Mkuu Brightman,
Nafikiri hoja yako ina mashiko ingawa humu jamvini wengi wetu tunatanguiza hisia za uchama zaidi kuliko ukweli uliopo. Tunasahau kuwa hata tuweke hisia mbele kiasi gani ukweli utabaki daima
labda ambacho hukufanya ni kueleza vipi umefikia kiwango hicho cha ushindi pamoja na na kufafanua ni sababu zipi ambzo zingepelekea kuwepo kwa hali ambayo itakipelekea CCM kuibuka na ushindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa mbao kwa mtazamo wangu kama matokeo yatakuwa kama alivyo ni ishara tosha kuwa mwaka 2015 wapinzani watapigwa mchana kweupe.
Uchaguzi huu ni muhimu zaidi kwa kuwa unajenga msingi wa uongozi wa ndani ya chama na ngazi ya serikali na hivyo kuwa na nafasi nzuri ya kuweka mikakati ya kuwezesha chama kupata ushindi, hivyo chama ambacho kitapata nafasi katik ngazi hii ambayo ndiyo iliyo karibu zaidi na wananchi, kina nfasi kubwa ya kuibuka na ushindi.
jambo moja nimebaini, taarifa ya idadi ya watu walijiandikisha kupiga kura za uchaguzi wa serikali za mita katika mkoa wa dar es salaam pekee, zinaonyesha kuwa ni asilimia 42 pekee ya wapiga kura ndio waliojiandikisha! kuna baadhi ya watu humu ndani hawakujiandikisha wakidai uchaguzi huu sio wa muhimu, wako busy N.K
jambo lenyewe ni hili, watanzania wanodai kuunga mkono vyama vya upinzani hufanya hivyo kwa mneo ya vijiweni na au kwenye mtandao lakini HAWAJITOI katika shughuli mbalimbali za vyama wanavyodai kuviunga mkono. Inawezekna unafahamu mifano mingi lakini kuna hili suala la waliojitokeza kuomba nafasi za uongozi kupitia Ukawa,nimebaini "wengi" hawana mvuto kwa wapiga kura kwa kuwa wale ambao wangetarajiwa kugombea wamebaki nyuma wakisubiri watu wengine walete mabadiliko yanayotarajiwa.
Inawezekana wagombea hao "wakashinda", lakini hii inaweza kusababishwa na "li-upepo" kuwa wananchi wanataka mabadiliko ya viongozi kutoka vyama vingine lakini sio mvuto kwa wapiga kura. Hata mapigamzi yanayodaiwa kuwa sababu ya wagombea wa Ukawa kuzuiwa yanayotoana na sababu iele ile ya wengi kuunga mkono vyama vya upinzani kwa maneno na sio vitendo!
Jambo moja na dhahiri viongozi wabovu huingia madarakani kutokana na wewe au mimi kushindwa kujitokeza kupiga kura au kupigiwa kura.