Utapeli wa ajira umekithiri, Serikali ipo wapi?

Kajeba

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2020
Posts
1,126
Reaction score
2,537
Wakuu,

Huku walimu wahitimu na wale wa kada ya afya wakifurahia ajira zilizotangazwa leo na TAMISEMI nayo matapeli yameshangilia haswa.

Katika kipindi hiki nasikitika vijana wengi wanaenda kulizwa vipesa vyao kwa kudanganywa kwamba ajira hizi zinatolewa kwa connection ambapo huihitajika walipie pesa kwa ahadi ya kupangwa kituo cha kazi, hakika mtaliwa pesa zenu bure .

Awamu hii hakuna connection, usikubali kuliwa na mwisho ukose kazi.
 
Kama hujui serikali ilipo basi ww ni raia wa kisengerema
Najua ndio maana nimesema Hela unafikiri bila kuliwa kidogo utapata kwanza majina yameshaandaliwa hizo application ni fake tu na bahati na sibu kama kubet
 
Usihofu,hiyo angalao ni tiba ya kisaikolojia japo ya muda kwa watafuta ajira waliojikatia tamaa kiasi cha kutamani kujiua,hivyo toeni tiba,japo hata tiba feki,kuwaponya hawa ndugu zetu japo kwa dakika chache tu😂😂
 
Najua ndio maana nimesema Hela unafikiri bila kuliwa kidogo utapata kwanza majina yameshaandaliwa hizo application ni fake tu na bahati na sibu kama kubet
Hizi kauli zinakatisha tamaa, lakini vijana wafanye application mimi nilipata kazi mapema tu bila connection yoyote.
 
Endelea kujidanganya, awamu pekee ambayo haikuhitaji connection ni awamu ya tano ambapo hata mkurugenzi aliogopa lakini sio Sasa.
 
Yaani hela zitapigwa sana,na mbaya zaidi watu waliopata kwa koneksheni awamu iliyopita, watatumika kama mfano. Watu wataongeza magari Tuombe tu. Mimi nimesoma English language kama teaching subject chuoni na nimemaliza 2016, ila kila nikiomba, sipatagi, hawa wa 2020-2021 na sasa 2022, utashangaa wanachukuliwa na huwa wanachukuliwa, kwakweli inafikirisha sana. Umri unazidi kwenda, biashara zikianzishwa, hazinawiri, zinakufa. Inachanganya sana, na kinacholeta mkanganyiko ni pale unapotolewa mfano wa mtu aliyepata ajira kwa koneksheni na ni wa 2020, inasikitisha sana, tunabaki dillema, tufanyaje, ila ndiyo hivyo, ngoja tuombe tena.
 
Pole mkuu
 
Ifikie hatua serikali nayo ipumzishwe

Ifikirie Madai ya CAG

May mosi

Ifikirie habari ya mwalimu au nesi mtarajiwa kwenye ajira , shule zinawasaidiaje
 
Usijali mkuu, ntaomba tena na nimesisitizwa niombe tena, asubuhi hii, nimepigiwa simu na wanaonifahamu, kunisihi nisiache kuomba, wanasema huwezi kujua yawezekana nikapata. Ila inakatisha tamaa sana, 2016 ni parefu sana na bado uhakika wa kupata ni mdogo, japo wanasema watu wa kiingereza ni moja ya walengwa, unaweza ukashangaa mimi wa 2016 nikaachwa, halafu mwenye sifa kama yangu aliyemaliza 2022 anaingia kwenye mfumo. Inasikitisha sana,hadi wengine tunawaza kua labda kuna kosa ambalo Mungu tulishamkosea, adhabu yake ndiyo hii tunaitumikia.
Pole mkuu
 
Dah pole sana mkuu, lakini usiache kuomba mkuu. Mungu ni mwema all the time ninaamini this time utapata, USIACHE.
 
Pole sana mkuu
Omba huku ukiwa na matumaini haba
 
Mmeelekezwa jinsi ya kujisajili, jinsi ya kuomba afu bado unatapeliwa
 
Shida ipo apa na sometime hua mtua anaeza kua amemaliza 2020 kwenye mkeka akaonekana na anaandikwa kamaliza 2016 lakin wanaomfaham wanajua kamaliza lin. Inasikitisha sana
 
Karbia nusu ya ajira wanachaguliwa kwa connection , nusu inayobaki mnawekewa gombania goli watoto wa maskini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…