David Harvey
JF-Expert Member
- Jul 17, 2014
- 3,119
- 6,783
Habarini wapendwa?
Miaka mitatu iliyopita nilileta thread ikisema "usioe mwanamke masikini"
Baada miezi 3 kuoa ndugu wa mwanamke walihamia nyumbani kwangu kutoka kijijini kwao walikuwa 11 wakiume walikuwa 7 wakike 4.
Kiukweli nilikwazika sana na ujio wao ukiangalia dar maisha ni tough kibaya zaidi walikuwa wanakula mno kama fundukwi mpka nikaja jf kuomba ushauri.
Ila kuna wadogo wawili wa mke wangu nilihamua kujitolea kuwasomesha nilikuwa nawaonea huruma sana..
Ila niwaombe radhi sana mashemeji zangu niliwakosea sana nilikuwa nawatukana sana moyoni ila leo hii mmekuwa baraka kwangu mmekuwa msaada mkubwa sana kwangu.
Nina miaka miwili tangu nifukuzwe kazi ila hawa mashemeji niliowachukia leo hii ndio wanaonipiga tafu wanasomesha watoto wangu 3.wawili wapo marian girls na mmoja yupo anasoma tusiime nadhani wote mnajua ada na gharama ya hizo shule
Lakini leo hii wale niliowasaidia kwa chuki pasipo wao kujua kama nawachukia leo ndio wanao nisaidia na wana pesa c mchezo ingalikuwa hawajasoma.Wale mashemeji wadogo niliowasomesha hivi sasa wapo muhas mwaka 3.
NB: Usichukie masikini wasaidie kama una uwezo waheshimu ndugu wa mke wako maana haujui kesho yako. Nisameheni wote niliowakwaza kwa ile thread yangu miaka 3 iliyopita.
Jumapili njema
Miaka mitatu iliyopita nilileta thread ikisema "usioe mwanamke masikini"
Baada miezi 3 kuoa ndugu wa mwanamke walihamia nyumbani kwangu kutoka kijijini kwao walikuwa 11 wakiume walikuwa 7 wakike 4.
Kiukweli nilikwazika sana na ujio wao ukiangalia dar maisha ni tough kibaya zaidi walikuwa wanakula mno kama fundukwi mpka nikaja jf kuomba ushauri.
Ila kuna wadogo wawili wa mke wangu nilihamua kujitolea kuwasomesha nilikuwa nawaonea huruma sana..
Ila niwaombe radhi sana mashemeji zangu niliwakosea sana nilikuwa nawatukana sana moyoni ila leo hii mmekuwa baraka kwangu mmekuwa msaada mkubwa sana kwangu.
Nina miaka miwili tangu nifukuzwe kazi ila hawa mashemeji niliowachukia leo hii ndio wanaonipiga tafu wanasomesha watoto wangu 3.wawili wapo marian girls na mmoja yupo anasoma tusiime nadhani wote mnajua ada na gharama ya hizo shule
Lakini leo hii wale niliowasaidia kwa chuki pasipo wao kujua kama nawachukia leo ndio wanao nisaidia na wana pesa c mchezo ingalikuwa hawajasoma.Wale mashemeji wadogo niliowasomesha hivi sasa wapo muhas mwaka 3.
NB: Usichukie masikini wasaidie kama una uwezo waheshimu ndugu wa mke wako maana haujui kesho yako. Nisameheni wote niliowakwaza kwa ile thread yangu miaka 3 iliyopita.
Jumapili njema
