UTAFITI: Athari wapatazo watoto baada ya mzazi kunywa Pombe anapokuwa Mjauzito

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,446
7,817
Moja kati ya vitu ambavyo wajawazito hawaruhusiwi kabisa kuvifanya ni pamoja na kunywa pombe ya aina yoyote ile ingawa hata hivyo wapo baadhi ya wanawake huamini mvinyo ‘wine’ huwa haina madhara kwa ujauzito hasa kama mjamzito atainywa kwa kiwango kidogo sana.

Katika utafiti mpya uliofanywa Marekani siku za karibuni umeonesha kuna madhara makubwa kwa watoto wanaozaliwa endapo mama zao walijihusisha na pombe ya aina yoyote na kiwango chochote hivyo wameshauri wanawake wasitumie kabisa vileo vyovyote wakiwa na ujauzito.

Miongoni mwa athari zilizotajwa na watafiti hao ambazo husababishwa na ulevi wakati wa ujauzito ni pamoja na mtoto kuzaliwa kabla ya wakati wake au ujauzito kuharibika, mtoto kuzaliwa na uzito mdogo, mtoto kuzaliwa na matatizo ya moyo, ini au mifupa.

Pia mtoto kuwa mzito katika kujifunza, matatizo ya kuona na kusikia, kichwa kikubwa au kuwa na uso wenye matatizo na mengineyo.

Kwa hisani ya Millard Ayo
 
Zamani mama zetu walipiga beer na ujauzito tena wakiamini Guinness inaongeza damu na tukizaliwa wazima
 
The most prominent effect of alcohol to the baby ni Fetal Alcohol Syndrome
 
Moja kati ya vitu ambavyo wajawazito hawaruhusiwi kabisa kuvifanya ni pamoja na kunywa pombe ya aina yoyote ile ingawa hata hivyo wapo baadhi ya wanawake huamini mvinyo ‘wine’ huwa haina madhara kwa ujauzito hasa kama mjamzito atainywa kwa kiwango kidogo sana.

Katika utafiti mpya uliofanywa Marekani siku za karibuni umeonesha kuna madhara makubwa kwa watoto wanaozaliwa endapo mama zao walijihusisha na pombe ya aina yoyote na kiwango chochote hivyo wameshauri wanawake wasitumie kabisa vileo vyovyote wakiwa na ujauzito.

Miongoni mwa athari zilizotajwa na watafiti hao ambazo husababishwa na ulevi wakati wa ujauzito ni pamoja na mtoto kuzaliwa kabla ya wakati wake au ujauzito kuharibika, mtoto kuzaliwa na uzito mdogo, mtoto kuzaliwa na matatizo ya moyo, ini au mifupa.

Pia mtoto kuwa mzito katika kujifunza, matatizo ya kuona na kusikia, kichwa kikubwa au kuwa na uso wenye matatizo na mengineyo.

Kwa hisani ya Millard Ayo
Teratogens ndo watoto watakaozaliwa, watoto walio na mutation fulani ya viungo vya mwili.
 
Back
Top Bottom