ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,115
- 49,835
Utafiti mpya uliofanywa na Chuo Kikuu cha Essex na Chuo Kikuu cha Adelaide nchini Australia umebainisha kuwa kukodi nyumba kutoka kwa mtu kibinafsi au kampuni binafsi kunaweza kumsababisha mtu kuzeeka haraka kwa asilimia 100 kulinganisha na wanaomiliki nyumba zao wenyewe.
Njia hili imeonekana kuwa na athari zaidi katika kuzeesha mtu kuliko ile ya kutumia sigara na ukosefu wa ajira ambayo awali iliyokuwa ikijulikana kama kichocheo kikubwa zaidi cha uzee.
Katika mambo yaliyoainishwa na utafiti huo yanayopelekea hali ya uzee kwa wapangaji wa nyumba binafsi ni kudaiwa kodi za nyumba mara kwa mara, kupangisha nyumba zilizo katika maneneo yenye viwango vya juu vya uchafuzi wa mazingira au nyumba zilizopo katika mazingira yenye usumbufu mwingi.
Utafiti huo unaeleza uzee huo husababishwa na msongo wa mawazo, jambo linalopelekea mwili kuzeeka upesi.
Utafiti huo umebainisha pia kuwa wale waishio katika makazi ya kijamii ambayo hayamilikiwi na mtu binafsi, kampuni binafsi au wanaoishi katika nyumba wanazozimiliki wenyewe hawakumbani na hali ya kuzeeka upesi kwa kuwa makazi hayo huwa yenye gharama nafuu na yenye ulinzi wa wa uhakika.
Utafiti huo uliendeshwa kwa kutumia taarifa za kiafya zilizokusanywa kutoka kwa watu 1,420 walioishi katikal kaya mbalimbali huko nchini uingereza.
Utafiti huo umechapishwa katika jarida la 'Epidemology' na afya ya jamii [Epidemiology and Community Health].
TBC
====
Angalizo.
Hii ni huko Ulaya ambako gharama za maisha ziko Juu na mtu mmoja mmoja kujenga ni Mtihani.
Njia hili imeonekana kuwa na athari zaidi katika kuzeesha mtu kuliko ile ya kutumia sigara na ukosefu wa ajira ambayo awali iliyokuwa ikijulikana kama kichocheo kikubwa zaidi cha uzee.
Katika mambo yaliyoainishwa na utafiti huo yanayopelekea hali ya uzee kwa wapangaji wa nyumba binafsi ni kudaiwa kodi za nyumba mara kwa mara, kupangisha nyumba zilizo katika maneneo yenye viwango vya juu vya uchafuzi wa mazingira au nyumba zilizopo katika mazingira yenye usumbufu mwingi.
Utafiti huo unaeleza uzee huo husababishwa na msongo wa mawazo, jambo linalopelekea mwili kuzeeka upesi.
Utafiti huo umebainisha pia kuwa wale waishio katika makazi ya kijamii ambayo hayamilikiwi na mtu binafsi, kampuni binafsi au wanaoishi katika nyumba wanazozimiliki wenyewe hawakumbani na hali ya kuzeeka upesi kwa kuwa makazi hayo huwa yenye gharama nafuu na yenye ulinzi wa wa uhakika.
Utafiti huo uliendeshwa kwa kutumia taarifa za kiafya zilizokusanywa kutoka kwa watu 1,420 walioishi katikal kaya mbalimbali huko nchini uingereza.
Utafiti huo umechapishwa katika jarida la 'Epidemology' na afya ya jamii [Epidemiology and Community Health].
TBC
====
Angalizo.
Hii ni huko Ulaya ambako gharama za maisha ziko Juu na mtu mmoja mmoja kujenga ni Mtihani.