k majaliwa
Senior Member
- Jul 31, 2017
- 140
- 186
Wanajukwaa heri ya mwaka mpya,
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Kuna kipindi niliwahi kuandika jinsi nilivyoumizwa kimapenzi, nashukuru kwa ushauri mzuri wa wataalum wa saikolojia wa JF maana walinishauri vyema na hakika ushauri wao umenitoa kwenye majonzi.
Sintakusahau nguriti na kapiti mmefanyika baraka sana kwangu, najiona nina thamani kubwa tofauti na awali.
Nichukue wasaa huu kuwasihi watu wanaopitia wakati mgumu kimapenzi au walikwishapitia lakini wakashindwa kurudi kawaida.
Tumeumbwa na tabia tofauti na kamwe hatuwezi kufanana suala la kuachwa au kukataliwa halijaanza leo ni jambo ambalo lipo na lilikuwepo na litaendelea kuwepo kwasababu mapenzi yana mambo mengi.
Usikubali kuumia wala kuendelea kuumia wakati aliyekuacha anandelea kula raha na mpenzi wake mpya.
Kama umeachwa ona ni jambo la kawaida hata kama umeumia.
Fanya yafuatayo kutokuruhusu kuumia zaidi.
Kubali matokeo, uambie moyo wako hili haliwezekani tena.
Usijiruhusu kumuwaza tena. Futa kila kinachokuletea kumbukumbu ya mapenzi yenu ya nyuma.
Jaribu kuwaeleza watu unao waamini usikae nalo moyoni peke yako litakutesa.
Usikurupuke kuanzisha mahusiano mapya wakat bado unaugulia maumivu.
Jiweke busy na mambo mengine.
Tumia muda wako kutafakari ukuu wa Mungu na kumshukuru kwani huenda umeepushwa na mabalaa.
Acha kuwaza kujiua. Jione kuwa unathamani kubwa machoni pa Mungu ndiyo maana Mungu amekuweka duniani.
Ukifanya hayo machache na mengine ambao wataalum wataongezea itakusaidia kuondoa machungu kwa haraka na kukufanya ufurahie maisha tena.
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Kuna kipindi niliwahi kuandika jinsi nilivyoumizwa kimapenzi, nashukuru kwa ushauri mzuri wa wataalum wa saikolojia wa JF maana walinishauri vyema na hakika ushauri wao umenitoa kwenye majonzi.
Sintakusahau nguriti na kapiti mmefanyika baraka sana kwangu, najiona nina thamani kubwa tofauti na awali.
Nichukue wasaa huu kuwasihi watu wanaopitia wakati mgumu kimapenzi au walikwishapitia lakini wakashindwa kurudi kawaida.
Tumeumbwa na tabia tofauti na kamwe hatuwezi kufanana suala la kuachwa au kukataliwa halijaanza leo ni jambo ambalo lipo na lilikuwepo na litaendelea kuwepo kwasababu mapenzi yana mambo mengi.
Usikubali kuumia wala kuendelea kuumia wakati aliyekuacha anandelea kula raha na mpenzi wake mpya.
Kama umeachwa ona ni jambo la kawaida hata kama umeumia.
Fanya yafuatayo kutokuruhusu kuumia zaidi.
Kubali matokeo, uambie moyo wako hili haliwezekani tena.
Usijiruhusu kumuwaza tena. Futa kila kinachokuletea kumbukumbu ya mapenzi yenu ya nyuma.
Jaribu kuwaeleza watu unao waamini usikae nalo moyoni peke yako litakutesa.
Usikurupuke kuanzisha mahusiano mapya wakat bado unaugulia maumivu.
Jiweke busy na mambo mengine.
Tumia muda wako kutafakari ukuu wa Mungu na kumshukuru kwani huenda umeepushwa na mabalaa.
Acha kuwaza kujiua. Jione kuwa unathamani kubwa machoni pa Mungu ndiyo maana Mungu amekuweka duniani.
Ukifanya hayo machache na mengine ambao wataalum wataongezea itakusaidia kuondoa machungu kwa haraka na kukufanya ufurahie maisha tena.