Bottom