Utani sio kwenye mapenzi jamani

Utani sio kwenye mapenzi jamani

Duh hii chai imewekwa muarobaini.

Mtu anaweza kukaa na mke miaka mitatu asijue huo ushabiki wa mkewe kwa simba au yanga????!!!!
 
Duuh!!!!!!!!!!!! Umri si kipimo cha ustaarabu ila ustaarabu ni matendo yenye umri.
 
Kuna rafiki yangu mmoja ambaye nilikuwa namheshimu na kumtumia kama mshauri wangu, lakini juzi kati amefanya kitendo ambacho kimenifanya nimuone hafai.

Heshima yangu nilikuwa nampa kwa kuwa alikuwa ameweza kuwa makini katika kuchagua mwanamke wa kuoa, na si hilo tu bali hata ndoa yake ilikuwa ni mfano kwa wengine kwani wameweza kuishi miaka zaidi ya mitatu ndani ya ndoa bila kuwa na ugomvi wa aina yoyote ile.

Chakushangaza eti juzi ilikuwa kama utani tu, yeye ni shabiki wa Yanga, sasa akamuuliza mkewe, "hivi mke wangu, wewe ni shabiki wa timu gani hapa Tanzania." mke akasema "mimi ni shabiki wa Simba",

Mmewe huku akionyesha sura ya kukasirika akamwambia "naomba ubebe kila kilicho chako uende kwenu isipokuwa wanangu tu."tukajua utani lakini mpaka hivi sasa wameshatengana mke yuko kwao na jamaa ndo amekomaa anasema hamtaki tena.

Hayatuhusu. Purely, private business. Mpelekee shigongo wa global publishers hii habari yako.
 
daaah nakulaani kwa kunipotezea muda wangu. sikupaswa hata kujaribu kutaka kujaribu kuwaza kufungua huu uzi kwa maana ni uzi kimeo sijapata kuona
 
Back
Top Bottom