Utani sio kwenye mapenzi jamani

Utani sio kwenye mapenzi jamani

youngsharo

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2015
Posts
2,491
Reaction score
500
Kuna rafiki yangu mmoja ambaye nilikuwa namheshimu na kumtumia kama mshauri wangu, lakini juzi kati amefanya kitendo ambacho kimenifanya nimuone hafai.

Heshima yangu nilikuwa nampa kwa kuwa alikuwa ameweza kuwa makini katika kuchagua mwanamke wa kuoa, na si hilo tu bali hata ndoa yake ilikuwa ni mfano kwa wengine kwani wameweza kuishi miaka zaidi ya mitatu ndani ya ndoa bila kuwa na ugomvi wa aina yoyote ile.

Chakushangaza eti juzi ilikuwa kama utani tu, yeye ni shabiki wa Yanga, sasa akamuuliza mkewe, "hivi mke wangu, wewe ni shabiki wa timu gani hapa Tanzania." mke akasema "mimi ni shabiki wa Simba",

Mmewe huku akionyesha sura ya kukasirika akamwambia "naomba ubebe kila kilicho chako uende kwenu isipokuwa wanangu tu."tukajua utani lakini mpaka hivi sasa wameshatengana mke yuko kwao na jamaa ndo amekomaa anasema hamtaki tena.
 
Hapo inawezakana mwanamke ndo alikuwa amebeba mji Kwa kunyenyekea na kufanya kila linalomfurahisha mwanaume so kujibu yeye yupo timu tofauti tayari kaona ameanza kumdharau. Huyo mwanaume hampendi kabisa.
 
Hapo inawezakana mwanamke ndo alikuwa amebeba mji Kwa kunyenyekea na kufanya kila linalomfurahisha mwanaume so kujibu yeye yupo timu tofauti tayari kaona ameanza kumdharau. Huyo mwanaume hampendi kabisa.

na ndo wengi tumefikiria hivyo.
 
Mtu makini anawezaje kufanya maanuzi kama hayo. Inawezekana huyo mwanamke ndo alikua brave na ndie alieifikisha hiyo ndoa yao hapo ilipoishia.
 
Mtu makini anawezaje kufanya maamuzi kama hayo. Inawezekana huyo mwanamke ndo alikua na busara na ndie alieifikisha hiyo ndoa yao hapo ilipoishia.
 
Back
Top Bottom