Utani wa ndani: Serikali ya CCM kama 'Big Brother'

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,137
17,908
Serikali ya awamu ya tano,chini ya Rais Magufuli,sasa imekuwa kama Jumba la Bigbrother. Kila juma la kazi,kuna mtumishi asiye mbishi anatumbuliwa,yaani kuachishwa kazi. Watumishi sasa hawana amani. Wanafanya kazi,si kwa weledi tena,ila kwa woga na mashaka.

Kila mtumishi anafanya kazi kwa woga unaompelekea kuwa mchonganishi na wa kuwasukumia wengine 'jumba bovu'. Watumishi sasa wanalazimika kujipendekeza hata kwa kuumiza ili wabaki salama. Serikali ya kuchongea na kuchongewa kwa ajili ya kutumbuliwa. Bigbrother.

Baada ya Kabwe,Simba na Kairuki kuaga kwenye Jumba la Bigbrother la awamu ya tano,watumishi wengine wanaendelea kupigiwa kura za ima kutoka au kubaki. Rais anapaswa kuwa makini na taarifa za majipu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Hizi propaganda na unafiki zilikuwa hot deal wakati wa utawala wa awamu ya nne.

Hii ni awamu nyingine na mnatakiwa mbadilishe aina ya unafiki na propaganda otherwise, you are just digging your own political grave.

Bado mnaishi jana wakati serikali inaishi leo.
 
Serikal ipo macho nyie ACHENI kupotosha watu.. Waliotufikisha hapa acha watumbuliwe tumwache raisi afanye kazi yake
 
Baada ya Kabwe,Simba na Kairuki kuaga kwenye Jumba la Bigbrother la awamu ya tano,watumishi wengine wanaendelea kupigiwa kura za ima kutoka au kubaki. Rais anapaswa kuwa makini na taarifa za majipu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Uko sahihi kabisa! Ni heri hata akapoteza Miezi miwili pale anapoletewa taarifa kabla hajafanya maamuzi! Bado miaka minne na ushehe ya kufanya kazi na watumishi wa Umma na anawahitaji-kauli ya JK ya akilini zako Changanya na za Mbayuwayu ni afya ikatumika. Lakini bado naamini kwa Issue kama hii ya Kairuki unaagiza Mkataba wake uliletwe siku mmoja tu inatosha kupata jibu-maana kama ameusaini maana yake kakubalia mshahara husika ,lakini kama hakusaini maana yake simfanyakazi halali-simple and Clear!
 
Serikali ya awamu ya tano,chini ya Rais Magufuli,sasa imekuwa kama Jumba la Bigbrother. Kila juma la kazi,kuna mtumishi asiye mbishi anatumbuliwa,yaani kuachishwa kazi. Watumishi sasa hawana amani. Wanafanya kazi,si kwa weledi tena,ila kwa woga na mashaka.

Kila mtumishi anafanya kazi kwa woga unaompelekea kuwa mchonganishi na wa kuwasukumia wengine 'jumba bovu'. Watumishi sasa wanalazimika kujipendekeza hata kwa kuumiza ili wabaki salama. Serikali ya kuchongea na kuchongewa kwa ajili ya kutumbuliwa. Bigbrother.

Baada ya Kabwe,Simba na Kairuki kuaga kwenye Jumba la Bigbrother la awamu ya tano,watumishi wengine wanaendelea kupigiwa kura za ima kutoka au kubaki. Rais anapaswa kuwa makini na taarifa za majipu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Wenye wasi wasi wa kutumbuliwa ni wale ambao ofisi zao zina ufisadi na ile tabia ya ukosefu wa uaminifu. Lakini wale waadilifu ambao walishazoea kuishi ndani ya mipaka ya mishahara yao, wala hawana hofu ya kutumbuliwa.
 
Kila cku anaangalia atapata kick kwa kumtumbua nani?watz washamuelewa mchezo anaoucheza,yaaani unamtega mtu ili uje umtumbue hadharani eti ili usifiwe?
 
Back
Top Bottom