Utabiri wangu mechi ya Simba na Yanga, tarehe 8 Machi

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,638
697,929
Nimechungulia anga la SIMBA kuna ung'avu mkubwa na nyota nne zinawaka kuzunguka kichwa cha mnyama SIMBA akiwa kakanyaga zulia jekundu na kuzingirwa na mataa yanayomeremeta, mekundu. Kwa upande wa YANGA kuna utusitusi na hali ya kufifia.

Huku vitu kama nyota vikiwa vimepoteza nuru. Kuna nyota mbili zinawaka na kufiifia kama umeme wa single phase wenye load iliyozidiwa pembezoni na chini kuna rangi ya khaki kama njano na ni kavu kama jangwani.

Chochote anachotaka kukifanya YANGA kwenye hiyo ndoto kinapata msaada na mwanga toka upande wa SIMBA.

Tafsiri yake ni ninini?
  • SIMBA atatawala mchezo mwanzo mwisho kasoro dakika chache tu za mwisho.
  • SIMBA itatoka kifua mbele kwa kulipenya lango la YANGA mara NNE.
  • Yanga watabahatika kupata kifuta machozi cha bao mbili au moja. Kama nia mbili, kila kipindi kitapata moja.
Kama huamini utabiri huu au unabisha njoo na wako lakini usiwe wa kufoji. Ama kaa tulia tusubiri kipenga cha mwisho tarehe hiyo ya 8.3.2020.

Jr
 
Back
Top Bottom