Utabiri: Bernard Membe hutaweza kutikisa hata unywele wa Rais Magufuli

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,738
15,209
Amani iwe nanyi.

Ikiwa leo tarehe 16/7/2020 Waziri wa zamani wa mambo ya nje Mh Bernard Membe anatangazwa rasmi kujiunga na chama cha ACT Wazalendo ambapo bila shaka atapewa ridhaa ya kuwania urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ifikapo mwezi October mwaka huu hivyo kuwa mshindani wa Rais Magufuli.

Kwa kumwangalia akiwa anaongea Bernard Membe inaonyesha ana uchungu sana na anataka kubadilisha kitu kwenye nchi hii, pia inaonyesha ndani ya moyo wake ameapa iwe mvua au jua lazima awe rais wa Tanzania!

Si jambo baya wala si uvunjifu wa katiba kuota kuwa rais wa Tanzania kama anavyofanya Membe lakini unatakiwa ujitafakari ni wakati gani hiyo ndoto unatakiwa uiote.

Kama mwaka 2015 Membe aliweza kupenya tano bora na Magufuli na akashindwa mbele ya kaka yake Jakaya Kikwete basi kwenye uchaguzi wa mwaka huu 2020 hataweza kumtikisa Magufuli hata kipande cha unywele wake. Inawezekana kweli wapo vigogo wanaomshawishi na kumhakikishia Membe kuwa atashinda urais hapo October na kutawazwa kuwa rais wa Tanzania lakini naomba nimwambie ukweli hao vigogo wamelenga kumlia hela zake tu.

Membe kaa utulie ulee wajukuu ,habari za kuwa rais wa Tanzania zimeshapita na hazitakurudia tena.
 
Mgombea Tundu A.Lissu, kule Membe ,kule Nyarandu, kule Zito, Kule Seifu n.k


Alafu sababu Tume sio huru, Tume ya Jiwe, Mnaiba Kura.

Safari hiii tunaingia Barabarani kwa wizi wenu wa Kura.
 
Mbona alimfukuza kwenye Chama baada ya kuonyesha nia ya kuchukua form ya urais?
 
Kazi zingine zinaruhusu kuingia tu hakuna kutoka sasa kwa nini huyu karuhusiwa kutoka? Mashaka yetu ndipo yanaanzia hapooooooo, huenda ni mpango mkakati
 
Mgombea Tundu A.Lissu, kule Membe ,kule Nyarandu, kule Zito, Kule Seifu n.k


Alafu sababu Tume sio huru, Tume ya Jiwe, Mnaiba Kura.

Safari hiii tunaingia Barabarani kwa wizi wenu wa Kura.
Unaongea haya huku umejifungia ndani kabisa tena na makomeo sebuleni kwa shemeji yako huku wao wakiwa wameenda kazini
 
Tupe historian ni lini na wapi magufuli aliwahi shinda,?? Toka enzi za marehemu kabuye mpaka enzi za lowasa magu hajawahi shindana akashinda
 
Amani iwe nanyi.

Ikiwa leo tarehe 16/7/2020 Waziri wa zamani wa mambo ya nje Mh Bernard Membe anatangazwa rasmi kujiunga na chama cha ACT Wazalendo ambapo bila shaka atapewa ridhaa ya kuwania urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ifikapo mwezi October mwaka huu hivyo kuwa mshindani wa Rais Magufuli.

Kwa kumwangalia akiwa anaongea Bernard Membe inaonyesha ana uchungu sana na anataka kubadilisha kitu kwenye nchi hii, pia inaonyesha ndani ya moyo wake ameapa iwe mvua au jua lazima awe rais wa Tanzania!

Si jambo baya wala si uvunjifu wa katiba kuota kuwa rais wa Tanzania kama anavyofanya Membe lakini unatakiwa ujitafakari ni wakati gani hiyo ndoto unatakiwa uiote.

Kama mwaka 2015 Membe aliweza kupenya tano bora na Magufuli na akashindwa mbele ya kaka yake Jakaya Kikwete basi kwenye uchaguzi wa mwaka huu 2020 hataweza kumtikisa Magufuli hata kipande cha unywele wake. Inawezekana kweli wapo vigogo wanaomshawishi na kumhakikishia Membe kuwa atashinda urais hapo October na kutawazwa kuwa rais wa Tanzania lakini naomba nimwambie ukweli hao vigogo wamelenga kumlia hela zake tu.

Membe kaa utulie ulee wajukuu ,habari za kuwa rais wa Tanzania zimeshapita na hazitakurudia tena.
Weka tume huru tuone kama ni kweli hata mshinda
 
kila kitu kinawezekana hapa duniani, hata mataifa ambayo vyama vikongwe vilipoteza nafasi yao walipoteza kimasihara masihara tu bila hata kutarajia.
 
Siasa na hususan ushindi WA kura ni matokeo ya mipango kisayansi, siyo hisia. Membe ni CCM insider; atawagawanya vipande. Tusubiri.
 
Mgombea Tundu A.Lissu, kule Membe ,kule Nyarandu, kule Zito, Kule Seifu n.k


Alafu sababu Tume sio huru, Tume ya Jiwe, Mnaiba Kura.

Safari hiii tunaingia Barabarani kwa wizi wenu wa Kura.
Anza kabisa kutokavunasubiriwa huku barabarani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom