Usinyooshe mkono ukiwa hujui wapi Mbingu ilipoanguka

Usinyooshe mkono ukiwa hujui wapi Mbingu ilipoanguka

Paspii0

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2020
Posts
638
Reaction score
1,038
Nature is always brutal si kwa sababu inachukia, bali kwa kuwa haijifunzi. Maji hayakubali kubebwa, bali hubeba.

Mwanga haufuati giza, bali hulivunja.
Waliokaa kimya ndani ya kelele wamezoea kutafuna pumzi badala ya mikate. Nguzo za uhai hazisimamishwi na sarafu, bali na kivuli cha dhamira iliyonyamazishwa.

Tunatembea kwenye sakafu ya uwongo, tukiamini ni ardhi ya matumaini. Kama mwamba huogopi upepo, kwa nini utu uinamie kivuli cha wenye kutwezwa?

Tusipoamka, tutalala hadi ndoto zituamue kwa kilio cha kimya.
 
Lecture ngumu ngoja nipate maji ya mende. Nimemkumbuka jamaa yangu kipindi cha representation anazitwanga kwanza basi akija kurepresent anatamba pale mbele km vile kakamata kibaka.
 
Yote ya yote tukimbizane na pesa wakuu
kwa wengine pesa ni taa bila mwelekeo,Wanaonekana wameshika dunia, kumbe wanakimbia kivuli chao kwa hakika Kuku mweupe huonekana mzuri, lakini mbele ya mganga… huwa hana bahati. Pesa si lolote bila mkondo.
 
Yote ni ubatili mtupu, Ni kama kutafuna upepo
Kutafuna upepo ni kazi ya yule asiyejua ladha, Maisha si kuhusu kiasi, ni kuhusu kiini. Wapo waliokusanya majumba, lakini roho zao hazina pa kukaa. Wapo waliopanda juu kwa maneno, lakini wakashushwa na ukimya wao wenyewe. Si kila atafunaye upepo yuko bure wengine wanafungua njia ya mawimbi mapya. Swali ni unatafuna kwa nini?
 
Hapo sentensi ya mwisho, funguka zaidi
namaanisha tutagundua kuwa kelele tulizopiga zilikuwa nyimbo tu za kuchombeza za usingizi. Tulisikia, lakini hatukusikiliza. Tuliona, lakini tulifumba macho kwa makusudi. Wakati tunadhani tunacheza karata za ujanja, kumbe tulikuwa tunajichezea nafsi. Maisha hayaombi ruhusa yanatuandika kwa wino wa matendo yetu wenyewe.
 
Kutafuna upepo ni kazi ya yule asiyejua ladha, Maisha si kuhusu kiasi, ni kuhusu kiini. Wapo waliokusanya majumba, lakini roho zao hazina pa kukaa. Wapo waliopanda juu kwa maneno, lakini wakashushwa na ukimya wao wenyewe. Si kila atafunaye upepo yuko bure wengine wanafungua njia ya mawimbi mapya. Swali ni unatafuna kwa nini?
Yote yalikuwepo na yatapita
 
Back
Top Bottom