Usiolewe na mwanaume masikini

Usiolewe na mwanaume masikini

Sham777

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2019
Posts
335
Reaction score
840
Nimeona baazi ya Wanawake wengi wana penda ku rush mambo ili ku prove kwa wenzao hasa kwenye ishu za mahusiano..
Tumeona dada na wadogo zetu Wameolewa na wanaume wasio na kipato cha kueleweka ili mradi tu wa Prove kwa wenzao kuwa nao wameolewa wapo katika ndoa na mwisho wake umekuwa mbaya kutokana na changamoto mbaya za maisha wanazo pitia katika ndoa zao.

Wew sio mwanamke wa Ndoto zake.. Wanaume wengi tuna wanawake wa ndoto zetu ila kutokana na kuwa nakipato kidogo tunashindwa fikia malengo ya kuwa na wanawake wa ndoto zetu na kuchukua mwanamke yoyote ambae ni cheap tunae weza kum afford.. Na ndio maana tunaona wanaume wengi wenye ndoa zao wanaendelea kucheat hasa pale wanapo pata kipato kila siku anabadirisha wanawake.. Ivyo kaa tambua wew sio mwanamke wa ndoto zake Muda utazungumza pindi atakapo anza kupata vijicent na kukuonesha tabia zake alizo zi hide kipindi hana kitu..

Smart Women Marry for Money
Wanawake ambao huchagua wenzi wao wa maisha walio na pesa wanaendelea vizuri kuliko wenzao ambao hawafanyi ivyo. Wanawake hawa wanajua kuwa ili ndoa iweze kujengwa lazima fedha iwepo na jukumu kubwa katika uwezekano wa ndoa kudum ni la mwanaume. Mwanamke alie kamilika kifikra na amekomaa kiakili anahitaji Mwanaume aliye na hela. je unajiona wapi katika miaka 2? Miaka 5? Miaka 10? Jibu hilo litaamua mwenendo wa Mahusiano yako.

NB
Neno langu sio Sheria endapo utaona ushauri wangu sio mzuri chukulia kama ni utani tu..
 
Umasikini wa Nini? Wa sperm, wa upendo, wa uvumilivu, wa nguvu za kiume, wa kipato au wa Nini?

Umasikini wa kipato Ni rahisi Sana kuushinda hasa mkiwa mwapendana kwa dhati.

Vichwa viwili vitafanya Mambo makubwa.

Lakini mumeo akiwa ni tajiri wa mali na ni masikini wa upendo, utajuta kuzaliwa. Utanyanyaswa wewe, utadharaulika wewe, utatukanwa wewe na wazazi wako, Tena atakwambia kabisa hapa umefuata mali tu wewe.

Ushauri wangu ni huu. Kama unataka kuoa, muombe Mungu akupatie mwenzi wa kufanana naye, mwenye upendo na atakayeweza kukuvumilia katika yote.

Mkweli asiye mnafiki, mzandiki Wala mtu wa shirki
 
Mwanamke atafutaye "green pasture" yaani "gold digger" mwisho wake ni ujane wakujitakia, kama akibahatika kuhonga sheria isimutie hatiani, mifano ipo mingi.
 
Hili Jambo rahisi Sana. Wazazi wanakuchagulia mchumba, mnaoana, mnazaa watoto, mnagombana mnapatana, maisha yanaendelea Hadi mola awatenganishe.

Tatizo mnapenda umagharibi Sana wakati mnaishi kusini mean jangwa la Sahara.
 
Ingawa inapingwa ila kuna kitu kina ukweli ndani yake. Mfano wanaume kubadilika akipata pesa. Ndoa kusambaratika baada ya pesa kuwa nyingi ndani.

Na mostly kuoa mtu kutokana na sababu kadhaa sio kwa kuwa amempenda. .....Though haiapply kwa wote
 
Tunarudi Palepale Haya mambo hayana formula.
Ingawa inapingwa ila kuna kitu kina ukweli ndani yake. Mfano wanaume kubadilika akipata pesa. Ndoa kusambaratika baada ya pesa kuwa nyingi ndani. Na mostly kuoa mtu kutokana na sababu kadhaa sio kwa kuwa amempenda. .....Though haiapply kwa wote
 
Waweza kuolewa na mwanaume wa ndoto yako lakn ghafla bin vuuuuuuu.....no money tena msela ndii kafirisika nafkri ndoto zako zitakuwa zimeishia apo na inabd ulale tena uote mwenye ela mwngine...
 
Ni kweli kila mwanamke ana ndoto ya kuolewa na mwanaume mwenye pesa.
Shida inakuja hapa, wanaume tupo wachache, na wenye pesa tupo wachache zaidi.
Anyway life goes on..
 
Baazi=baadhi
ukimaliza hapo endelea hivi usipende ku GENERALIZE MAMBO !!!
Unaanzaje kuisemea nafsi ya mwenzako??
 
Jaïna shida endelea kuwaza kuwa SMART GIRL MARRY FOR MONEY, Lwakatare yupo atakutumia kisulisuli.
Hebu ongea n'a mama ako Alimpendea Nini baba ako.
 
Mleta Mada upo sahihiii kabisa, kuna mizigo mingine huwa inacross mbele yangu wallah huwa nashindwa kuisemesha kwasababu yauchumi so huwa naangalia wanyonge wenzangu
 
Back
Top Bottom