Usingizi wa UVCCM ndio chanzo cha matatizo ya CCM

EL MAGNIFICAL

JF-Expert Member
Jan 11, 2011
938
125
ndg wajumbe chama cha mapinduzi ni chama tawala hapa nchini, pamoja na kwamba ndicho chama kilichoshikilia usukani wa uongozi lakini kimekuwa kikikumbwa na lawama nyng sana kama tuhuma za ufisadi dhini ya viongozi wake wakubwa, kukosa majawabu ya matatizo ya wananchi, uongozi usiosimamia haki na mengineyo mengi. Imefikia hatua chama kimepewa majina mengi ya ajabu kama tafsili ya ccm, mfano chama cha magamba, chama cha majambazi, chama cha mafisadi nk. Na yote hii imetokana na hali halisi inayoendelea ndani ya system ya chama hiki tawala.
Kwanini nasema uvccm ndio chanzo ?
Japo siwezi sema wanahusika moja kwa moja ktk tuhuma hizo ila wao nitawalaumu kwa yafuatayo:
1.ktk jamii yoyote ile vijana ndio chachu ya maendeleo na mageuzi lakini imekuwa tofauti kwa uvccm kwani hawa ndugu zetu wanaonesha wameridhika na system ya utawala wao kwani kuna kipindi walidiriki hata kufanya fujo ili kuwatete baadhi ya mafisadi wasivuliwe nyazfa zao ktk chama na wakafanikiwa je kama hili liliwezekana kwann ktk mambo ya msingi uvccm wanalala ?
2. Viongozi wao wakubwa wamekuwa na tabia ya kuwasimamisha watoto zao ktk nafasi flan flan za kisiasa ile hali watoto hao wengne taaluma yao si siasa na wala hawana uwezo wala mvuto wa kisiasa mbona hamkemei haya ! Hamuoni mmesababisha chama chenu kubomoka kwa utawala huo wa kurisishana ?
3. Umoja wa vijana ktk chama chochote cha siasa ndio inatakiwa wawe kama kambi ya upinzani ndani ya chama kwa kukosoa mabaya na kujenga mazuri lakini imekuwa tofauti kwa uvccm. Kwani hata leo hii ukikaa na hawa ndugu wao watakwambia mwakyembe ndio ameibua ufisadi bila hata kujiuliza je hoja iliibuliwa na nani ?
Uvccm kwanini mmekuwa vijana wa ndio mzee ?
4. Kuwa na kundi kubwa ambalo ndani yake limekosa wazalendo, jamani uvccm jisafisheni ninyi kwanza mkiwa kama vijana ndipo muanze kuzalisha viongozi wazuri na waadirifu, atleast mukiendeleze chama chenu ila mkitaka na nyie mcopy na kupaste wafanyayo maboss wenu mtaujutia mda wenu.
Rai yangu kwa umoja wa vijana ktk vyama vingine vya upinzani MUONEKANO WA CCM leo hii kwenu liwe darasa ya kwamba kukosekana kwa watu wa kuikosoa ccm ndani ya familia yao leo hii ndio imefikia hapo ilipo.
Pia viongozi wa vyama watumieni vijana kufanya masahihisho na si kuwabana na kuwapuuza.
Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom